AN-NUUR
Na.185 Shawwal 1419, Januari 22 - 28, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
Mtambani wasema kamwe hawakubali pumbao la kisiasa

FFU watinga na kuondoka patupu

MAPEMA wiki hii historia ya nchi hii nusura igubikwe na doa jingine sawa na lile la Mwembechai, kufuatia jaribio la s zilipandisha mori na hisia kwa waumini hao ambapo imamu aliyesalisha Swala ya laasiri aliwataka waichukulie swala hiyo kuwa ni ya mwisho kabla ya mapambano kuanza ambayo yangeamua hali yao ya baadaye. 

"Ilikuwa kama majogoo yanayoangaliana kwa hasira na kisasi kabla ya kurukiana, mimi nilishangaa kama polisi wangelivamia basi ama ningekutwa gerezani, mochuari au hospitali", amedai kijana mmoja aliyetokea maeneo ya Mwananyamala. 

Kadri muda ulivyozidi kusonga mbele ndivyo waumini walivyozidi kumiminika mahali hapo. 

Katika hatua za awali za kutaka kuzuia Baraza hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Alfred Gewe inasemekana alifika Msikitini hapo na kutaka kuongea na Imamu. 

Hata hivyo, ilibidi aondoke kuepusha shari baada ya kujibiwa kwamba Mtambani hakuna Imamu kwani Imamu wake Mzee Chatta alishauliwa. 

Baadae aliwasili mkuu wa upelelezi wa mkoa (RSO) akiwa amevalia kanzu na kofia ambapo baada ya mazungumzo na Alhaj Hanzuruni Mungula, aliwaamuru polisi waondoke. 

AN-NUUR ilishuhudia mabasi madogo aina ya DCM yapatayo sita yakiwasili na kuteremsha waumini waliobeba mabango yanayoonyesha mahali wanapotokea. 

Akiwa katika harakati za kufuatilia kila tukio lililotokea mahali hapo, mwandishi alivamiwa na vijana watatu huku mmoja wapo uso ukiwa umezibwa na kitambaa cheupe kilichoachia sehemu ya macho tu. Vijana hao walimshuku mwandishi kuwa huenda ni mmoja wa "watafuta habari wa serikali.". Walimuamuru atulie mahali pamoja vinginevyo wangelimchukulia hatua. 

Hata hivyo jitihada za kujitambulisha zilifanikiwa kuwashawishi vijana hao ambao walionekana wako tayari kwa lolote. 

Kila aliyefika eneo hilo na kusimama kando alifuatiliwa na vijana hao kwa siri au kwa uwazi. Makachero waliofika mahali hapo walikuwa na wakati mgumu kimajukumu kutokana na ulinzi wa "para military" hao. 

Wakati wa onesho la mkanda wa Mauaji ya Mwembechai ulipowadia watu wote waliokuwa eneo hilo ikiwa ni pamoja na wakazi walio nyumba za jirani na msikiti huo walishonana mahali hapo kiasi cha kukanyagana. 

Waumini wengine walijazana juu ya jengo la msikiti linaloendelea kujengwa. 

Mkanda huo ulionekana kuvuta hisia za wengi hasa pale mmoja wa mapolisi walikuwa katika operesheni hiyo alipokuwa amelala chini akimlenga kijana mmoja ambaye baadaye alimfyatulia risasi na kumuua papo hapo. 

Sehemu nyingine iliyoamsha masikitiko ni pale polisi mmoja alipoamrisha "piga yule, mwongeze tena." 

Viongozi wa kamati iliyoandaa baraza hilo walifanya kazi ya ziada kuwanasihi waumini waliokuwa wakiangalia onesho hilo ili kuwatuliza kutokana na yale waliyokuwa wakiyashuhudia katika onesho hilo. 

"Haya ni yale yale ya Soweto wakati wa ubaguzi wa rangi Afrika kusini, alisema muumini mmoja aliyeonekana kujawa na hasira baada ya kuangalia mkanda huo. 

Hadi mwandishi anaondoka eneo hilo hapakuwa na tukio lolote lililoashiria kuvurugika kwa amani ukiondoa vitisho vya magari sita yaliyokuwa yakiranda eneo hilo kabla ya shughuli hiyo kuanza.

Juu
 

YALIYOMO
  

Tahariri
Fundisho toka Mtambani

Waislamu wataka serikali iwajibike

Serikali yakiri kupokea malalamiko ya Waislamu: Mkapa awataka Watanzania waepuke kubaguana

Mtambani wasema kamwe hawakubali pumbao la kisiasa

Maoni: Kweli ikisimama uongo hujitenga

MARADHI YA KISAIKOLOJIA:  TRANSVESTISM

Mjue Usama bin Ladin

Risala ya Waislamu katika Baraza la Idd  kwa Mgeni Rasmi Rais  Benjamin Mkapa

Wafanyakazi TANESCO waingiwa hofu ya wingu la udini

Hotuba ya Rais Mkapa kwenye Baraza la Idd Diamond Jubilee Jan. 19, 1999

Makala: Hotuba ya Mkapa, Magazeti ya Ruzuku na Waislamu
Na J. Hussein

Kutoka magazeti ya zamani: Washitakiwa walipelelezwa

Hivi siku ya ibada ni ipi?: Ijumaa, Jumamosi au Jumapili?
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu

'Msitarajie kupambana na adui kwa upanga wa Hamza'

Sasa ni kulishwa nguruwe kwa nguvu

Sayansi na Teknolojia
[KUPELEKA  FAX NCHI ZA NG'AMBO BURE!]

Masomo ya Dini ya Kiislamu

Barua za Wasomaji

Mashairi

Chakula na lishe
[Faida na  hasara za kupika chakula]
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita