|
Na. 052 Jumatano Juni 14 - 20, 2000 |
|
|
|
|
|
Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi watajwa
TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza majina ya wasimamizi wasidizi wakuu wa uchaguzi (Principal Assistant Returning Officers) kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu, ambapo Watanzania watapiga kura kuwachagua Rais wa Muungano, wabunge na madiwani. Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa na tume hiyo katika vyombo vya habari Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifanya kikao chake Juni 9 mwaka huu na kuwateua watumishi kutoka serikali kuu na serikali za mitaa kuwa wasimamizi wasidizi wakuu wa uchaguzi huo utakaovishirikisha vyam vingi vya siasa. Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa zaidi ya asilimia 80 ya wasimamizi hao wa uchaguzi wana majina yenye kuashiria kuwa ni wafuasi wa dini ya Kikristo. Orodha ya kwanza ya wasimamizi wakuu wa uchaguzi (Principal Returning Officers) iliyotangazwa miezi michache iliyopita ililalamikiwa na Waislamu kwa madai kuwa zaidi ya asilimia 90 ya walioteuliwa walikuwa ni Wakristo. Hata hivyo si tume ya uchaguzi wala serikali iliyodiriki kujibu kadai hayo ya Waislamu. Aidha, mara kadhaa, Rais Benjamin William Mkapa amekuwa akikemea udini hapa nchini. Hivi karibuni, akizungumza katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Mkapa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho tawala, alisema serikali yake haitavumilia ubaguzi wa raia kwa misingi ya dini, kabila au jinsia. Huko nyuma Waislamu wamewahi kupeleka kwa Rais
Mkapa madai yao yakiwemo ya kubaguliwa kwa msingi wa dini. Hata hivyo Waislamu
nchini wanadai kwamba malalamiko yao yamepuuzwa na Mhe. Rais.
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Mkapa, Karume wapewa tiketi za CCM kugombea urais Kufuatia
kukamatwa kwa Sheikh Mbukuzi na Ricco:
HABARI
Amiri Mbukuzi ahojiwa na polisi Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi watajwa USHAURI NASAHA
MAKALA
MAKALA
MAKALA
MAKALA
HOJA BINAFSI
Makala maalum ya Maulid
MAKALA
Habari za Kimataifaza Kimataifa Lishe
RIWAYA
MICHEZO
|
|
|
|
|