NASAHA
Na. 047 Jumatano Mei 10 - 16, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
HABARI 

Nchi wafadhili wataka upinzani, CCM yalalama 

NJIA pekee itakayoweza kuifanya Serikali iwajibike kwa wananchi wake ni kuwepo kwa upinzani wenye nguvu.

Kauli hiyo imetolewa na Profesa Palle Svensson wa chuo kikuu cha Arhus kilichoko nchini Denmark, wakati wa mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Philip Mangula yaliyofanyika Mei 8, jijini Dar es Salaam. 

Mtaalamu huyo yupo nchini kufuatilia maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, akiziwakilisha nchi wafadhili. 

Nchi hizo ni Sweden, Canada, Uingereza, Finland, Ireland, Norway, Uholanzi na Switzerland. 

Mwakilishi huyo wa nchi wafadhili pia alikutana na maafisa wa tume ya uchaguzi. 

Kwa kawaida katika nchi zenye vyama vya kisiasa vyenye nguvu, wananchi wanajulishwa udhaifu wa serikali iliyoko madarakani na hatimaye wanaiondoa serikali hiyo madarakani kwa njia ya uchaguzi, na kukiweka madarakani chama kingine. 

Kutokana na hali hiyo, baadhi ya serikali hasa katika nchi ambazo hazijali utawala wa kidemokrasia, zinavibana na kuvihujumu vyama vya upinzani ili visiwe na nguvu, na hatimae kudharauliwa na wananchi. 

Baadhi ya njia zinazotumika kuvihujumu na hatimaye kuvidhoofisha vyama vya upinzani ni pamoja na kuzuia mikutano ya wazi ya vyama vya upinzani, kuwakamata na kuwafungulia mashitaka viongozi wa upinzani, kuwatisha matajiri ili wasivisaidie vyama vya upinzani na mara nyingine hufikia hata kuwatisha na kuwanunua viongozi na wananchi. 

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Bw. Philip Mangula, akizungumza katika kikao hicho na Profesa Palle Svensson, alisema nchi wafadhili kuacha fikra alizoziita potofu kwamba uchaguzi wowote hapa nchini utakubaliwa tu kuwa umekuwa huru na wa haki ikiwa CCM itaondolewa madarakani. 

Bw.Mangula pia aliwaomba wafadhili waisaidie Tume ya Taifa ya Uchaguzi. "Ni vyema wafadhili waisaidie Tume ya Taifa ya Uchaguzi kujenga uwezo wa kutoa elimu ya uchaguzi kwa umma na kujenga uwezo wa kuendesha na kusimamia uchaguzi kwa ufanisi mkubwa zaidi ili uchaguzi uwe huru na haki", alisema katibu huyo wa CCM. 


Waislamu Musoma walalamika 

Mwandishi Wetu, Musoma

WAUMINI wa dini ya Kiislamu wilayani Musoma mjini wamemtumia barua Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba, kulalamikia kitendo cha mahakimu wa wilayani hapa kuwataka wavue kofia mahakamani wakati wa kutoa ushahidi au kuwachukulia dhamana watuhumiwa.

Katika barua hiyo ya tarehe Mosi Mei mwaka huu, yenye kumbukumbu Na. Vol.Bak/MB/16/3/292 iliyosainiwa na Bwana Nyamrasa Said, Waislamu wa mjini hapa wamedai kuwa hatua hii ya mahakama ni ya kuwadhalilisha wao na dini yao. 
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Mazingira ya uchaguzi huru na haki yasivurugwe

Wananchi washutumu vyombo vya habari

Lipumba awaambia wananchi wasibabaishwe na walioko madarakani

Wasomi SUA walaani ‘rushwa’ ya kisiasa

Polisi kataeni kutumiwa - Lipumba 

Maelfu ya tani za matunda yanaoza Tanga

Habari za ndani
Uondoeni ‘ukoloni’ wa CCM- Mbukuzi

MPASHO NASAHA
WABONGO HAWANA NYONGO !

HABARI
Nchi wafadhili wataka upinzani,  CCM yalalama

Waislamu Musoma walalamika

Habari za Kimataifa

Ushauri Nasaha
Jukumu la wazazi, walimu kwa wanafunzi wanaomaliza masomo

Makala
Madhara ya ulevi kwa binadamu

MAKALA
Sababu ‘1000’ kwanini tunataka CCM ing’oke madarakani - 6

MAKALA
Kiini macho cha msamaha wa deni

Kalamu ya Mwandish
Kama CUF ni chama cha Waislamu 
Jee, CCM ni chama cha Wakristo?

MAKALA
Chama cha Mapinduzi na sera za maendeleo (2)

RIWAYA
Mapinduzi ya fikra

Lishe
Jinsi ya kuzuia utapiamlo kwa wanawake

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Real Madrid yaingia fainali
  • Mapunda, Makoye hawafai timu ya Taifa - Kipingu
  • Tarimba ashinikizwa kujiuzulu Yanga

  •  

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita