NASAHA
Na. 047 Jumatano Mei 10 - 16, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Lipumba awaambia wananchi wasibabaishwe na walioko madarakani:
Wameshindwa miaka 40 hawataweza 5 ijayo

Na Mwandishi Wetu 

MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF) Mhe. Profesa Ibrahim Lipumba amewataka wananchi kutokubabishwa na wale walioko madarakani kuwa wanaweza kuwaletea maendeleo katika kipindi cha miaka mitano ijayo wakati wameshindwa kufanya hivyo kwa kipindicha miaka 40.

Mhe. Lipumba aliyasema hayo Mewi 6 na 7 mwaka huu alipokuwa akizungumza na mamia ya wananchi wa Mlandizi na Chalinze katika mikutano mwili tofauti ya chama hicho. 

Alisema kuwa kipindi cha miaka 40 ni kikubwa mno ambacho mtu anaweza kuzaa na kujukuu, lakini Chama Cha Mapinduzi na mzazi wake TANU vimeshindwa kufanya lolote katika kuleta maendeleo ya wananchi hadi kuitumbukiza nchi katkka umaskini uliokithiri. 

Alisema kuwa 1961 viongozi wa TANU waliwaahidi wananchi kuwa wangetumia muda wa miaka 10 tu kuleta maendeleo na maisha bora kwa wananchi zaidi ya maendeleo yaliyoletwa katika muda wa miaka 76 ya ukolohi wa Wajerumani na Waingereza. 

Baada ya miaka 40 ya uhuru, Mhe. Lipumba alisema, asilimia 50 ya Watanzania wanaishi katika maisha ya umasikini wa kutupwa, ambapo asilimia hiyo hiyo ya watoto wadogo chini ya umriwa miaka 5 wanautapiamlo. 

"Hali ya maradhi inatisha, malaria imeshakuwa sugu. Serikali ya Japan imetoa mabilioni ya shilingi katika kupambana na malaria, lakini fedha zimetafunwa na wenye meno", alisema Mhe.Lipumba. 

Alisema kuwa hali ya upatikanaji wa huduma muhimu katika nchi imekuwa ngumu, na akatolea mfano wa maji na elimu kukazia nukta hiyo. 

"Hivi sasa Watanzania zaidi ya milioni 2 wenye umri wa kujiunga na shule za msingi hawamo mashuleni. Katika kila vijana 100 ni vijana 70 tu ndio wako mashuleni. Na hata hao walioko mashuleni hawapati elimu yakufaa", alisema. 

Akizungumzia kuporomoka kwa sekta ya kilimo na biashara alisema kuwa wakati mbogamboga na matunda kama vile mabibo, embe na machungwa yana soko kubwa katika nchi za Ulaya na Marekani, hapa nchini bidhaa hizo zinaoza kwa kukosa soko na hivyo kuwakatisha tamaa wakulima. 

Aidha aliwataka wananchi nchini kuwa na msimamo wakupambana na udhalimu na kwamba wasiwe waoga, kwani hakuna jamii ya waoga ambayo imeweza kupambana na watawala wenye kuendeleza udhalimu juu ya raia zao. 

Aliwahimiza wananchi hao kuendelea kuhamasishana na kujitokeze kwa wingi kujiandikisha na hatimaye kupiga kura muda utakapofika, kwani kwa kuindoa CCM pekee ndio wanaweza kuondokana na madhila haya yanayowakabili. 

Mwenyekiti huyo wa CUF alimalizia kwa kusema, "Watanzania hatujamkosea Mungu, matatizo yetu ni matokeo ya sera mbovu na zisizotekelezeka za CCM." 
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Mazingira ya uchaguzi huru na haki yasivurugwe

Wananchi washutumu vyombo vya habari

Lipumba awaambia wananchi wasibabaishwe na walioko madarakani

Wasomi SUA walaani ‘rushwa’ ya kisiasa

Polisi kataeni kutumiwa - Lipumba 

Maelfu ya tani za matunda yanaoza Tanga

Habari za ndani
Uondoeni ‘ukoloni’ wa CCM- Mbukuzi

MPASHO NASAHA
WABONGO HAWANA NYONGO !

HABARI
Nchi wafadhili wataka upinzani,  CCM yalalama

Waislamu Musoma walalamika

Habari za Kimataifa

Ushauri Nasaha
Jukumu la wazazi, walimu kwa wanafunzi wanaomaliza masomo

Makala
Madhara ya ulevi kwa binadamu

MAKALA
Sababu ‘1000’ kwanini tunataka CCM ing’oke madarakani - 6

MAKALA
Kiini macho cha msamaha wa deni

Kalamu ya Mwandish
Kama CUF ni chama cha Waislamu 
Jee, CCM ni chama cha Wakristo?

MAKALA
Chama cha Mapinduzi na sera za maendeleo (2)

RIWAYA
Mapinduzi ya fikra

Lishe
Jinsi ya kuzuia utapiamlo kwa wanawake

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Real Madrid yaingia fainali
  • Mapunda, Makoye hawafai timu ya Taifa - Kipingu
  • Tarimba ashinikizwa kujiuzulu Yanga

  •  

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita