NASAHA
Na. 047 Jumatano Mei 10 - 16, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Polisi kataeni kutumiwa - Lipumba

Na Mwandishi Wetu 

MWENYEKITI wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba amelaani kitendo cha Polisi kutumika kuvuruga mikutano ya chama cha chake. Hayo aliyasema alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara mjini Chalinze mkoa wa Pwani Jumapili iliyopita, kufuatia kilichodaiwa Polisi kuzuia msafara wa wanachama wa CUF waliokuwa wakifuatana na mwenyekiti huyo katika ziara ya Mlandizi na Chalinze zilizofanyika Mei 6 na 7.

Imeelezwa kwamba katika msafara wa Mei 6, magari yaliyo wabeba wanachama na wapenzi wa CUF yalisimamishwa Kibaha Maili Moja, kwa madai mbali mbali ikiwemo magari kuchubuka rangi. 

Aidha katika msafara wa Mei 7 magari ya CUF yalizuiliwa katika eneo la Pingu, kilometa chache kabla ya kufika Chalinze takriban kwa zaidi ya masaa 7. 

Katika msafara huo ilidaiwa kwamba Polisi waliyasimamisha magari ya CUF kwa sababu kadhaa ikiwemo ya kukosa kibali cha kusafiri katika njia hiyo. 

Juhudi za viongozi wa CUF kutaka msafara huo uruhusiwe kuendelea na safari hazikufanikiwa na badala yake watu watano akiwemo kiongozi wa chama hicho, Bw. Akwilombe ambaye ni Mkurugenzi wa Vijana, walifunguliwa mashitaka, katika mahakama ya Wilaya, mjini Bagamoyo. 

Hata hivyo baadhi ya wanachama wa CUF walifanikiwa kufika katika mkutano huo baada ya kukodisha magari yaliyokuwa na kibali cha kwenda Chalinze. 

Pamoja na hali hiyo, Polisi wengi walipelekwa katika mkutano huo na imedaiwa kuwa wananchi walitishwa ili wasihudhurie mkutano huo wa chama cha upinzani. 

Mwenyekiti wa CUF, Profesa Lipumba aliwataka polisi wakatae kutumiwa na CCM kuvuruga demokrasia nchini bali wafanye kazi kwa kuzingatia sheria. 

Aliwafahamisha polisi kuwa katika mfumo wa kidemokrasia wenye kuthamini haki za binadamu polisi hawana haki ya kumzuia raia kutembea au kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Hivyo kitendo cha kuwazuia wananchi na wanachama wa CUF kuhudhuria mikutano ya Mlandizi na Chalinze ni kwenda kinyume haki hiyo. 

Aliwakumbusha polisi hao juu ya kisa cha aliyekuwa Rais wa Chile, Generali Agusto Pinochet ambaye alijitengenezea na kuweka mazingira ya utawala, ambao haukujali demokrasia, leo anatapatapa kwa ubaya alioufanya. 

Aidha Mwenyekiti huyo wa CUF alieleza katika mkutano huo kuwa mikutano yao mara kwa mara inavurugwa na vyombo vya dola, na kila walipolalamika baadhi ya watu wakiwemo mabalozi wa nchi za nje, walikuwa wakidai vielelezo vya ushahidi. 

Hivyo aksema kuwa matukio hayo ni ushahidi wa kutosha. 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Mazingira ya uchaguzi huru na haki yasivurugwe

Wananchi washutumu vyombo vya habari

Lipumba awaambia wananchi wasibabaishwe na walioko madarakani

Wasomi SUA walaani ‘rushwa’ ya kisiasa

Polisi kataeni kutumiwa - Lipumba 

Maelfu ya tani za matunda yanaoza Tanga

Habari za ndani
Uondoeni ‘ukoloni’ wa CCM- Mbukuzi

MPASHO NASAHA
WABONGO HAWANA NYONGO !

HABARI
Nchi wafadhili wataka upinzani,  CCM yalalama

Waislamu Musoma walalamika

Habari za Kimataifa

Ushauri Nasaha
Jukumu la wazazi, walimu kwa wanafunzi wanaomaliza masomo

Makala
Madhara ya ulevi kwa binadamu

MAKALA
Sababu ‘1000’ kwanini tunataka CCM ing’oke madarakani - 6

MAKALA
Kiini macho cha msamaha wa deni

Kalamu ya Mwandish
Kama CUF ni chama cha Waislamu 
Jee, CCM ni chama cha Wakristo?

MAKALA
Chama cha Mapinduzi na sera za maendeleo (2)

RIWAYA
Mapinduzi ya fikra

Lishe
Jinsi ya kuzuia utapiamlo kwa wanawake

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Real Madrid yaingia fainali
  • Mapunda, Makoye hawafai timu ya Taifa - Kipingu
  • Tarimba ashinikizwa kujiuzulu Yanga

  •  

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita