|
Na. 047 Jumatano Mei 10 - 16, 2000 |
|
|
|
|
|
Maelfu ya tani za matunda yanaoza Tanga Na Ali Shechonge ZAIDI ya tani 32,000 za matunda na mboga mboga zinazolimwa mkoani Tanga, zinaoza kila mwaka kwa kukosa soko na kiwanda cha kusindika mazao hayo ya kilimo. Akinukuliwa na vyombo mbali mbali vya habari mwanzoni mwa wiki hii, Afisa wa Kilimo na Mifugo wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Twaha Kizunguto, alisema hali ya soko la mazao ya matunda na mboga mboga katika wilaya hiyo inasikitisha sana. Mtaalam huyo wa wilaya aliongeza kwa kusema ubovu wa bara bara ni kikwazo kingine kinachowafanya wakulima kushindwa kupeleka mazao yao katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Kilimanjaro, ambako angalau kuna soka la matunda na mboga mboga. Mkoa wa Tanga na hasa wilaya yake ya Lushoto inaongoza kwa uzalishaji wa matunda. Bw.Twaha Kizunguto ametoa wito kwa serikali kutafuta wawekezaji ili wajenge viwanda vya kusindika matunda na mboga mboga, hatua ambayo itawasaidia wakulima kuepukana na hasara wanayoipata kila mwaka.
UMETOLEWA wito wa kuwataka wananchi wakiondoe Chama Cha Mapinduzi (C.C.M) madarakani.katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Wito huo umetolewa hivi karibuni na Amir wa Shura ya Maimamu Sheikh Juma Mbukuzi, wakati akihutubia katika maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislam wa 1421 A.H. yaliyofanyika katika msikiti wa Ijumaa wa Gongo la Mboto mwisho. Amir Mbukuzi aliuambia umati wa waumini waliohudhuria maadhimisho hayo kuwa wakati wa kuhakikisha jamii inakombolewa kutoka katika ukoloni wa CCM hivi sasa umekwishawadia. Sheikh Mbukuzi aliufananisha utawala wa C.C.M na wakoloni kwa kuwabagua wananchi na kutojali maslahi yao.Akitoa mfano,Sheikh huyo alisema. "Wakoloni (Wazungu) waliichukia sana TANU, hadi Baba yangu Mzee Mbukuzi kwa hofu akawa anaificha kadi yake ya TANU ndani ya shimo la choo kwa kuining'iniza na uzi ili asijulikane kuwa yeye ni mwana-TANU. Hii ni sawa na leo wapinzani wanavyochukiwa. Imefikia akikamatwa Sheikh au kiongozi yeyote wa Kiislam basi huusishwa na CUF. "Sasa kwani kuwa CUF ni dhambi?", alihoji Sheikh Mbukuzi. Aliwataka waumini wazipuuze propaganda za kutochanganya dini na siasa, na badala yake waendelee kuelimishana popote pale walipo jinsi gani wataikomboa jamii. Alisema msamiati wa kutochanganya dini na siasa umetungwa maalum muda mrefu ili kuwaziba mdomo Waislamu wasipate kuyabainisha maovu yanayofanywa na CCM na serikali yake dhidi ya raia. Alisema inashangaza sana kuwaona watu hawa leo wanajitia kusahau kwamba jambo la kuchanganya dini na siasa ndio lililoleta uhuru wa nchi ya Tanganyika, ambapo Waislamu ndio waliokuwa mstari wa mbele na kusimama kidete katika kumwondoa mkoloni. "Wanajifanya hawajui kuwa Mufti wa Waislamu, Almarhuum Sheikh Hassani bin Amir, pamoja na kufundisha dini katika msikiti wa Ngazija, alikuwa pia akigawa wazi kadi za TANU msikitini hapo", alisema Amir Mbukuzi. Aidha, Sheikh Mbukuzi alionesha kushangazwa na ukimya wa viongozi wa serikali pale ambapo wakristo hasa kanisa katoliki linapozungumzia siasa. "Lakini wao hawasemwi kuwa wanachanganya dini
na siasa, ila Waislamu tu. Tutambue kuwa propaganda hiyo dhidi yetu ni
kuogopa tusiwaseme kwani ni sisi ndio waliotuathiri sana. Hivyo, wanachokihami
hapo ni ukweli wa mambo unaowauma tunaowasema. Sasa tunasema hivi, hatutoishia
tu katika kuchanganya dini na siasa bali ni kukorogwa hadi dhulma iondoke".
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Wananchi washutumu vyombo vya habari Lipumba awaambia wananchi wasibabaishwe na walioko madarakani Wasomi SUA walaani ‘rushwa’ ya kisiasa Polisi kataeni kutumiwa - Lipumba Maelfu ya tani za matunda yanaoza Tanga Habari za ndani
MPASHO NASAHA
HABARI
Ushauri Nasaha
Makala
MAKALA
MAKALA
Kalamu ya Mwandish
MAKALA
RIWAYA
Lishe
|
|
|
|
|