NASAHA
Na. 043 Jumatano Aprili 12- 18, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Habari za Kimataifa
 
 

Museveni awasaka Wakristo wauaji

KAMPALA, Uganda,

SERIKALI ya Rais Museven wa Uganda imetangaza kutoa donge nono la dola 1300 za Kimarekani kwa yeyote atakayesaidia kupatikana kwa viongozi wa Kikristo waliosababisha vifo kwa kuungua moto mamia ya waumini.

Wiki iliyopita serikali hiyo ilitamka rasmi kuwakamata mara wakionekana wadhamini sita wa dhehebu hilo linalojiita Kuhuisha amri kumi za Mungu. 

Mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu, huko Kanungu nchini Uganda Kanisa moja liliwaka moto na wahanga mamia walipoteza maisha. 

Kufuatia tukio hilo, serikali ya Uganda imechukua hadhari ikiwemo kuzifanyia utafiti dini na madhehebu mbalimbali zinazosadikiwa kuwafundisha waumini wake kibubusa. 

Inasemekana viongozi hao wamekimbilia baadhi ya nchi jirani ikiwemo Congo Kinshansa. 

Uganda nchi iliyopo Afrika ya Mashariki ina idadi kubwa ya waumini wa dini ya Kikristo na Waislamu ni asilimia 30. 



Wairaq milioni moja wafa kwa vikwazo 

AMMAN, 

Waziri wa Afya wa Iraq, Umid Medhat Mubarak Jumatatu alisema kwamba zaidi ya Wairaq milioni moja, wengi wao wakiwa watoto, walikufa kutokana na vikwazo vya Umoja wa Mataifa ambavyo vimechukua miaka kumi sasa.

"Kiwango cha vifo vya watoto wachanga kimepanda nchini Iraq kufuatia vikwazo hadi kufikia vifo 108 kwa kila watoto 1000 wanaozaliwa wakati ambapo kabla ya vikwazo kulikuwepo vifo 42 kati ya 1000 wanaozaliwa", Mubarak aliwaambia waandishi. 

Alihitaja kwamba idadi ya vifo vilivyosababishwa na vikwazo ni 1,294,882, kati yao 523,204 walikuwa watoto wa chini ya umri wa miaka mitano. Umoja wa Mataifa uliiwekea vikwazo Iraq mwaka 1990 baada ya kuivamia Kuwait mwaka 1989, mwaka mmoja kabla Umoja wa Mataifa haujaweka vikwazo, madaktari walifanya operesheni 151,525 kwa kila mwezi kulinganisha na sasa ambapo operesheni kama hizo ni 4442 tu kwa mwezi. 

Pia Waziri huyo alilaumu vikwazo kwamba ndiyo chanzo cha utapiamlo ambao unasababishwa na uzazi kabla ya muda wake na kuenea kwa magonjwa ya kuambukiza kama kipindupindu, magonjwa ambayo yalishakoma katika Iraq kabla ya 1990. 

Waziri wa Afya wa Iraq alianzisha kampeni ya kitaifa mnamo Machi 28 ya chanjo kwa watoto milioni 3.5 walio chini ya umri wa miaka mitano dhidi ya maradhi ya polio. Hatua ya pili ya kampeni hii itaanza Aprili 25. 

Shirika la Afya Ulimwenguni liligundua ongezeko kubwa la idadi ya watoto wa Iraq wanaougua pepopunda (polio) na lilitoa kauli ya hofu kwamba ugonjwa huo ungeenea. 



G77 kukuza ushirikiano

HAVANA, Cuba

MATAIFA yanayoinukia kimaendeleo hii leo katika mkutano wa kilele yanatarajiwa kupitisha azimio la ushirikiano wa nguvu kati yake na nchi changa.

Naibu Waziri Mkuu wa Cuba akizungumza hapo jana katika matayarisho ya mkutano huo amesema kuwa nchi yake inatoa mwito wa kuunda mfumo moya wa kutukuza utu. 

Mfumo ambao amesema utaondoa au kupunguza pengo kubwa lililopo kati ya maskini na matajiri. 

Ushirikiano wa mataifa hayo utatilia mkazo kuwekeza biashara na rasilimali, kukuza uchumi, ubadilishanaji wa fedha pamoja na ujuzi, ufundi wa teknolojia mpya. 

Mataifa yanayoendelea yajulikanayo kama G77 yaliunda umoja huo mnamo mwaka 1967 azimio la biashara la UNCTAD mnamo 1964. 

Zaidi ya nchi 160 zinatarajiwa kuwakilishwa na wakuu wa nchi zao, wajumbe 122 kutoka sehemu mbalimbali na wasio wanachama wapatao 34 watashiriki. 



Hizbullah wanusurika

MSEMAJI wa kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu ­ Hizbullah amesema jana kuwa mabomu yaliyorushwa na ndege za Israel hayakuua wala kujeruhi.

Ndege za kivita za Israel jana zilidondosha mabomu katika eneo walipo Hizbullah kusini mwa Levnan. 

Wapiganaji hao wanapambana na Israel kusini ili kurudisha ardhi yao ambayo ilitekwa na Israel. 

Israel inakalia milima ya Golan kwa mabavu, iliteka milima hiyo katika vita yake na Syria mnamo miaka ya sitini. 

Juu
 

YALIYOMO
 

Tahariri
Wanaokemea dhuluma wasinyanyaswe

Waislamu waapa kuinyima kura CCM

Mkapa ahutubia Taifa: 
Ugumu wa maisha kuendelea

Wananchi wamuunga mkono Askofu Kakobe

MPASHO NASAHA
WAKIAMUA, HATA WAKICHAFUKA WATANAWA!!!

SHERIA
Faida ya kuwepo kwa sheria za haki kunategemea na wanaozisimamia

Ushauri Nasaha
Namna ya kumfanya mtoto wako aweze kuzungumza

MAKALA
Sababu ‘1000’ kwanini tunataka CCM ing’oke madarakani - 2

WAZO  LA  WIKI
Polisi acheni ubalakala

MAKALA
Kuporomoka kwa maadili  katika jamii yetu; Sababu na utatuzi wake - 2

Kalamu ya Mwandishi
Tatizo si jino kwa jino, bali utekelezaji muafaka!

MAKALA
Uchaguzi Mkuu Mwaka 2000 (6)
Vijana mjiandikishe kwa wingi na siku ya uchaguzi mjitokeze

Makala ya Mtangazaji
LEO NI SIKU YA ASHURA

Habari za Kimataifa

Riwaya
Kisasi cha mauti -3

Lishe
Ni kwa jinsi gani wanawake wanapata utapiamlo

MASHAIRI

MICHEZO

  • Madadi, Jamhuri acheni ‘rusha roho’ katika soka – Wapenzi
  • Yanga wakumbwa na kiwewe
  • Mapunda asema hana bahati ya kutia mabao

  • •••Golikipa Majimaji alia na mabeki
     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita