NASAHA
Na. 043 Jumatano Aprili 12- 18, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Mkapa ahutubia Taifa: 
Ugumu wa maisha kuendelea 
  • Maghimbi amshangaa kuacha kukemea polisi kupiga raia Z'bar 
Na Mwandishi Wetu 

RAIS Benjamin Mkapa juzi Aprili 10, alilihutubia taifa ambapo alitangaza kuwa Tanzania itaanza kunufaika na mpango wa kusamehewa madeni, mpango ambao matunda yake yataanza kuonekana miezi 18 baada ya kuanza kutekelezwa msamaha huo.

Rais Mkapa aliyasema hayo wakati akitangaza hatua ya Tanzania kusamehewa madeni ya thamani ya dola za Marekani bilioni 2 mashirika ya fedha ya kimataifa na baadhi ya nchi za nje. 

Hata hivyo Mhe. Rais hakutaja ni lini mpango huo wa msamaha wa madeni utaanza kutekelezwa jambo ambalo linaashiria kuendelea kwa hali ngumu ya maisha inayowakabili wananchi. 

Mhe. Rais aliendelea kueleza kuwa kiasi hicho cha msamaha ni sawa na nusu ya madeni ambayo nchi hii imekuwa ikidaiwa. 

Alifafanua kuwa msamaha huo umetolewa kufuatia Tanzania kutekeleza kikamilifu masharti ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Dunia(IMF), ikiwemo kukusanya kodi kwa wingi. 

Mhe. Rais alisema kuwa kwa msamaha huu nchi itafaidika kutumia kiasi cha shilingi bilioni 80 (dola za Marekani milioni 100)kila mwaka katika kuboreshwa huduma za jamii, pesa ambazo zingetumika kulipa madeni. 

Hata hivyo alieleza kwamba manufaa hayo ya msamaha wa madeni yatategemea kutekelezwa kwa masharti kadhaa, yakiwemo kukuza demokrasia na kuendelea kusanya kodi kwa wingi. 

Katika hotuba hiyo Rais Mkapa pia alieleza kuwa serikali itafanya kila lililo ndani ya uwezo wake ili kuwe na uchaguzi huru na wa haki na akawaonya wale ambao wameanza kudai damu itamwagika na waliotangaza sera za jino kwa jino. 

Vyombo vingi vya habari vimeonyesha tafsiri ya kuwa onyo hilo la Rais limeelekezwa kwa Chama cha Wananchi (CUF). 

Wakati huo huo, Kiongozi wa upinzani Bungeni ambaye pia ni Waziri Mkuu kivuli Bi. Fatma Maghimbi amesema kwamba ameshangazwa na kauli hiyo ya Rais ya kuelekeza onyo kwenye chama chake (CUF). 

Akizungumza na Shirika la Habari la Utangazaji la BBC jana jioni alisema kuwa awali aliposikia kuwa Rais angehutubia Taifa alitegemea kuwa Rais angezungumzia na kuonesha kuguswa na kitendo cha Polisi kuwapiga raia hovyo huko Zanzibar hivi sasa. Alisema kwamba amesikitishwa kuona Mhe. Rais akielekeza lawama kwenye chama chake cha CUF. 

Alieleza kuwa katika vurugu hizi za polisi wamewashauri wanachama wa CUF kutonyanyua mkono kujibu mashambulizi hayo ya polisi,na kwamba ikiwezekana wakimbie tu. 

Akizungumzia shutuma za "jino kwa jino" Bi. Fatma Maghimbi alieleza kwamba wao walitangaza kuwa mwaka 1995 Chama cha CUF kilidhulumiwa. Hivyo waliazimia kwamba mwaka huu hawatakubali kudhulumiwa tena na kwamba endapo wataonewa itakuwa "jino kwa jino". Akifafanua usemi huo Mhe. Maghimbi alisema, "...ukianza kuning'oa jino langu nami nitakung'oa lako... na hiyo ni wakati wa uchaguzi mkuu." 

Alishangaa kuwa kauli hiyo inapewa tafsiri potofu wakati iko wazi katika Kiswahili kilicho fasaha. 

Juu
 

YALIYOMO
 

Tahariri
Wanaokemea dhuluma wasinyanyaswe

Waislamu waapa kuinyima kura CCM

Mkapa ahutubia Taifa: 
Ugumu wa maisha kuendelea

Wananchi wamuunga mkono Askofu Kakobe

MPASHO NASAHA
WAKIAMUA, HATA WAKICHAFUKA WATANAWA!!!

SHERIA
Faida ya kuwepo kwa sheria za haki kunategemea na wanaozisimamia

Ushauri Nasaha
Namna ya kumfanya mtoto wako aweze kuzungumza

MAKALA
Sababu ‘1000’ kwanini tunataka CCM ing’oke madarakani - 2

WAZO  LA  WIKI
Polisi acheni ubalakala

MAKALA
Kuporomoka kwa maadili  katika jamii yetu; Sababu na utatuzi wake - 2

Kalamu ya Mwandishi
Tatizo si jino kwa jino, bali utekelezaji muafaka!

MAKALA
Uchaguzi Mkuu Mwaka 2000 (6)
Vijana mjiandikishe kwa wingi na siku ya uchaguzi mjitokeze

Makala ya Mtangazaji
LEO NI SIKU YA ASHURA

Habari za Kimataifa

Riwaya
Kisasi cha mauti -3

Lishe
Ni kwa jinsi gani wanawake wanapata utapiamlo

MASHAIRI

MICHEZO

  • Madadi, Jamhuri acheni ‘rusha roho’ katika soka – Wapenzi
  • Yanga wakumbwa na kiwewe
  • Mapunda asema hana bahati ya kutia mabao

  • •••Golikipa Majimaji alia na mabeki
     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita