AN-NUUR
Na.163 Rabiul Thani 1419, Agosti 21 - 27, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
Marekani yashambulia Sudan, Afghanistan

Watu wengi wahofiwa kujeruhiwa, kufa
 

Ndege za kijeshi za Marekani zimeshambulia Sudani na Afghanistan jana (Alhamisi) saa tatu usiku wa kwa majira ya Afrika mashariki.

Kwa mujibu wa matangazo ya CNN, mashambulizi hayo ya yamefanywa kufuatia tuhuma kwamba nchi hizo zinahusika na milipuko ya mabomu kwenye balozi za Marekani katika miji ya Nairobi na Dar es salaam.

Ikulu ya Marekani imesema kuwa mashambulizi hayo yamefanywa ili kutoa kile ilichodai kuwa ni onyo kwa mataifa yanayojihusisha na Ugaidi.

Msemaji wa Ikulu hiyo ameeleza kwamba mashambulizi hayo yaliidhinishwa na Rais Bill Clinton saa chache kabla ya kufanyika na kwamba yalielekezwa katika maeneo yaliyolengwa.

Akitoa sababu za kushambulia Sudan na Afghanistan, Rais Bill Clinton amedai kwamba ana ushahidi wa kutosha kuhusika kwa mataifa hayo na mipango ya kigaidi, kwamba yalishawahi kufanya ugaidi, kwamba yanajiandaa kufanya mashambulizi mengine ya kigaidi katika balozi za Marekani na kwamba yanamiliki silaha za Sumu.

Nchini Sudani ndege hizo za mashambulizi zilikiangushia mabomu kiwanda cha madawa kusini mwa jiji la Khartoum.

Aidha nchini Afghanistan mabomu yaliangushwa katika vituo sita vinavyodaiwa kuwa kambi za "magaidi" hao.

Alipohojiwa mashambulizi hayo yamefanyika kutokea wapi, msemaji wa Ikulu ya Mareakni alijibu kwa mkato kwamba yamefanywa na majeshi ya Marekani.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya ndani wa Sudan, ameyaeleza mashambulizi hayo kuwa ni maendelezo ya hujuma zinazofanywa na Marekani dhidi ya nchi yake na kuwa yamefanywa katika kiwanda cha madawa ya binadamu ( Shifer Parmaceutical plant) kinachomilikiwa na watu binafsi kilichopo Kartoum.

Msemaji mmoja wa Afghanistan Bw. Noordullah Zadran alipohojiwa jana usiku na vyombo vya habari alisema kwamba, kwanza hakuna ushahidi wa kumhusisha Bwana Usama bin Laden na milipuko ya hivi karibuni na pili hawatosalimu amri kwa yoyote.

Wakati huo huo, Seneta wa Jimbo la Indiana nchini Marekani bwana Dancoats, ameshutumu mashambulizi yaliyofanywa na nchi yake katika nchi za Sudan na Afghanistan.

Kwa mujibu wa taarifa za CNN, Seneta huyo amesema kwamba licha ya shambulio hilo kutokidhi haja inayokusudiwa, Rais Bill Clinton hana mamlaka ya kuidhinisha jambo zito kama hilo kutokana na kashfa inayomkabili hivi sasa.

Aidha ameshangazwa na uamuzi wa nchi yake wakati uchunguzi wa kuwasaka watuhumiwa bado haujakamilika.

Aidha Seneta huyo ameongeza kusema kwamba mashambulizi hayo huenda yakawaweka Wamarekani katika wakati mgumu wa kuchukiwa na dunia nzima.

Seneta huyo amemtaka Rais Bill Clinton ajiuzulu mara moja kwa hatua yake hiyo ambayo ameieleza kuwa haikuwa na ridhaa ya Wananchi wa nchi hiyo. 

mashambulizi mengine ya kigaidi katika balozi za Marekani na kwamba yanamiliki silaha za sumu.

Nchini Sudani ndege hizo za mashambulizi zilikiangushia mabomu kiwanda cha madawa kusini mwa jiji la Khartoum.

Aidha nchini Afghanistan mabomu yaliangushwa katika vituo sita vinavyodaiwa kuwa kambi za "magaidi" hao.

Alipohojiwa mashambulizi hayo yamefanyika kutokea wapi, msemaji wa Ikulu ya Mareakni alijibu kwa mkato kwamba yamefanywa na majeshi ya Marekani.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya ndani wa Sudan, ameyaeleza mashambulizi hayo kuwa ni maendelezo ya hujuma zinazofanywa na Marekani dhidi ya nchi yake na kuwa yamefanywa katika kiwanda cha madawa ya binadamu ( Shifer Parmaceutical plant) kinachomilikiwa na watu binafsi kilichopo Kartoum.

Msemaji mmoja wa Afghanistan Bw. Noordullah Zadran alipohojiwa jana usiku na vyombo vya habari alisema kwamba, kwanza hakuna ushahidi wa kumhusisha Bwana Usama bin Laden na milipuko ya hivi karibuni na pili hawatosalimu amri kwa yoyote.

Wakati huo huo, Seneta wa Jimbo la Indiana nchini Marekani bwana Dancoats, ameshutumu mashambulizi yaliyofanywa na nchi yake katika nchi za Sudan na Afghanistan.

Kwa mujibu wa taarifa za CNN, Seneta huyo amesema kwamba licha ya shambulio hilo kutokidhi haja inayokusudiwa, Rais Bill Clinton hana mamlaka ya kuidhinisha jambo zito kama hilo kutokana na kashfa inayomkabili hivi sasa.

Aidha ameshangazwa na uamuzi wa nchi yake wakati uchunguzi wa kuwasaka watuhumiwa bado haujakamilika.

Aidha Seneta huyo ameongeza kusema kwamba mashambulizi hayo huenda yakawaweka Wamarekani katika wakati mgumu wa kuchukiwa na dunia nzima.

Seneta huyo amemtaka Rais Bill Clinton ajiuzulu mara moja kwa hatua yake hiyo ambayo ameieleza kuwa haikuwa na ridhaa ya Wananchi wa nchi hiyo. 
 
 

Juu

YALIYOMO



TAHARIRI

Milipuko ya mabomu Dar, Nairobi: Waislamu walaani vyombo vya habari
Na Mwandishi wetu

Wanawake Waislamu Tanga waazimia kupigania haki
Na Ibn Masoud, Tanga

Marekani yashambulia Sudan, Afghanistan

Maoni: Kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani:
Huu ni unazi au sehemu ya mtandao?

Nguruwe kuzua tafrani Kibamba
Na Mwandishi Wetu

Sheikh Mbukuzi ataka vijana wajihadhari  na utamaduni wa Magharibi
Na Said Shariff

TAMPRO kuzindua Tawi Iringa
Na Mwandishi Wetu

Tamasha la kusaidia wagonjwa laanza Moro
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro

Kambi ya matibabu ya Macho Tanga yaanza
Na Mwandishi Wetu

MAONI: Kanisa mshiriki wa ukandamizaji

Porojo za Ngatara
Na J. Hussein

Ubatizo kupitia TVZ?
Na Salahuddin Ahmad

Waislamu Kosovo waangamizwa

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA 
SHIRIKISHO LA TANZANIA -2

Hoja binafsi: Uhusiano na Marekani usituletee maafa
Na Said Rajab

Darasa la Muhammad (s.a.w)

Wanamume toeni haki  za wanawake kuepusha ufisadi
Na Halima Issa Ndabi,  Mwanza

MAKALA: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 2
Na Muhibu Said

Mwanaadamu alipofikia
Na Nineka B.N., Geita

Mafunzo ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe

Matangazo
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita