|
Na.163 Rabiul Thani 1419, Agosti 21 - 27, 1998 |
WAISLAMU wamevilaumu vyombo vya habari kwa kuihusisha dini yao na ulipuaji wa mabomu ya kigaidi mjini Nairobi. Baraza Kuu la Waislamu Kenya (SUPKEM) limesema kwamba Waislamu hawakubaliani na vitendo vyovyote vya kinyama na hivyo hawawezi kuhusika kwa namna yoyote na ulipuaji wa mabomu. Katika taarifa yake iliyosainiwa na Katibu Mkuu wake, Sheikh Ahmad Khalifa, SUPKEM limesema kwamba Uislamu kama dini nyingine yoyote haiwezi kuunga mkono mauaji ya watu wasio na hatia. Na hivyo, akasema kwamba kuhusisha Uislamu na tukio hilo kulikofanywa na vyombo vya habari ni kuupaka Uislamu matope. SUPKEM imeongeza kusema kwamba ugaidi ni sumu hatari na uovu kwa dunia nzima ambao hauwezi kuhusishwa na dini yoyote. Taarifa ya SUPKEM imesisitiza kwamba ni jambo la kusikitisha kwamba hata kabla ya uchunguzi kukamilika zimekuwepo juhudi za baadhi ya vyombo vya habari kuonyesha kwamba wa kulaumiwa katika vitendo hivi vya ugaidi ni Waislamu. Imevitaka vyombo vya habari viwaache wachunguzi wafanye kazi yao kwa sheria, kanuni na taratibu zao. Wakati huo huo, Waislamu sehemu mbali mbali duniani, wamekuwa wakielezea wasi wasi wao kufuatia shutuma zinazotolewa kupitia vyombo vya habari kwamba waliohusika na milipuko ya Dar na Nairobi ni Waislamu au makundi ya kiislamu yanayodaiwa kuwa na msimamo mkali. Akionyesha kushangazwa na shutuma hizo, Msomi maarufu duniani Dk. Jamal Badawi, amehoji ni kwa vipi Waislamu watajwe kuhusika na milipuko hiyo wakati uchunguzi bado haujakamilika. Dk. Badawi amesema kwamba kuwahusisha Waislamu na matukio hayo kwa haraka kiasi hicho kunaweza kudhaniwa kwamba huo ulikuwa ni mpango uliopangwa muda mrefu wa kutafuta visingizio ili kuwadhuru. Dk. Badawi aliyasema hayo wakati akihojiwa na shirika la utangazaji la Uingereza BBC, havi karibuni. Mwanachuoni huyo wa kiislamu wa masuala ya Utawala, amesema kwamba inawezekana kuhusishwa huko kwa Waislamu kunatokana na uadui mkubwa uliopo kati ya Marekani na baadhi ya nchi na makundi ya Waislamu. Hata hivyo Dk. Badawi amesema kuwa kuwatuhumu na kuwaandama Waislamu kiasi hicho huenda kukawa na ajenda ya hatari. Dk. Badawi amefafanua kwamba kama itakuwa ni uadui, Marekani ina maadui sehemu mbali mbali duniani ikiwa ni pamoja na Ukanda Mzima wa Maziwa Makuu barani Afrika. Aidha, Dk. Badawi ameelezea kuchukizwa kwake na jinsi vyombo vya habari vinavyowaripoti Waislamu kwa kuwahusisha na mambo mabaya ulimwengu mzima. Naye Sheikh Abubakar Mwilima akihojiwa na Michael Sikawa wa BBC juu ya tuhuma za kuhusika kwa Waislamu, alisema kwamba mabomu ya Waislamu ni Qur’an na kwamba Uislamu ni dini ya amani na salama. Nchini Afghanistan ambako inadaiwa kuwa ndiko alikojificha "mfadhili" wa makundi ya kiislamu yenye msimamo mkali, Wanaharakati wa nchi hiyo wameripotiwa kutoa tamko la kukanusha uzushi unaoenezwa dhidi yao. Wanaharakati hao wametoa onyo la kuwa tayari kupambana na yeyote yule atakayejaribu kuvamia nchi hiyo kijeshi. Wamemtaja Usama bin Laden kwamba hahusiki na milipuko iliyotokea Dar na Nairobi na kwamba hawako tayari kumkabidhi kwa Marekani na wameahidi kumlinda hata kwa kumwaga damu yao. |
Milipuko ya mabomu Dar, Nairobi: Waislamu
walaani vyombo vya habari
Wanawake Waislamu Tanga waazimia kupigania
haki
Marekani yashambulia Sudan, Afghanistan Maoni: Kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani:
Nguruwe kuzua tafrani Kibamba
Sheikh Mbukuzi ataka vijana
wajihadhari na utamaduni wa Magharibi
TAMPRO kuzindua Tawi Iringa
Tamasha la kusaidia wagonjwa
laanza Moro
Kambi ya matibabu ya Macho Tanga
yaanza
MAONI: Kanisa mshiriki wa ukandamizaji Porojo za Ngatara
Ubatizo kupitia TVZ?
MAPENDEKEZO YA KATIBA YA
Hoja binafsi: Uhusiano na Marekani
usituletee maafa
Wanamume toeni haki za
wanawake kuepusha ufisadi
MAKALA: Hoja za kutofautisha Yesu
na Issa ni udhaifu, ni uzushi mtupu! - 2
Mwanaadamu alipofikia
|
Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua kwa: webmaster@islamtanzania.org