NASAHA
Na. 067 Jumatano Septemba 27 - Oktoba 2, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
LISHE

Kimfaacho mtoto

Mariam Mbwambo

Kwa mara nyingine tena, wapendwa wasomaji tunawaletea mfululizo wa makala za lishe. Leo tutaangalia uboreshaji wa afya ya mtoto.

Mtoto anahitaji uangalifu wa hali ya juu ili kumwezesha kukua vizuri. Mtoto huyu atahitaji virutubisho muhimu kama proteni, wanga (starch),vitamin, maji yaliyo safi na salama, madini mbalimbali, kwa ajili ya kuimarisha mifupa yake na meno. Pia kumwepusha na magonjwa yasababishwayo na ukosefu wa madini hayo kama goita (tezi la shingo) n.k.

Hivyo, mtoto kama kiumbe mwingine ana vipimo maalum. Katika kukamilisha mahitaji hayo, maziwa ya mama ni muhimu sana tangu mtoto anapozaliwa hadi anapofikia umri wa miezi minne hadi atakapohitajia vyakula vya ziada ambavyo vitatayarishwa katika hali ya usafi na utaalam wa hali ya juu.

Maziwa ya mama ni chakula tosha cha mtoto awapo mdogo kwa sababu yamekamilika katika virutubisho vyote muhimu vihitajikavyo mwilini. Kutoka umri wa miezi 4-6 maziwa peke yake humtosheleza mtoto. Maziwa ni muhimu kwa mtoto kwani huzidisha upendo kati ya mama na mtoto. Hayana vimelea vya magonjwa, humuepusha mtoto na magonjwa kama kuhara, na mengine mengi, humuongezea uzito na afya nzuri.

Iwapo akaanza kupatiwa maziwa ya chupa kutokana na kufa kwa mama yake, chupa hizo lazima visafishwe vizuri kwa maji ya mtoto na vikaushwe vizuri. Vyombo vya mtoto visichanganywe na vya watu wazima. Ili visipate shombo, ikasababisha maziwa kuchacha au harufu mbaya katika chakula cha mtoto.

Unashauriwa kuzingatia muda wa kulisha mtoto wako kila baada ya masaa 3 au 4. Ama kwa masaa 3, saa 12 asubuhi, saa 3 asubuhi, saa sita mchana, saa tisa na saaa 12 jioni. Mlo wake kwa ujumla waweza kuwa uji, wali bokoboko (ubwabwa) na mchuzi usio na chumvi wala ndimu nyingi, supu ya nyanya. Juisi ya matunda na maziwa, bila kusahau maji.

Baada ya kuacha maziwa ya mama lazima apewe vyakula vya kujenga na kulinda mwili zaidi ili kujenga mwili wake na kumwepusha na utapiamlo au P.E.M. (protein energy malnutrition).

Vyakula hivyo vyaweza kuwa juisi ya machungwa, papai, mboga mboga kama nyanya za kusaga, karoti, juisi, mchicha n.k.

Mayai, hasa kiini cha yai kilichopikwa na maziwa.

Kwa watoto wanaoanza kutembea, wapewe vyakula vya kuvutia kwani huwa wabishi kula. Hivyo lazima wabadilishiwe vyakula ili kuwapa hamu ya kula vyakula hivyo. Wakati huu maziwa yanahitajika kwa wingi, mayai, samaki wa kuchemsha, nyama ya kusaga,viazi vya kusaga, ndizi, uji. Supu ya mbogamboga na matunda aina mbalimbali.

Vyakula kama dagaa, maharage, supu ya maharage apewe kwa wingi zaidi.

Vyakula vya sukari nyingi, vya kukaanga, samaki ambao itawawia vigumu kutafunwa wasipewe pamoja na pastries wasipewe.

Hivyo basi tunashauriwa kufuata maelekezo na mawaidha mazuri kutoka kwa wataalm wa lishe ili kuweza kuwapatia lishe bora, watoto ambao ni taifa la kesho. 
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Polisi ‘isiibebe’ CCM

Wapinzani kumuimarisha Prof. Lipumba

Ngangari kung’olewa Sokoni, Ilala

Polisi nchini hawajui mipaka ya kazi yao -OAU

MAKALA
BBC, CCM ndugu au tajiri na kibaraka?

HABARI
‘Walioshindwa kutawala wasikimbilie matusi’

ATV yatakiwa kuzingatia maadili

Wakazi wa Tabata walalamikia athari ya maji machafu

Maalim Seif akanusha madai ya kumwaga damu

USHAURI NASAHA
‘Mama, hela hii inanunua nini?'

MAKALA
Demokrasia ni kukubaliana kutokukubaliana

MIPASHO NASAHA
HEBU VUENI MIWANI ZENU!

KALAMU YA MWANDISHI
Juha haliambiliki!Juha haliambiliki!

MAKALA
Amani ya Tanzania itadumishwa na haki

MWENYE MACHO…
Hoja za uongo katika kampeni

MAKALA
Chonde Dk. Omari na Karume wahurumieni Wazanibari wenzenu

Habari za Kimataifa

LISHE
Kimfaacho  mtoto

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Yanga kuwakosa Mahadhi, Mbuna
  • Idd Azzan lawamani
  • Kibadeni, Kayuni wanafaa Stars - Machuppa
  • Said Maulidi: Sihami Simba

  •  

       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita