NASAHA
Na. 067 Jumatano Septemba 27 - Oktoba 2, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
HABARI
 
 

Maalim Seif akanusha madai ya kumwaga damu

  • Aitaka CCM itoe ushahidi
  • CUF ikishindwa kihalali hawatapinga
  • Lakini hawatakubali kudhulumiwa ushindi wao


Na Hassan Simba -Zanzibar

Chama cha Wananchi (CUF) kimekanusha habari zinazoenezwa na CCM, kuwa CUF endapo itashindwa katika uchaguzi wa mwaka huu kitamwaga damu.

Katibu Mkuu wa chama hicho Bwana Seif Sharif Hamadi, amesema chama chake hakijawahi kutoa kauli kama hiyo na kwamba maneno hayo ni uzushi mtupu unaoenezwa na CCM.

Katibu Mkuu huyo ambaye pia ndiye mgombea Urais wa Zanzibar ameyasema hayo alipokuwa akihutubia wananchi wa Jimbo la Mlandege katika viwanja vya Lumumba.

Bwana Hamadi amesema kila mara chama chake kimekuwa kikisisitiza kuwa endapo kitashindwa katika uchaguzi ulio halali basi kitaridhia matokeo kwa lengo la kuheshimu maamuzi ya wananchi walio wengi.

Amesema anashangazwa na viongozi wa CCM ambao wamekuwa hawatamki hadharani kama watayakubali matokeo pindi chama chao kitashindwa.

Amedai kukaa kimya kwa CCM bila kueleza msimamo wake ni dalili kuwa chama hicho hakina nia nzuri na ndio maana wamekuwa wakifanya hila ili kuvuruga uchaguzi kwa vile tayari CCM imeshapoteza matumaini ya kushinda.

"Nawataka viongozi wa CCM , Mkapa, Dr. Omar na mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Bwana Amani waseme ni wapi na lini chama chetu kimetamka kuwa endapo tutasindwa tutamwaga damu", amehoji Bw.Hamad

Amesema mbali na kumwaga damu ya mtu hata ya inzi haitomwagika, lakini wakishinda kisha kudhulumiwa ushindi wao hawatakubali, alisisitiza Bw. Hamad.

Aidha Bw. aliwaambia wananchi wa Jimbo la Mlandege kuwa endapo watamchagua kuwa rais wa Zanzibar atahakikisha anatatua kero zote zinazowakabili .

Pia Bw.Hamad amewahidi wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Jula Kali kuwa atawajengea vibanda vya kufanyia biashara zao na kwamba tayari ameshajitokeza mfadhili atakayefanya hivyo na kinachosubiriwa ni serikali ya CUF kuingia madarakani.
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Polisi ‘isiibebe’ CCM

Wapinzani kumuimarisha Prof. Lipumba

Ngangari kung’olewa Sokoni, Ilala

Polisi nchini hawajui mipaka ya kazi yao -OAU

MAKALA
BBC, CCM ndugu au tajiri na kibaraka?

HABARI
‘Walioshindwa kutawala wasikimbilie matusi’

ATV yatakiwa kuzingatia maadili

Wakazi wa Tabata walalamikia athari ya maji machafu

Maalim Seif akanusha madai ya kumwaga damu

USHAURI NASAHA
‘Mama, hela hii inanunua nini?'

MAKALA
Demokrasia ni kukubaliana kutokukubaliana

MIPASHO NASAHA
HEBU VUENI MIWANI ZENU!

KALAMU YA MWANDISHI
Juha haliambiliki!Juha haliambiliki!

MAKALA
Amani ya Tanzania itadumishwa na haki

MWENYE MACHO…
Hoja za uongo katika kampeni

MAKALA
Chonde Dk. Omari na Karume wahurumieni Wazanibari wenzenu

Habari za Kimataifa

LISHE
Kimfaacho  mtoto

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Yanga kuwakosa Mahadhi, Mbuna
  • Idd Azzan lawamani
  • Kibadeni, Kayuni wanafaa Stars - Machuppa
  • Said Maulidi: Sihami Simba

  •  

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita