|
Na. 067 Jumatano Septemba 27 - Oktoba 2, 2000 |
|
|
|
|
|
Hoja za uongo katika kampeni Na Toroka Kanyika LEO katika safu hii tutaona jinsi wananchi wenye usongo na maendeleo ya nchi yao walivyofanikiwa kuwaweka watawala roho juu. Kilipoanza kipindi cha kampeni za uchaguzi Agosti 18, kauli iliyokuwa inasikika kutoka kwa viongozi wa chama tawala ilikuwa ni kusisitiza kwamba wao watanadi sera zao na kuwa wananchi watawachagua kwani vyama vya upinzani havina sera. Kwa majigambo haya ilitegemewa kwamba hotuba zote za viongozi wa CCM zitakuwa zimejaa sera za chama hicho kwa lengo la kuwafanya wananchi kupima sera hizo na kuzilinganisha na zile za wapinzani ambazo tangu hapo CCM ilishadai kuwa wapinzani hawana sera mbadala ya kuwaletea wananchi maendeleo. Tunachokishuhudia sasa ni ama uongo au matusi kwa wapinzani. Uongo na matusi au kejeli zinazotolewa zinakilenga zaidi chama cha wananchi, CUF. Viongozi wake wamekuwa wakiandamwa sana. Tumesikia ikidaiwa kuwa CUF inakusudia kumwaga damu endapo itashindwa katika uchaguzi MKUU UJAO. Lengo la uongo huu ni kuwatisha wananchi ili wasikichague chama hiki. Ama kwa upande mwingine kinachokusudiwa na kwa dhana kuwa upo wizi wa kura. Awali chama cha CUF kilitangaza na kimeendelea kushikilia msimamo wake kuwa endapo kitapokonywa ushindi kwa hila yoyote ile ikiwapo ya wizi wa kura wanachama wake hawatokubali;. Ikaelezwa bayana kuwa wakati itakapobainika kuwa CUF imepokonywa ushindi basi sera ya 'Jino kwa Jino' itatumika. Chama kinachotuhumiwa kuhusika na wizi wa kura hakijajitolea kujibu tuhuma hizi kwa hoja za kueleweka bali zimebuniwa mbinu za kuonesha kuwa lengo la CUF ni kumwaga damu. Jambo la kushukuru ni kuwa kila uchao wananchi kwa mamia wanakuwa ngangari. Wameshapania uchaguzi huu, wamejiandikisha kwa wingi na wanasubiri kupiga kura zao na kisha kuzilinda. Umejengwa pia uongo mwingine kuwa CUF ni chama cha Waarabu chenye nia ya kurudisha usultani na utumwa. Uongo huu nao kwa mwenye macho hausaidii kumwepusha na CUF bali huwa kama barometa ya kujua ni kwa kiasi gani watawala wameingia hofu na woga juu ya kuzipoteza nafasi zao. Pili wengi wa watu waliopo leo masuala ya utumwa na usultani kwao ni mambo ya historia tu. Haingii akilini kuwa Prof. Lipumba anaweza kuacha kazi zake katika anga za kimataifa arudi nyumbani kuikabidhi nchi kwa wakoloni. Kuhusu wagombea imekuwa ilidaiwa kuwa Prof. Lipumba hafai kuongoza nchi kwani hana mke. Japo haijawahi kuelezwa kuwa sifa ya mtu mgombea urais ni kuoa, lakini uzushi huu umekuwa ukienezwa na watu wenye hadhi upande wa chama tawala. Wananchi licha ya kufahamu kuwa mke siyo sifa ya kutawala, wanafahamu pia kuwa Prof. Lipumba anaye mke. Ukweli huu umesaidia wenye macho kuthibitisha kuwa wale waliodai kuwa na sera hawanazo badala yake wana kejeli na uongo. Hatua ya hivi karibuni ni ya chama tawala kuagiza
polisi kuwa macho na CUF. Hatua hii kwa wengine imejenga hisia kuwa yanafanywa
maandalizi ya kuwatisha wananchi. Hata hivyo CUF haikukawia kujibu. Imeripotiwa
kuwa CUF wanadai kuwa sasa wao ni ngangari kinoma.Ifahamike kuwa uogo hautadumisha
amani na utulivu unaodaiwa kuwepo....Tukutane wiki ijao.
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Wapinzani kumuimarisha Prof. Lipumba Ngangari kung’olewa Sokoni, Ilala Polisi nchini hawajui mipaka ya kazi yao -OAU MAKALA
HABARI
ATV yatakiwa kuzingatia maadili Wakazi wa Tabata walalamikia athari ya maji machafu Maalim Seif akanusha madai ya kumwaga damu USHAURI NASAHA
MAKALA
MIPASHO NASAHA
KALAMU YA MWANDISHI
MAKALA
MWENYE MACHO…
MAKALA
LISHE
|
|
|
|
|