NASAHA
Na. 041 Jumatano Machi 29 - Aprili 4, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Ushauri Nasaha

Urafiki na makuzi ya mtoto 

NA KHADIJA IDD 

MAKUZI ya mtoto yanaweza kugawanywa katika nyanja kadhaa mfano makuzi ya kimiwili, kiakili, kimaono, kimaadilin.k. Katika makala hii tutajaribu kuona jinzi marafiki wanavyoweza kuathri ukuaji wa mtoto kimaadili. Upo msemo kuwa tabia ya mtu inaweza kueleweka vyema kwa kuzingatia tabia ya rafiki yake au marafiki zake. Msemo huu unatilia mkazo dhana nzima ya kuchagua marafiki wema ili kujenga tabia njema.
 

MALEZI ya mtoto huanzia nyumbani kwa wazazi wake. Kipindi cha awalicha maisha ya mtoto (miaka 0-2) mtoto huishi zaidi katika mazingira ya nyumbani natabia zake zote hutegemea tabia za watu wa nyumba husika. Baada ya hapo mtoto huanza kutokana kuchanganyika na watoto wa nyumba jirani pamoja na watu wa vimo tofauti na yake. 

Piakwa hali ilivyo sasa watotohuanza kwenda shule za awaliau madrasa (miaka 3-6). Baadaye hujiunga na shule za msingi kuanzia miaka 7 - 14 na hatimaye kuingia sekondariakiwa naumriwa mika 15-19. Tutaona kuwa umahiri wa stadi mbalimbali kama lugha, michezo,hobi na mengineyo hupatikana katika kipindi ambacho mtoto ameshaanza kuwa na maingiliano na watu wa nje ya familia yake. 

Tutakubaliana kuwa wazazi kama waalimu wa mwanzo kabisa wa mtoto watahusika sana na mustakabali mzima wa tabia za mtoto wao. Hawa ndiyo wenye jukumu la kumjengea msingi mzuri wa maadili ya jamii ambapo chimbuko la tabia njema hupimwa kutokanana jinsi mtu anavyoweza kutenda mambo yake kwa kuzingatia maadili ya jamiihusika. 

Katika nyumba ambaye maadili huchungwa watoto hujifunza pia kuchunga maadili. Marafiki katika familia hizi hulingana kabisa na familia husika katika suala zima la kuzingatia maadili. 

Utakapofika wakati wa mtoto kutoka nyumbani na kuingia mitaani tayari kuwa amejengewa msingi ambao utamsaidia kupata marafiki wema. Awali wazazi humsaidia mtoto kuchagua marafiki ambao huwa ni wale wanaotoka katika familia zenye maadili mema. 

Msingi huu pia humsaidia mtoto kuchagua hobi nzuri ambazo haziendi kinyume na maadili yajamii. Izingatiwe kuwa tabia za wizi, uvutaji wa bangi, madawa ya kulevya, utoro shuleni n.k. huigwa na watoto wakiwa katika vikundi. Kama wazazi watawaacha watoto wao bila kuwapa muongozo bora wa namna ya kupata marafikiwema basi wasishangae watoto wao kukosa kabisa makuzi mwema katika hii nyanja ya maadilina hivyo kuishia kuwa watu mizigo "liability" katika jamii. 
 
 

Juu
 

YALIYOMO
 

Tahariri
Tume ya Uchaguzi ipigwe msasa, sio wananchi

Mkapa awatahadharisha wanawake  CCM

Lipumba: Wananchi wana uwezo wa kuondoa utawala mbovu 

Wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuishitaki Serikali

Habari za ndani
Polisi hawana uwezo wa kuzuia mabadiliko’

Sherehe za mwaka mpya wa Kiislamu kufanyika Dar

MPASHO NASAHA
Hawavumi lakini...

Ushauri Nasaha
Urafiki na makuzi ya mtoto

MAKALA
Toba ya ‘Pope' liwe somo kwa utawala wa Mkapa

WAZO  LA  WIKI
Viva Senegal

MAKALA
Tatizo la ubakaji katika jamii yetu:
Mazingira katika shule zetu

Kalamu ya Mwandishi
Tahadhari isipochukuliwa huenda damu ikamwagika Zanzibar

MAKALA
Uchaguzi Mkuu Mwaka 2000 (4)

Habari za Kimataifa

Barua

Riwaya
Kisasi cha mauti

Lishe
Baba kulea ujauzito

MICHEZO

  • Ndoa ya Mobitel na Yanga mashakani
  • Homa ya pambano la Ghana na Stars yapanda

  • Makoye: Fedha za Simba nimetafuna mwenyewe 



     
     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com



     
     
     
     
     
     
     
     

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita