AN-NUUR
Na.162 Rabiul Thani 1419, Agosti 14 - 20, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Chakula na lishe
Njia bora ya kuandaa maji baridi

Na Mujahiid Mwinyimvua 

Watu wengi hupendelea kunywa maji ya baridi (cold water) hasa majira ya joto. Hata hivyo baadhi wa watu wanaandaa maji hayo kwa njia zilizo kinyume na kanuni za afya bora. 

Makala hii inalenga kuielimisha jamii kuhusu njia iliyo kinyume na kanuni za afya bora. Pia makala hii itawaelimisha wananchi njia bora (zinazokubalika na kanuni za afya) za kuandaa maji ya baridi. 

Njia mojawapo inayotumika na baadhi ya watu ya kuandaa maji ya baridi, ambayo ni kinyume cha kanuni za afya, ni ile ambayo mtu anachemsha maji ya kunywa, lakini katika kuyafanya maji hayo yawe baridi mtu anachanganya maji yaliyochemshwa na kipande cha barafu (maji yaliyoganda). 

Barafu hizo hutengenezwa kwa kutumia maji yasiyochemshwa au yasiyokuwa salama. Njia hii ni kinyume na kanuni za afya bora na ni ya hatari kwa sababu, barafu iliyotengenezwa kwa maji yasiyokuwa salama (yenye vijidudu) inaweza kusambaza vijidudu kwenye maji yaliyochemshwa. 

Kama tulivyoona katika makala zilizopita, kuwepo kwa vijidudu kwenye maji ni chanzo kikubwa cha magonjwa kama vile kipindupindu, kuharisha na homa ya matumbo. 

Njia tuliyoiona hapo juu ya waandaaji wa maji ya baridi inatokana na ufahamu mbaya kwa watu wanaotumia njia hiyo. Ufahamu waliokuwa nao ni kuwa maji yakiwekwa kwemye friza na kuganda huwa hayana tena vijidudu. 

Kwa maneno mengine, watu wanaotumia njia tuliyoiona hapo juu wanaamini kuwa friza au friji inaua vijidudu vilivyomo kwenye maji. Imani hiyo si sahihi. Usahihi ni kuwa, friji au friza hasa hizi za majumbani hazina ubaridi wa kuviua vijidudu vyote vilivyomo katika maji. 

Kinachotokea ni kwamba, vijidudu hivyo huwa haviwezi kuzaliana (kwa kasi kubwa). Lakini vikipata mazingira mazuri kama vile hali ya joto lililoko katika tumbo la mwanaadamu, vinaweza kuzaliana na hatimae kusababisha maradhi kwa binadamu aliyekuwa na vijidudu hivyo. 

Njia bora na ambayo inakubalika na kanuni za afya bora, ya kuandaa maji ya baridi ni kuwa, mtu achemshe maji ya kunywa na ayaache yapoe. Halafu ayatie katika chombo safi na chenye mfuniko. Baada ya kuyatia maji hayo katika chombo safi na kuyafunika, ayaweke maji hayo katika friji au friza kwa muda anaoutaka. 

Wakati wa kuyatumia maji hayo kama yamekuwa barafu (yameganda) au yamekuwa baridi zaidi, ayachanganye maji hayo kwa kutumia maji mengine yaliyochemshwa (ambayo hayajawekwa kwenye friza au friji). 

Napenda kuimalizia makala hii kwa kuwaomba wananchi wanaofanya biashara ya barafu au maji baridi, wafanye biashara hiyo kwa kutumia maji yaliyochemshwa. Vile vile serikali iwekeze zaidi katika sekta ya majisafi ili wananchi waweze kupata maji safi na salama kwa urahisi zaidi. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998: 
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa wafikia 258 
Na Mwandishi Wetu 

Wakuu wa mashule waache ubaguzi 
Na Mwandishi Wetu 

ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA 

Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa na Ukristo vimeshindwa 
Na Abdul Gullam 

Kina Ngatara na wenzake ndio urithi tulioachiwa na Wakoloni 
Na J. Hussein 

HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai, serikali imeumbuka 
Na Mwinjilisti Kamara Kusupa 

Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu tumejifunza nini? 
Na RAJAB RAJAB

MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Na Muhibu Said

Utangazeni Uislamu kwa nguvu zote – Sheikh Jongo
Na Badru Kimwaga

Salafiya wataka wanawake wawe macho na vyombo vya habari
Na Mwandishi Wetu

Waumini Misufini Morogoro waazimia kujenga Msikiti
Na Rajab Rajab, Morogoro

Serikali yatakiwa kuondoa askari Mwembechai
Na Badru Kimwaga

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo 

Chakula na Lishe  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita