AN-NUUR
Na.162 Rabiul Thani 1419, Agosti 14 - 20, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 
  

Uchunguzi uliofanywa kwa muda mrefu bandarini Zanzibar umebaini kuwa Zanzibar inaingiza kreti 325 za bia kila wiki kwa wastani. Idadi hii ni sawa na wastani wa kreti 1300 kwa mwezi ambazo soko lake ni Zanzibar na wale wanaokuja kwa muda. 

Mbali na ulevi huo wimbi kubwa limeendelea kuikumba Zanzibar kwa upande wa pombe za kienyeji. 

Hivi karibuni kumekuwako na ongezeko la kukamatwa kwa galoni, madebe na matangi (mapipa) ya pombe hiyo. Sehemu ambazo zimekuwa na mafuriko ya pombe hii ni Chukusani, Kisakasaka, Kisauni, Shakani, Kiyanga, Dole n.k. Nyingi ya sehemu hizi ni zile zenye wahamiaji Wakristo kutoka Tanzania Bara. 

Aidha imebainika kuwa wengi wa wapikaji wa ulevi huo ni hao hao wanaotoka Bara. 

Uchunguzi umebainisha zaidi kuwa waingizaji wakubwa wa pombe zitokazo nje ya Zanzibar ni Shirika la Utalii, Bottom’s Up, Golf Club, Scotch Store, Shangani Everest Trade, Prakash, Kampuni moja ya Dubai inayomiliki Duty Free Shop (Uwanja wa Ndege) n.k. 

Watu wa kati na wanaomiliki maduka ya pombe wamebainika ni watu wenye asili ya kiasia (Mabaniani au Magoa), Wakristo kutoka Tanzania Bara na Wazanzibari wanaomiliki mahoteli na mikahawa. 

Watumiaji wa pombe inayoingizwa, uchunguzi umebainisha kuwa ni wageni kutoka nje ya Tanzania, wafanyazi wa Taasisi za Muungano walio Zanzibar (hususan JWTZ) ambao wengi wao ni Wakristo na Wazanzibari wachache. 

Pamekuwepo na wasiwasi kuwa ongezeko hili ni katika mkakati maalumu wa kuifisidi Zanzibar kwani imebainika kuwa Sheria ya Utoaji leseni za vileo (pombe) imekuwa haifuatwi. 

Sheria hiyo inakataza ujenzi au ugeuzaji wa nyumba kuwa mabaa sehemu wanazoishi watu. 

Maduka ya pombe na mabaa yote yamo ndani ya sehemu za kuishi watu na yamekuwa yakiongezeka kila siku. Aidha wingi wa wamiliki hawa wa maduka haya na mabaa wanaonekana ni maajenti au wanafadhiliwa na nguvu zilizofichikana. 
 
 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Wapiganaji wa Kiislamu wa Twalaban nchini Afghanistan wameuteka mji wa Taloqan ulioko kaskazini mashariki ya nchi hiyo. 

Taarifa kutoka Afghanistan zinafahamisha kwamba wapiganaji hao wameukamata mji huo baada ya kuyazidi nguvu majeshi ya upinzani. 

Wapiganaji hao ambao wamedhamiria kusimamisha serikali ya Kiislamu nchini humo, wameukamata mji huo ulio umbali wa kilometa 240 katoka mji wa Kabul, katikati ya wiki hii. 

Jeshi la Twalaban lilianza mapambano dhidi ya Serikali ya Afghanistan kufuatia viongozi wa serikali hiyo kushindwa kutekeleza ahadi walizozitoa wakati wa kushika madaraka. 

Kikosi cha Tawalaban kiliundwa na wahadhiri wa vyuo, wanafunzi wa vyuo, shule za sekondari na vijana wengine ambao wengi wao ni wanafunzi wa aliyekuwa mwanachuoni na mwanaharakati maarufu wa Kiislamu duniani, Sayyid Abul A’la Maududi. 

Kikosi hiki cha vijana wa Kiislamu awali kiliingia vitani dhidi ya majeshi ya Urusi ambayo yalivamia nchi hiyo mwaka 1980. Baada ya kuyasukuma nje ya nchi majeshi hayo ya uvamizi, kiligeuza mtutu kwa vibaraka wake wakiongozwa na dikteta Najibullah hadi kuung’oa utawala wa kikomunisti nchini humo. 

Hata hivyo licha ya ushindi ilioupata, Twalaban inadharamia kufanya mazungumzo na makundi ya upinzani ili upatikane muafaka utakaopelekea amani ya kudumu nchini humo chini ya Sheria ya Kiislamu. 
 
 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

KITENGO cha uchapishaji cha Mfalme Fahd hivi karibuni kimechapisha kitabu cha rejea ya tafsiri ya Qur’an ambacho kitajulikana kwa jina la "Qur’an Interpretation made simple." 

Waziri wa Mambo ya Kiislamu, Tabligh na Malezi wa Saudi Arabia, Bw. Abdullah el Turki, amerioitiwa kusema kwamba kitabu hicho kitatumika kama rejea katika uandishi wa Tafsiri utakaofanywa siku za usoni. 

Aidha, Bwana el Turki aliongeza kusema kuwa kitabu hicho huenda kikakidhi hitajio la kuwa na tafsiri za Qur’an ambazo zitakuwa nyepesi kueleweka kwa wasomaji. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998: 
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa wafikia 258 
Na Mwandishi Wetu 

Wakuu wa mashule waache ubaguzi 
Na Mwandishi Wetu 

ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA 

Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa na Ukristo vimeshindwa 
Na Abdul Gullam 

Kina Ngatara na wenzake ndio urithi tulioachiwa na Wakoloni 
Na J. Hussein 

HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai, serikali imeumbuka 
Na Mwinjilisti Kamara Kusupa 

Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu tumejifunza nini? 
Na RAJAB RAJAB

MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Na Muhibu Said

Utangazeni Uislamu kwa nguvu zote – Sheikh Jongo
Na Badru Kimwaga

Salafiya wataka wanawake wawe macho na vyombo vya habari
Na Mwandishi Wetu

Waumini Misufini Morogoro waazimia kujenga Msikiti
Na Rajab Rajab, Morogoro

Serikali yatakiwa kuondoa askari Mwembechai
Na Badru Kimwaga

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo 

Chakula na Lishe  
 
 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita