AN-NUUR
Na.162 Rabiul Thani 1419, Agosti 14 - 20, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 Athari ya milipuko Dar, Nairobi:
Waliokufa wafikia 258

Wengi watuma rambirambi na misaada 

Vyombo vya habari vyaitaka serikali iache papara 

Na Mwandishi Wetu 

Idadi ya watu waliokufa katika milipuko ya mabomu mjini Dar es Salaam na Nairobi imedaiwa kufikia 258 hadi kufikia jana, 248 wakiwa ni waliokufa Nairobi na 10 Dar es Salaam. 

Waliokufa katika tukio la Dar es Salaam wametajwa kwamba ni Ramadhani Mahundi, Mtendeje Rajabu, Abbas William na Omar Ahmed Nyumbu. Wengine ni Abdallah Mohamed, Dotto Selemani, Abrahman Abdallah; Hassan Siyad na Yusuf Shamte. Maiti moja ilikuwa haijatambuliwa. 

Msiba huu mkubwa umesababishwa na milipuko miwili mikubwa katika Balozi za marekani jijini Dar es Salaam na Nairobi Ijumaa ya Agosti 7; 1998. 

Serikali kupitia viongozi wake wa ngazi za juu; imeeleza kushtushwa kwake na tukio hilo na kwamba itafanya kila iwezalo kuwapata watu waliohusika. 

Aidha watu binafsi, mashirika yasiyo ya kiserikali na nchi za nje zimekuwa zikitoa salamu za rambirambi; pole na misaada ya matibabu. 

Wakati askari wa Israel wamekuwa wakishiriki katika zoezi la kuwaokoa walionasa katika vifusi vya majengo yaliyobomoka 

mjini Nairobi. Serikali ya Misri imetuma madaktari na tani mbili za madawa. Saudi Arabia nayo imeripotiwa kutuma ndege ya msaada kwa ajili ya waathirika wakati inasemekana kwamba serikali ya Canada imetoa msaada wa shilingi milioni 45. 

Wakati juhudi za Serikali ya Tanzania ikishirikiana na vyombo vya usalama vya Marekani; ikiendelea na juhudi zake za kuwatafuta wahusika imeripotiwa kwamba Waislamu nchini Kenya wanalalamika kuwa wamekuwa wakinyanyaswa toka kutokea kwa mlipuko huo. 

Taarifa za vyombo vya habari zimedai kwamba vijana wa Kiislamu na baadhi ya waalimu wa dini wamekuwa wakikamatwa bila maelezo yoyote. Naibu Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu nchini Kenya (SUPKEM) amewataja watu waliokamatwa na polisi kuwa ni Amjad Javed na Mwalim wa Dini Abdulrazak Qare aliyekamatwa huko Isiolo. Mwalimu Abdulrazak ana asili ya Pakistani. 

Aidha Sheikh Ibrahim amekaririwa alisema kwamba vijana wawili raia wa Kenya wenye asili ya Kiarabu walikamatwa mjini Nairobi na haijulikana wanakoshikiliwa. 

Nalo Baraza la Ushauri la Waislamu wa Kenya limelaani kitendo cha gazeti la ‘East Africa Standard’ la Jumatano Agosti 12, kuchapisha Katuni ikionyesha Muislamu akiswali kando ya bango lililoandikwa "Kambi ya Ugaidi". 

Wakati huo huo, baadhi ya vyombo vya habari vimeitaka serikali kuchukua hadhari katika zoezi la kuwasaka waliohusika na mlipuko wa mabomu katika Ubalozi wa Marekani. 

Vyombo hivyo vimeishauri serikali iacha papara inayoashiria kujitokeza katika usakaji wa watuhumiwa. 

Ushauri huo umekuja kufuatia kukamatwa kwa watu 14 ambao imedaiwa ni raia wa nchi za Sudan, Iraq, Somalia na Uturuki. Ambapo masaa machache baadaye ikaripotiwa kwamba mmoja wa watuhumiwa hao mwenye asili ya Kisomali ni mfanyakazi wa shirika moja la Umoja wa Mataifa ambaye kituo chake cha kazi ni mkoa wa Kigoma. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998: 
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa wafikia 258 
Na Mwandishi Wetu 

Wakuu wa mashule waache ubaguzi 
Na Mwandishi Wetu 

ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA 

Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa na Ukristo vimeshindwa 
Na Abdul Gullam 

Kina Ngatara na wenzake ndio urithi tulioachiwa na Wakoloni 
Na J. Hussein 

HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai, serikali imeumbuka 
Na Mwinjilisti Kamara Kusupa 

Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu tumejifunza nini? 
Na RAJAB RAJAB

MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Na Muhibu Said

Utangazeni Uislamu kwa nguvu zote – Sheikh Jongo
Na Badru Kimwaga

Salafiya wataka wanawake wawe macho na vyombo vya habari
Na Mwandishi Wetu

Waumini Misufini Morogoro waazimia kujenga Msikiti
Na Rajab Rajab, Morogoro

Serikali yatakiwa kuondoa askari Mwembechai
Na Badru Kimwaga

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo 

Chakula na Lishe  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita