AN-NUUR
Na.162 Rabiul Thani 1419, Agosti 14 - 20, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 

Yawashukuru wafadhili toka nchi za Kiarabu 

Aboud Jumbe ataka amana itunzwe 

Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Serikali imesema kwamba inathamini sana huduma za elimu, afya na ustawi wa jamii zinazotolewa na mashirika ya kidini. 

Aidha Serikali imetoa shukurani kwa wahisani wa miradi hiyo na kusisitiza kwamba Serikali inathamini sana juhudi za mashirika ya dini kwa mchango wake katika kuboresha huduma za jamii na kutoa misaada ya kibinaadamu. 

Hayo yapo katika salamu za Serikali za hivi karibuni katika hafla rasmi ya ufunguzi wa ‘Markaz Al Hudaa’ mjini Moshi ambayo ni taasisi rasmi ya huduma za Elimu, afya na 

ustawi wa jamii. Taasisi hiyo inamilikiwa na Shirika lenye Makao yake makuu Kuwait. 

Akiwasilisha salamu hizo za Serikali kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Prof. Philemon Sarungi; Afrisa Elimu Bw. Majili aliwataka wasimamizi wa Taasisi hiyo wafikishe salamu na shukrani za dhati za Mkuu wa Mkoa na Serikali kwa ujumla kwa Shirika la Africa Muslim Agency na kwa wahisani wote wanaochangia huduma hizo. 

Kituo hicho cha Al-Hudaa kipo kata ya Kaloleni katika manispaa ya Moshi na kinajumuisha Al-hudaa Secondary School, Al-hudaa Daru-aytama; Eh-Ahsa Health Centre na Darul-Muuminat Vocatinal Centre. 

Taasisi zote hizo zishaanza kufanya kazi ambapo nyumba ya yatima inalea watoto 72, wakati Chuo cha ufundi kimesajili wanawake 25 ambao hujifunza ushonaji, misingi ya uhasibu, hisabati. lugha ya kiingereza na Maarifa ya Uislamu. Shule ya Sekondari itakuwa na kidato cha kwanza hadi cha sita. 

Mzee Aboud Jumbe, Rais Mstaafu wa Zanzibar ambaye alikuwa mgeni Rasmi katika sherehe hizo aliwaomba watakaonufaika na huduma hizo wazienzi na kwamba hiyo ni amana toka kwa Mola wao. 

Miongoni mwa wageni waliohudhuria sherehe hizo ni Sheikh Muhammad Al-Khamis toka Kuwait; Sheikh Twariq Al-Muhsin na Mar’wa Algamzi kutoka Emarati. 

Wao ni miongoni mwa Waislamu ambao swadaka zao husaidia kuendesha huduma hizo. Akielezea msimamo wa Shirika lake, Mkurugenzi wa Africa Muslim Agency Ofisi ya Dammam Sheikh Muhammad Al-Khamis alisema kuwa Waislamu wenye azma ya kutumia kile walichoruzukiwa kwa njia ya Allah wameamua kutoa huduma mbalimbali ili Waislamu na jamii kwa ujumla ifaidike kwazo. 

Africa Muslim Agency ina Ofisi kuu mjini Dar es Salaam ikiongozwa na Sheikh Shakir; wakati ile ya Kanda ya Kaskazini (Moshi) inaongozwa na Sheikh Majid. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998: 
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa wafikia 258 
Na Mwandishi Wetu 

Wakuu wa mashule waache ubaguzi 
Na Mwandishi Wetu 

ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA 

Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa na Ukristo vimeshindwa 
Na Abdul Gullam 

Kina Ngatara na wenzake ndio urithi tulioachiwa na Wakoloni 
Na J. Hussein 

HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai, serikali imeumbuka 
Na Mwinjilisti Kamara Kusupa 

Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu tumejifunza nini? 
Na RAJAB RAJAB

MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Na Muhibu Said

Utangazeni Uislamu kwa nguvu zote – Sheikh Jongo
Na Badru Kimwaga

Salafiya wataka wanawake wawe macho na vyombo vya habari
Na Mwandishi Wetu

Waumini Misufini Morogoro waazimia kujenga Msikiti
Na Rajab Rajab, Morogoro

Serikali yatakiwa kuondoa askari Mwembechai
Na Badru Kimwaga

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo 

Chakula na Lishe  

 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita