AN-NUUR
Na.162 Rabiul Thani 1419, Agosti 14 - 20, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Inaendelea kutoka toleo lililopita... 

Abu Ameena: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Nilijiunga na chuo kikuu cha Kiislamu Madina na kupata shahada ya Usuli diin mwaka 1979. Mwaka 1985 nilipata shahada ya pili katika Theolojia ya Kiislamu na mwaka 1994 nikapata Ph.D. 

Nilifundisha elimu ya Kiislamu na lugha ya Kiarabu katika mashule binafsi mjini Riyadh kwa muda wa miaka 10. Na miaka mitatu baadae nikawa Mhadhiri wa Islamic Studies katika Chuo Kikuu cha Kiislamu Jijini Cotabato nchini Philippines. Wakati huo huo nikiwa mhadhiri katika chuo cha Kimarekani katika falme za Kiarabu. 

Nilivyo fanya Daawah katika kambi za jeshi la Marekani Ghuba. 

Wakati wa vita vya Ghuba, nilifanya kazi ya Da’awah miongoni mwa askari wa Marekani kupitia idara ya mambo ya dini ya kikosi cha anga cha jeshi hilo. Askari wa Marekani kama ilivyo kwa watu wa Magharibi walikuwa wakiuelewa vibaya Uislamu. Wanajeshi hao walipewa amri ya kutosogea futi 10 kutoka misikitini. 

Kinyume na amri hiyo sisi tuliwachukua hadi misikitini. Walivutiwa mno na jinsi mazingira ya ndani ya misikiti yalivyo. Hawakuona humo jambo lolote la kustaajabisha zaidi ya miswala. Wakati walipofika nchini Saudi Arabia walishangazwa kuwaona wanawake wa Kiislamu wakiwa katika vazi la Hijab. Waliwapa jina la utani UBO (Unidentified Black Objects) yaani "maumbile meusi yasiyo tambulika." Lakini kadri walivyoendelea kuzoea mazingira ya Saudi Arabia ndivyo walivyozidi kufunguka macho na fahamu. Walishuhudia ukarimu waliotendewa na mabedui (watu wa jangwani). 

Mabedui hao walikuwa wakitembelea mahema ya askari hao wa Marekani na kugawa tende na maziwa. Askari hao hawakuuona ukarimu huu Korea, Japan wala mahali pengine popote pale ambako jeshi hilo limekuwa na vituo kwa miongo kadhaa. 

Kutokana na mazoeano ya miezi kadhaa na vikosi hivyo, baada ya vita kumalizika nilipata fursa ya kwenda Marekani ambako nilifungua ukurasa mpya wa Uislamu katika idara ya ulinzi ya nchi hiyo. 

Nakisia askari wapatao 3000 wa jeshi la Marekani wamesilimu, wengi wakiwa wamesilimu kipindi kile kile cha vita Ghuba. Niamini nikisema kwamba Saudi Arabia ni mahali pekee duniani ambako askari wa Kimarekani wameshindwa kuacha watoto wa vita", hali kadhalika pamoja na ulevi uliokithiri kwa askari hao, pombe ilinywewa kwa nadra. 

Nikiwa India 

Kwa mara ya kwanza nilizuru India mwaka 1991. Hii ilikuwa wakati nafanya utafiti. 

Nchini India nilikutana na Waislamu wa Jimbo la Kaskazini. Waislamu niliokutana nao walikuwa wamezama kwenye mambo ya ushirikina. Ushirikina ulifanywa sehemu ya ibada. 

Mara yangu ya pili kutembelea India ilikuwa mwaka jana (1997), safari hii ilinichukua hadi mji wa Karala. 

Mjini Karala kuna jumuiya za Kiislamu kama Jamaat Islam na Islamic Research Foundation ambazo zinafanya kazi nzuri ya Da’awah. 

Da’awah ya Jumuiya hizi imelenga vyuo vikuu na wasomi wengine katika taasisi mbali mbali ipo pia Jumuiya ya Tabligh ambayo harakati zake zimeelekea zaidi misikitini. 

Kwa hali niliyoiona India, ningependa kushauri kwamba ipo haja kwa jumuiya za Kiislamu kushirikiana. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998: 
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa wafikia 258 
Na Mwandishi Wetu 

Wakuu wa mashule waache ubaguzi 
Na Mwandishi Wetu 

ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA 

Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa na Ukristo vimeshindwa 
Na Abdul Gullam 

Kina Ngatara na wenzake ndio urithi tulioachiwa na Wakoloni 
Na J. Hussein 

HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai, serikali imeumbuka 
Na Mwinjilisti Kamara Kusupa 

Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu tumejifunza nini? 
Na RAJAB RAJAB

MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Na Muhibu Said

Utangazeni Uislamu kwa nguvu zote – Sheikh Jongo
Na Badru Kimwaga

Salafiya wataka wanawake wawe macho na vyombo vya habari
Na Mwandishi Wetu

Waumini Misufini Morogoro waazimia kujenga Msikiti
Na Rajab Rajab, Morogoro

Serikali yatakiwa kuondoa askari Mwembechai
Na Badru Kimwaga

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo 

Chakula na Lishe  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita