|
|
|
Kwa mara nyingine Serikali imetoa pongezi na kuzishukuru taasisi za kidini kwa mchango mkubwa zinazotoa kuboresha huduma za elimu, afya na jamii kwa ujumla. Kama alivyozungumza Afisa Elimu wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa akifungua kituo cha Markaz El-Hudaa; huduma hizi ni za thamani kubwa kwa Watanzania na hapana budi kuwashukuru wahisani wahusika. Tungependa tuungane na Serikali katika kutambua na kuthamini misaada katika huduma za jamii zinazotolewa na mashirika ya dini na hivyo kuyapa moyo yazidishe juhudi zake. Aidha pamoja na kwamba yapo mashirika mengi ya dini yanayofanya shughuli mbalimbali kuwasaidia Waislamu na Watanzania kwa ujumla; tungeyaomba yaige mfano wa Africa Muslim Agency ambayo imelenga katika ile miradi ambayo hasa ndio kilio cha Waislamu. Suala la kujenga na kuendesha mashule, mahospitali na miradi mingine mikubwa kama hiyo ni suala linalohitaji nguvu kubwa inajumuisha misaada toka sehemu mabalimbali. Umuhimu wa misaada hiyo ya mashirika ya dini unapata nguvu zaidi ikizingatiwa kwamba uwezo wa Serikali yetu kutoa huduma muhimu kwa jamii unazidi kupungua mwaka hadi mwaka. Na pengine ni kwakuzingatia ukweli huo Mabaraza ya Kikristo yaliingia mkataba na Serikali ya Tanzania, maarufu kwa ‘Memorandum of Understanding" ambapo misaada ya Kielimu na Afya kwa Tanzania toka kwa Serikali za nchi kama Ujerumani itakuwa ikipitia katika mashirika ya Kikristo. Aidha Serikali ya Tanzania inawajibika kuyaombea misaada mashirika hayo ya Kikristo toka nchi za nje. Tunaimani kwamba kwa msimamo huu wa Serikali Mashirika ya Kidini toka nchi mbalimbali za Ulaya; Arabuni, Asia n.k. yataitumia fursa hii kuwahudumia waumini wao na wananchi kwa ujumla ili kuimarisha imani zao na kuboresha maisha yao. Kwa upande mwingine tungependa tutoe wito kwa wananchi kwamba wawe ni wenye kuenzi na kutunza miradi na huduma mbalimbali zinazotolewa na mashirika ya dini ili lengo lililokusudiwa liweze kufikiwa. |
Serikali yaipongeza Africa Muslim
Agency
Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba
1998:
Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa
wafikia 258
Wakuu wa mashule waache ubaguzi
ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi Twalaban wadhibiti Afghanistan yote Madina yachapisha kitabu cha rejea MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa
na Ukristo vimeshindwa
Kina Ngatara na wenzake ndio urithi
tulioachiwa na Wakoloni
HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai,
serikali imeumbuka
Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu
tumejifunza nini?
MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu
na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Utangazeni Uislamu kwa nguvu
zote – Sheikh Jongo
Salafiya wataka wanawake
wawe macho na vyombo vya habari
Waumini Misufini Morogoro
waazimia kujenga Msikiti
Serikali yatakiwa kuondoa
askari Mwembechai
|