NASAHA
Na. 045 Jumatano Aprili 26 - Mei 2, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Wakati Kanisa Katoliki likitoa miongozo ya kisiasa:
Sheikh mwingine ahojiwa Mwanza

Na Mwandishi Wetu Mwanza

POLISI mjini Mwanza ilimkamata na kumhoji kiongozi wa dini ya Kiislamu,Sheikh Adailla Abdulkadir kwa madai ya kuzungumzia siasa kwenye mihadhara ya dini.

Sheikh huyo ambaye ni Imamu wa msikiti wa AL-Asays uliopo Makongoro mjini hapa, alikamatwa saa mbili ya usiku Ijumaa iliyopita akidaiwa kuruhusu kuandaliwa kwa kongamano ambalo lingezungumzia masuala ya "kuchanganya dini na siasa "kwenye msikiti wake. Imamu huyo alikamatwa na kuhojiwa katika kituo cha polisi cha Kati kwa masaa kadhaa. 

Akielezea juu ya kukamatwa kwake, Sheikh Abdulkadir alisema kuwa aliwaeleza Polisi kwamba yeye kama kiongozi wa msikiti ambayo ni nyumba ya Mwenyezi Mungu, asingeweza kuwazuia waumini wake waliomchagua kuitumia nyumba hiyo kuzungumza chochote kinachoruhusiwa na dini. Alisema kuwa siasa ni sehemu ya dini na haviwezikutenganishwa, kwani kuzungumzia siasa ni sawa na kuzungumzia dini. Imamu Abdurkadir aliachiwa bila masharti yoyote baada ya mahojiano. 

Wiki iliyopita polisi walimkamata mhadhiri maarufu mjini hapa ustaadh Ilunga Hassan Kapungu kwa madai hayo ya kuchanganya dini na siasa kwenye mihadhara ya waislamu. 

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi wa mkoa kuzungumzia kadhia hiyo hazikufanikiwa. 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Acheni  kuwacheza shere Waislamu, ondoeni udini

Serikali iache udini, kuwagawa wananchi - Sheikh  Mbukuzi

Wakati Kanisa Katoliki  likitoa miongozo ya kisiasa:
Sheikh mwingine ahojiwa Mwanza

Hakuna maendeleo bila Demokrasia -  Lipumba

MPASHO NASAHA
KAMCHEZO  AU?

HABARI
Sheikh Jongo asababisha mtafaruku mbele ya Al-Haji Mwinyi

‘Suala la kuirekebisha jamii lisiachwe mikononi mwa Serikali pekee’

Jiandikisheni na pigeni kura -Balozi

Tanzania kufutiwa madeni:
Wananchi hawatarajii nafuu yoyote

Ushauri Nasaha
Vyombo vya habari na vijana  - 2

MAKALA
Sababu ‘1000’ kwanini tunataka CCM ing’oke madarakani - 4

Kalamu ya Mwandishi
Muungano watimiza miaka 36 kwa migogoro

MAKALA
Chama cha Mapinduzi na sera za maendeleo (1)

Lishe
Jinsi ya kutunza virutubisho wakati wa maandalizi ya vyakula

Habari za Kimataifa

RIWAYA
Maisha mema ya akhera

MASHAIRI

MICHEZO

  • Raoul Shungu apigwa ‘Dafrao’ 
  • Yanga wamfurusha Waziri Mudhihir uwanjani
  • Simba wampongeza Msajili wa Vyama

  •  

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita