AN-NUUR
Na.168 Jamadul Akhir 1419, Septembe 24 - Oktoba 1, 1998

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita

 

LISHE

Matatizo ya tumbo yanayosababishwa na utumiaji wa maziwa

Na Mujahiid Mwinyimvua

BAADHI ya watu hupata matatizo ya tumbo mara tu wanapokunywa maziwa. Matatizo hayo ni kama vile kuliona tumbo zito, kujaa gesi (hewa) na wengine hufikia hatua ya kuharisha.

Mtu mwenye hali hiyo hujulikana kuwa ana tatizo la tumbo lake kushindwa kusaga chakula cha Laktosi (Lactose). Kwa kimombo hali hiyo hujulikana kama Lactose intolerance.

Takriban watu asilimia sabini (70%) duniani wanasumbuliwa na Lactose intolerance. Tatizo hilo linaweza kuleta athari mbaya katika lishe ya binadamu, hivyo basi ni vyema tukaitazama dhana hiyo japo kwa kiasi kidogo.

Katika maziwa kuna virutubisho kadhaa, kimojawapo kinaitwa Lactosi (Lactose).

Kimaumbile, mwili (utumbo) wa binadamu una vitu vinavyosaga chakula. Vitu hivyo vinaitwa vimeng'enyo (Enzymes).

Aina moja ya kimeng'enyo ni Lactase, 'Lactase' husaga chakula kinachoitwa laktosi (ambacho nimekitaja awali) na baada ya kusagwa hutumiwa na mwili.

Mtoto anapozaliwa huwa na kimeng'enyo lactase ambacho humwezesha kusaga maziwa anayonyonya kutoka kwa mamake.

Mtoto anavyozidi kukua ndivyo idadi ya 'Lactase' inavyopungua. Kwa baadhi ya watu wazima 'Lactase' hupotea kabisa (haizalishwi).

Inapotokea hali hiyo, Laktosi ya kwenye maziwa anayonyonya mtu huwa haisagwi kwa njia ya kawaida na yenye manufaa katika mwili.

Badala yake, bakteria (vijidudu) waliomo katika utumbo hukisaga chakula hicho (Laktosi) na kutoa hewa/gesi (CO2 na H2).

Hewa hiyo hulifanya tumbo kujaa na kwa baadhi hufikia hatua ya kuharisha. Kitendo cha kuharisha ni cha hatari, kwa sababu kinapoteza maji na virutubisho vingine.

Baadhi ya watu hasa wafugaji huwa hawana kabisa matatizo ya 'Lactose intolerance'. Sababu ya hali hiyo bado haijawa wazi kwa wanasayansi.

Hivyo, elimu ya sayansi inasaidia kwa kiwango kikubwa kukabiliana na tatizo la 'Lactosse Intolerance'. Mbinu ya kwanza ni kuwa, watu wenye matatizo watumie maziwa yaliyochachuka ( mtindi/yoghurt).

Mbinu ya pili, ni kunywa maziwa pamoja na kitu kinachoitwa 'Lact-Aid'. Kitu hicho kinafanya kazi kama 'Lactase (kimeng'enyo). 'Lact-Aid hupatikana maduka ya dawa, maduka ya vyakula n.k.

Watu wenye matatizo ya 'Lactose Intolerance' wasisuse kutumia maziwa bali wafuate ushauri wa hapo juu.

Maziwa ni chakula kizuri na ni chanzo muhimu cha madini ya Kasiam (Calcium). Madini hayo muhimu zaidi kwa kina mama wanaonyonyesha na wale wajawazito.

Kwa wale wanaotumia, watumie maziwa yaliyoongezwa vitamini D. Vitamini D ni muhimu pamoja na kazi nyingine kuuwezesha mwili kuweza kuyatumia vizuri madini ya Kasiam. 

Juu 
 

YALIYOMO  
 
TAHARIRI 
Iran ina agenda gani?

Mauaji,udhalilishaji Mwembechai: Wanawake Waislamu waandamana Tabora Na Mwandishi Wetu

BUCHA YA NYAMA YA NGURUWE KATIKATI YA WAISLAMU
Na Mwandishi Wetu

'Serikali ieleze hatua iliyochukua kuhusu mauaji Mwembechai'
Na Kassim Juma

Vijana wa Kiislamu wajiimarisha Bukoba
Na Nooh Mustafa, Bukoba

Sheikh Mzonge awataka Waislamu Moshi wasimamishe swala
Na Ashraf Yussuf, Moshi

TAMKO LA PAMOJA LA MISIKITI SABA YA MWANZA-KUPINGA OMBI LA BAKWATA KWA SERIKALI LA KUIFUTIA USAJILI WAKE

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 7

MAKALA: Baadhi ya Watanzania wangali wanaishi ‘Tanganyika’
Na Mwandishi Wetu

HOJA BINAFSI: Maendeleo ya Tanzania ni ndoto
Na Fatma Mussa

‘Musiwasingizie wake zenu maovu’
Na Habiba Swedi, Arusha

Wanafunzi Waislamu Songea wapata viongozi
Na Mwandishi Wetu, Songea

Kikundi cha wanawake wa Kiislamu Bi. Khadija – Dodoma
Na Abu Zuberi, Dodoma

Waahidi kutekeleza majukumu kwa jina la Allah
Na Habiba Swedi, Arusha

Arumeru wahitaji Da’awa
Na habiba Swedi, Arusha

Wanawake wa Kiislamu wazungumzia maendeleo yao

Kauli ya wanawake wa Kiislamu Iringa kuhusu kadhia ya Mwembechai

Uislamu ulivyoingia Zanzibar

Wanawake Singida walaani mauaji Mwembechai Wamchangia Mama Chuki 17,000/-
Na Mwandishi Wetu

Sekondari ya Kiislamu kujengwa Maere Tanga
Na Abu Abdullah, Tanga

Sheikh ahimiza Waislamu Lindi wafuate mafunzo ya Uislamu
Na Mohamed Mussa, Lindi

Sheikh Zuberi awataka Waislamu Dodoma kuimarisha Misikiti
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Mafundisho ya Quran 
Dhikiri maana yake nini? - 2

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matatizo ya tumbo yanayosababishwa na utumiaji wa maziwa

Matangazo 
 

 

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org  

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita