|
AN-NUUR
|
BUCHA YA
NYAMA YA NGURUWE KATIKATI YA WAISLAMU
Na Mwandishi Wetu WAISLAMU wa Mirerani wiki iliyopita waliazimia 'kulishughulikia' bucha moja la nyama ya nguruwe mjini hapo baada ya malalamiko yao kutokusikilizwa. Haikuweza kufahamika mara moja kwamba ni hatua gani wangechukua, lakini Waislamu hao walikuwa wameamua kuswali Ijumaa ya pamoja ambapo baada ya swala wangepeana maelekezo nini cha kufanya. Ijumaa hiyo maalum ilikuwa iswaliwe Septemba 18, mwaka huu. Hata hivyo, muda mfupi kabla ya Ijumaa hiyo kusimama, uongozi wa serikali ngazi ya kata ulileta barua kwa Waislamu ikieleza kwamba serikali inachukua hatua kuondoa bucha hiyo. Barua hiyo yenye kumb. Na. WEO/MRN/ML/Vol.11/78 ya Septemba 18 kutoka ofisi ya Mtendaji Kata iliwaarifu Waislamu kwamba bucha hilo la nyama ya nguruwe litahamishiwa sehemu nyingine isiyo na madhara na Waislamu. Bucha hilo linalomilikiwa na Bw. E. Urio lipo mtaa wa Zaire eneo la Kijiweni ambapo ni eneo la maduka na makazi ya watu. Awali, Waislamu wa Mirerani waliandika barua serikalini kulalamikia kuwepo kwa bucha hilo ambalo walidai kwamba mara nyingi nyama ya ng'ombe na nguruwe imekuwa ikipimwa kwenye mizani moja. |
YALIYOMO
TAHARIRI Iran ina agenda gani? Mauaji,udhalilishaji Mwembechai: Wanawake
Waislamu waandamana Tabora Na Mwandishi Wetu 'Serikali ieleze hatua iliyochukua
kuhusu mauaji Mwembechai' ‘Musiwasingizie wake zenu maovu’
Barua za wasomaji
|
Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua kwa: webmaster@islamtanzania.org