AN-NUUR
Na.168 Jamadul Akhir 1419, Septembe 24 - Oktoba 1, 1998

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita

 

'Musiwasingizie wake zenu maovu'

Na Habiba Swedi, Arusha

WANAUME wa Kiislamu wameonywa dhidi ya tabia ya kuwasingizia uovu wake zao, na badala yake wametakiwa kuwaamini, kuwapenda, kuwasaidia na kuwausia kheri ili wote mke na mume wapate radhi ya Mwenyezi Mungu.

Onyo hilo limetolewa na Sheikh Swaleh bin Said wakati akitoa hotuba katika Swala ya Ijumaa hivi karibuni kwenye Msikiti wa Zawiyatul Qadiriya, Ngarenaro mjini hapa.

Akitoa mifano mbalimbali ya maisha ya kila siku, ambapo mume hutoa idhini kwa mkewe kuhudhuria madrasa, kwenda kazini,harusini, sokoni na kwingineko, lakini alistaajabu kwa kusema kuwa mume humgeuka mkewe pindi anapochelewa kurudi nyumbani na kuanza kumsingizia maovu mkewe huyo.

Alizidi kufahamisha kuwa, mume katika maisha ya ndoa ya Kiislamu ni budi awe makini kwa mkewe dhidi ya kila analotamka na kwamba azingatie mipaka ya sheria iliyowekwa na Allah ndani ya Qur'an na mafundisho ya Mtume (saw) ili kuwa na ndoa zenye furaha na amani.

Sheikh Swaleh alisisitiza kwamba, mume kumsingizia mkewe uovu, ni kinyume kabisa na mafundisho ya Allah kwani huleta fitna katika ndoa na jamii ya Waislamu kwa ujumla na Mwenyezi Mungu amelikemea vikali ikiwa ni pamoja na kuliwekea adhabu ya kupigwa viboko kwa kila afanyaye hivyo.

Akapambanua wazi kuwa, mke anayo sheria inayomlinda dhidi ya kusingiziwa huko endapo atashitaki katika vyombo vya dini.

Akinukuu aya katika Qur'an Sheikh Swaleh alisema: "Na wale wanaowasingizia wake zao, na hawana ushahidi ila nafsi zao Mwenyezi Mungu anakunasihini msirudi nyuma kabisa kufanya haya, ikiwa ninyi ni Waislamu wa kweli".

Kwa mafundisho ya Mtume, Sheikh Swaleh alitoa hadithi inayokataza Waislamu kushiriki mambo saba yanayoangamiza, mojawapo likiwa hilo la kuwasingizia wake maovu.

Aliongeza kuwa mke amepewa heshima kubwa sana katika Uislamu, hivyo anastahili asitiriwe.

Pamoja na hilo, Sheikh Swaleh alipinga vikali propaganda za baadhi ya watu kuwa Uislamu unamkandamiza mke na kumpa nguvu mume kumwonea, kumsingizia ama kumtukana namna atakavyo.

Waislamu mbalimbali walitoa maoni yao juu ya hotuba hiyo, Bi. Sadia Swaleh wa Mji wa Kati Arusha alionyesha kuvutiwa sana na hotuba kwa kusema kuwa inaigusa jamii ya Kiislamu kwani hayo hutokea kila siku katika maisha ya ndoa kiasi cha kuwa chanzo cha migogoro mingi inayopelekea talaka.

Naye Ustaadh Khamswaan wa Yam Investment alisema kuwa, inafurahisha na kutia moyo kuona kuwa viongozi wa dini wanakemea maovu yanayotendeka kila siku katika familia za Kiislamu.



Wanafunzi Waislamu Songea wapata viongozi

Na Mwandishi Wetu, Songea

JUMUIYA ya wanafunzi Waislamu wanaosoma katika sekondari na vyuo mbalimbali mkoani Ruvuma wamefanya uchaguzi na kupata viongozi wapya watakaondesha shughuli za kidini katika jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka 1998 - 99.

Jumuiya hiyo inaundwa na shule tano za sekondari na vyuo viwili katika wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Shule hizo ni Songea Boys na Songea Girls, shule nyingine ni pamoja na sekondari ya kutwa ya Ruvuma, sekondari ya Rukuwiko na sekondari ya Kiislamu ya Msamala.

Aidha, jumuiya hiyo inaundwa pia na vyuo vya Ualimu Matogaro TTC na Chuo cha Waganga Wasaidizi wilayani Songea COTC.

Uchaguzi huo ulifanyika katika chumba cha mikutano cha TTC siku ya Jumapili Septemba 9, mwaka huu.

Waliochaguliwa kutoka Songea Boys ni Hamza Makila kuwa Mwenyekiti, Luhunilo alichaguliwa Makamu mwenyekiti.

Kwa upande wa nafasi ya Ukatibu Juma Nchia kijana kutoka Songea Boys alichaguliwa kuwa Katibu Mtendaji na Hamza Kondo kutoka Luhuniko alichaguliwa Katibu msaidizi.

Nafasi ya Mweka hazina alichaguliwa Safia Hassan kutoka Songea Girls na msaidizi wake alichaguliwa Salima Ali kutoka Chuo cha Ualimu Matororo TTC.

Wakitoa nasaha zao, viongozi waliokuwa wanastaafu waliwashukuru wanajumuia kwa ushirikiano wao. Wote pia walionyesha masikitiko yao kwa walimu walezi ambao wameitelekeza jumuia na kuwaacha wanafunzi kama watoto yatima.

Viongozi hao waliyasema hayo kufuatia kutofika hata mwalimu mmoja katika kikao hicho muhimu.

Kwa mujibu wa taarifa za viongozi wa matawi, walisema hawana taarifa zozote kuhusiana na walimu wao kutokufika.

"Ni mwalimu mmoja tu mlezi wa Songea Boys ndiye aliyetoa taarifa kwamba ana dharura na hivyo ama atafika basi angechelewa kwa sababu zisizozuilika, hakuweza kufika kabisa", walieleza viongozi hao.

Uongozi mpya uliwataka wanajumuia kuacha fikra potofu za kudhani lengo la harakati hizo za wanafunzi ni kupata vyeti na kula pilau pindi watakapohitimu. Waliwataka wanajumuia hao kujua kwamba matatizo ya Waislamu katika nchi hii yataisha tu endapo vijana ambao ndio taifa la leo wataujua vyema Uislamu wao na kuutekeleza ipasavyo.

Juu 
 

YALIYOMO  
 
TAHARIRI 
Iran ina agenda gani?

Mauaji,udhalilishaji Mwembechai: Wanawake Waislamu waandamana Tabora Na Mwandishi Wetu

BUCHA YA NYAMA YA NGURUWE KATIKATI YA WAISLAMU
Na Mwandishi Wetu

'Serikali ieleze hatua iliyochukua kuhusu mauaji Mwembechai'
Na Kassim Juma

Vijana wa Kiislamu wajiimarisha Bukoba
Na Nooh Mustafa, Bukoba

Sheikh Mzonge awataka Waislamu Moshi wasimamishe swala
Na Ashraf Yussuf, Moshi

TAMKO LA PAMOJA LA MISIKITI SABA YA MWANZA-KUPINGA OMBI LA BAKWATA KWA SERIKALI LA KUIFUTIA USAJILI WAKE

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 7

MAKALA: Baadhi ya Watanzania wangali wanaishi ‘Tanganyika’
Na Mwandishi Wetu

HOJA BINAFSI: Maendeleo ya Tanzania ni ndoto
Na Fatma Mussa

‘Musiwasingizie wake zenu maovu’
Na Habiba Swedi, Arusha

Wanafunzi Waislamu Songea wapata viongozi
Na Mwandishi Wetu, Songea

Kikundi cha wanawake wa Kiislamu Bi. Khadija – Dodoma
Na Abu Zuberi, Dodoma

Waahidi kutekeleza majukumu kwa jina la Allah
Na Habiba Swedi, Arusha

Arumeru wahitaji Da’awa
Na habiba Swedi, Arusha

Wanawake wa Kiislamu wazungumzia maendeleo yao

Kauli ya wanawake wa Kiislamu Iringa kuhusu kadhia ya Mwembechai

Uislamu ulivyoingia Zanzibar

Wanawake Singida walaani mauaji Mwembechai Wamchangia Mama Chuki 17,000/-
Na Mwandishi Wetu

Sekondari ya Kiislamu kujengwa Maere Tanga
Na Abu Abdullah, Tanga

Sheikh ahimiza Waislamu Lindi wafuate mafunzo ya Uislamu
Na Mohamed Mussa, Lindi

Sheikh Zuberi awataka Waislamu Dodoma kuimarisha Misikiti
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Mafundisho ya Quran 
Dhikiri maana yake nini? - 2

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matatizo ya tumbo yanayosababishwa na utumiaji wa maziwa

Matangazo 
 

 

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org  

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita