AN-NUUR
Na.168 Jamadul Akhir 1419, Septembe 24 - Oktoba 1, 1998

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita

 

Sheikh Mzonge awataka Waislamu Moshi wasimamishe swala

Na Ashraf Yussuf, Moshi

IMAM wa Msikiti wa Alharamain mjini Moshi, Sheikh Ramadhani Mzonge amesema Waislamu wanapaswa kuipa sala nafasi yake katika Uislamu kinyume na hivi sasa, ili kuimairisha imani zao.

Sheikh Mzonge aliyasema hayo katika khutba ya sala ya Ijumaa ya Agosti 21, mwaka huu katika Msikiti wa Alharamain Moshi Majengo.

Akizungumzia maana ya sala, Sheikh Mzonge alisema, "Sala ni mazungumzo au mawasiliano baina ya mja na Mola wake, hivyo mja hana budi kunyenyekea kikamilifu awapo katika sala bila kufanya mzaha".

Akinukuu baadhi ya aya na hadithi alisema sala ndio nguzo (muhimu) ya pili ya Muislamu baada ya kutoa shahada mbili, na atakayesimamisha sala atakuwa amesimamisha dini na atakae acha atakuwa kaivunja dini.

Sheikh Mzonge aliendelea kusema kitu cha kwanza atakachoulizwa Muislamu siku ya Kiama ni sala na iwapo itatimia basi na mambo yake yatakuwa mazuri na iwapo haitatimia, basi nguzo nyingine zote zitachunguzwa.

Akisikilizwa na mamia ya waumini, Sheikh Mzonge alisema Waislamu wanapaswa wasali sala kwa wakati wake maalum uliowekwa.

Vile vile alisema Mtume (saw) alifaradhishiwa sala katika safari yake tukufu ya mbinguni hivyo alitoa aya kwa kusema "Ole wao wanaosali wasiojali muda wa sala unaotakiwa".

Sheikh Mzonge alimalizia kwa kusema, "Sala humuongoza mja au Muislamu katika kheri na mambo mema, hivyo ni muhimu itiliwe mkazo na kupewa umuhimu mkubwa kwani Mwenyezi Mungu anatutahadharisha juu ya kuacha sala kwa kutufahamisha hatima ya wanaopuuza sala kwa kusema: "Ni kipi kilichokupelekeni motoni? Waseme: Hatukuwa miongoni mwa waliokuwa wakisali".

"Katika aya nyingine Mwenyezi Mungu anasema: "Hakika amekwisha faulu aliyejitakasa akakumbuka jina la Mola wake na akasali", alisema Sheikh Mzonge.

"Hivyo sala imewekwa kuizunguka siku nzima ili Muislamu akumbuke lengo halisi la kuumbwa na Mola wake na uhai wake ili shughuli anazozifanya zisipelekee aghafilike na lengo hili kuu", alimazilia Sheikh Mzonge.

Juu 
 

YALIYOMO  
 
TAHARIRI 
Iran ina agenda gani?

Mauaji,udhalilishaji Mwembechai: Wanawake Waislamu waandamana Tabora Na Mwandishi Wetu

BUCHA YA NYAMA YA NGURUWE KATIKATI YA WAISLAMU
Na Mwandishi Wetu

'Serikali ieleze hatua iliyochukua kuhusu mauaji Mwembechai'
Na Kassim Juma

Vijana wa Kiislamu wajiimarisha Bukoba
Na Nooh Mustafa, Bukoba

Sheikh Mzonge awataka Waislamu Moshi wasimamishe swala
Na Ashraf Yussuf, Moshi

TAMKO LA PAMOJA LA MISIKITI SABA YA MWANZA-KUPINGA OMBI LA BAKWATA KWA SERIKALI LA KUIFUTIA USAJILI WAKE

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 7

MAKALA: Baadhi ya Watanzania wangali wanaishi ‘Tanganyika’
Na Mwandishi Wetu

HOJA BINAFSI: Maendeleo ya Tanzania ni ndoto
Na Fatma Mussa

‘Musiwasingizie wake zenu maovu’
Na Habiba Swedi, Arusha

Wanafunzi Waislamu Songea wapata viongozi
Na Mwandishi Wetu, Songea

Kikundi cha wanawake wa Kiislamu Bi. Khadija – Dodoma
Na Abu Zuberi, Dodoma

Waahidi kutekeleza majukumu kwa jina la Allah
Na Habiba Swedi, Arusha

Arumeru wahitaji Da’awa
Na habiba Swedi, Arusha

Wanawake wa Kiislamu wazungumzia maendeleo yao

Kauli ya wanawake wa Kiislamu Iringa kuhusu kadhia ya Mwembechai

Uislamu ulivyoingia Zanzibar

Wanawake Singida walaani mauaji Mwembechai Wamchangia Mama Chuki 17,000/-
Na Mwandishi Wetu

Sekondari ya Kiislamu kujengwa Maere Tanga
Na Abu Abdullah, Tanga

Sheikh ahimiza Waislamu Lindi wafuate mafunzo ya Uislamu
Na Mohamed Mussa, Lindi

Sheikh Zuberi awataka Waislamu Dodoma kuimarisha Misikiti
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Mafundisho ya Quran 
Dhikiri maana yake nini? - 2

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matatizo ya tumbo yanayosababishwa na utumiaji wa maziwa

Matangazo 
 

 

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org  

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita