|
|
| Home |
Maelezo ya Mjumbe wa Kisarawe katika mkutano wa kina mamaMimi natoka Kisarawe lakini nimepata uchungu baada ya kusikia hapa Dar es Salaam, tunanyanyasika wanawake, mpaka kufika kupigwa na kuvuliwa nguo na kuadhiriwa hadharani.Kinachonitia uchungu sana ndugu zangu wanawake wa Kiislamu, Uhuru (umeletwa) na Babu zangu. Mpaka uhuru unapatikana. Babu zetu walipata taabu kuchangishwa sumni sumni ili uhuru upatikane. Lau kama babu zangu wapo mbele ya haki, siwataji kwa majina kwasababu Yaa Rabbi; Bwana Julius Nyerere Kambarage kusikia haya majina atasikitika sana. Kutunyanyasa sisi Waislamu waliokwenda kuomba uhuru na kumpa yeye madaraka.(Leo tunanyanyaswa sisi) hasa Waislamu wa Kisarawe, Msanga, Visiga, Mwanarumango.Wazazi wetu walipata taabu sana nikifikiria natamani kulia. Tumesoma sisi kwa taabu sana.Yaa Rabbil-Alamina Mwenyezi Mungu leo tumeletewa madhara, mtu huyo kwa babu zetu taabu waliyopata kuleta uhuru. Uhuru wamepata Wakristo sie Waislamu hatuna. Wanawake wamevulia nguo, Ya Rabbi Mungu; kitu kinaniuma sana hasa mimi Mwislamu kutoka Kisarawe. Najisikia uchungu sana. Mimi najua mwanzo mpaka mwisho (Tulivyopata uhuru).Kitu kinaniuma sana leo mmetugeukia; mmetugeukia wewe (Mhe. Mwalimu Nyerere). Sisi hatusemi wengine. Ninachosema mimi Yaa Rabbil Alamina Mwenyezi Mungu atupe salama na amani Uislamu wetu uwe juu. Lakini unyonge wetu (kudhalilishwa kwetu) tutalipwa na Allah Subhana Wataala. Yaani sisi tumeomba uhuru wa kuja kuteseka. Mimi nataka nielewe, kama wapo hapa wanasikia wende wakaniulizie suala hili. Uhuru huu wa wanawake wa Kikristo au wa wanawake wa KiislamuMababu zetu walipata taabu sana kuomba uhuru huu. Wengine walisoma misahafu (Qur'an) kwa ajili ya uhuru huu. Leo uhuru umekuwa taabu (balaa) kwetu sisi wanawake wa Kiislamu ndio hatusemi. Imekuwa sisi tunavuliwa nguo hadharani. Serikali gani ya kuwavua nguo wanawake wa Kiislamu. Wavuliwa nguo na wanaume wasio kuwa waume zao. Jamani Yaa Rabbil Alamina. Jamani Yaa Rabbil Alamina muogopeni Subhana wa Taala.Au kumbukeni mlipata wapi uhuru huu. Kumbukeni nani alikusaidieni (alileta) uhuru huu!(Walileta) Waislamu hasa wanawake wa Kiislamu mama zetu walikuwa wanakwenda; Bwana Julius Kambarage unarudi (UNO) wamekuimbia "Sasa hata kabwela UNO". Sasa UNO imekuwa taabu kwetu sisi. Kumbe "hata kabwela UNO" itakuwa hata kabwela UNO yenu nyinyi Wakristo sio sie Waislamu.Assalaam alaikum warahmatullah Waabarakatuh. Nasikia uchungu sana.. |
Uvamizi wa Polisi Mwembe Chai: Mwanafunzi aliyepigwa risasi apooza Muhimbili Maoni yetu: Vipi watu wafurahie mateso ya wengine? Wanawake wakutana na kudai:
Gewe, Makamba wajiuzulu
Waraka wa Baraza Kuu kwa Mh. Rais Mmiliki wa Biblia na mbinu za kuhubiri MAKALA:
MAKALA MAALUM
Mdahalo juu ya kudhulumiwa Waislamu: Tuache hisia na kejeli, tutoe hoja Hali ilivyokuwa kwenye shule za Misheni Makala: Baada ya miaka 34 Zanzibar yakosa Majaji - na S. Mzee Bakwata ithamini juhudi za wengine Masheih Arusha wamuunga mkono
K.K.
Makamba aliongezea AN-NUUR 'Mashitaka' MSAUD wafikisha suala la Chuki
AMNESTY
|
| An-nuur Home | Links | Islam Tanzania | Matoleo yaliyopita |