AN-NUUR
Na.153 Safar 1419, Juni 12-18, 1998
 
Home 

Links 

Islam Tanzania 

Matoleo ya nyuma 
 
 

Masheih Arusha wamuunga mkono K.K.Na Mwandishi Wetu Arusha

MASHEIKH kadhaa mkoani Arusha na Kilimanjaro, wameungana na Mbunge wa Kigamboni Mhe. Kitwana Kondo kuiambia Serikali iwape dhamana Waislamu waliopo ndani na kuwafutia mashitaka wale ambao wameshitakiwa kinyume cha katiba na sheria za nchi.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Sheikh Mohamed Hemed Anzuwani alisema anaungana na Mhe. Kitwana Kondo kuisihi Serikali ama iwaachilie kabisa watuhumiwa wa Mwembechai au iwape dhamana. 

Alisema ni jukumu la kila Muislamu kuamrisha mema na kukataza mabaya; na hivyo Mhe. Kondo katekeleza wajibu wake kulisemea jambo baya analoona linafanywa na Serikali.

Sheikh Anzuwani alisema kama \wakristo wenyewe wanasema hawakukashifiwa; vipi tena Muislamu leo ashitakiwe kwa kosa la kashfa.Naye Sheikh Hashim Juma alitahadharisha kwamba isingekuwa jambo la busara Waislamu kuwekwa katika mazingira ya kujiandaa kuwasomea khitma walioko mikononi mwa Serikali.Sheikh Hashim alionyesha masikitiko yake kutokana na kauli za baadhi ya mabaraza ya dini kwamba hayajaweza kuwasaidia Waislamu kwasababu hayajaombwa. Alitoa wito mafunzo na ujumbe unaopatikana katika Surat Abzab Aya ya 21 mpaka 36 uzingatiwe kwa makini.

Naye Sheikh Farijala Hussein akilizungumzia suala hili alisema kwamba imekuwa ni kero kubwa kwa wananchi kutokana na Serikali kufumbia macho na kujifanya bubu kuhusu suala zima la kuvunjwa kwa haki za binadamu na hasa Waislamu.Sheikh Farijala alisema hivi sasa Waislamu wanakamatwa ovyo, kuwekwa ndani, kupigwa na wengine kuuliwa bila ya haki wala sheria. Katika hali hiyo anasema haungani tu na Mhe. Kitwana Kondo lakini kwa kila mpenda haki na amani.

Alisema hakuna amani inayopatikana kwa mabavu wala vitisho, bali kwa kuwapa watu uhuru na haki zao.Sheikh Yusuf Ismail Kimaro ambaye ni Imam wa Msikiti wa Bondeni Wilayani Hai; akiungana na Masheikh wenzake alisema aliyozungumza Mhe. Kitwana Kondo ndiyo yanayotegemewa kwa mtu yeyote mkweli na muadilifu. Kwa ajili hiyo amewataka Waislamu wote kumuunga mkono.Hivi karibuni Mbunge wa Kigamboni Mhe. Kitwana Kondo aliongea na waandishi wa habari ambapo aliishauri Serikali iwape dhamana watuhumiwa wa kesi ya Mwembechai walioko ndani, pamoja na kuiomba iondoe shitaka la kashfa kwa aliyesema Yesu si Mungu. 

Aidha, Mhe. Kondo katika mkutano huo aliilaumu Serikali kwa kutojali masuala ya Waislamu kiasi cha kuwaruhusu Polisi kuvunja Msikiti na kuingia ndani na viatu. 

 
 

YALIYOMO

TAHARIRI  

Uvamizi wa Polisi Mwembe Chai:  Mwanafunzi aliyepigwa risasi apooza Muhimbili   

Maoni yetu: Vipi watu wafurahie mateso ya wengine?  

Wanawake wakutana na kudai:  Gewe, Makamba wajiuzulu    
  
Maelezo ya Mjumbe wa Kisarawe katika mkutano wa kina mama   

Waraka wa Baraza Kuu kwa Mh. Rais   

BARUA ZA WASOMAJI  

Mmiliki wa Biblia na mbinu za kuhubiri   

MAONI YA WASHAIRI  

MAKALA:   
KAMATI YA KINA MAMA WA KIISLAMU - TAARIFA YA MATUKIO JUU YA UNYANYASAJI WA POLISI DHIDI YA WANAWAME WA KIISLAMU   

MAKALA MAALUM   
Waziri Dossa Azizi: Shujaa aliyesahaulika - Na. Mohammed Said  

Mdahalo juu ya kudhulumiwa Waislamu: Tuache hisia na kejeli, tutoe hoja  

TAMKO LA WANAWAKE WA KIISLAMU DHIDI YA MAUAJI YA WAISLAMU MWEMBECHAI NA KUDHALILISHWA WANAWAKE WAISLAMU MAHABUSU   

Hali ilivyokuwa kwenye shule za Misheni   

Makala: Baada ya miaka 34 Zanzibar yakosa Majaji - na S. Mzee   

Bakwata ithamini juhudi za wengine  

Masheih Arusha wamuunga mkono K.K.   
Na Mwandishi Wetu Arusha  

Makamba aliongezea  AN-NUUR 'Mashitaka'  

MSAUD wafikisha suala la Chuki AMNESTY  
  
Wazee Handeni wakwamisha mhadhara 

 
 Maoni yoyote kuhusu ukarasa huu yapelekwe kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
An-nuur Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita