| Home
Links
Islam Tanzania
Matoleo ya nyuma
|
Maoni yetu
Vipi watu wafurahie mateso ya wengine?
Awali ya yote tungependa kuuliza ni kitu gani hasa Serikali inanufaika
iwe ni kisiasa au usalama wa nchi kwa Chuki Athumani kuteseka hospitalini
akiwa kapooza miguu huku akiwa bado kafungwa pingu.
Manufaa gani hasa serikali inapata kwa Chuki kuota vidonda kwa vile kafungwa
pingu na hana mtu wa kumsaidia kumgeuza na kumbadili nguo mara kwa mara
kama hali yake inavyohitaji!
-
Manufaa gani hasa Serikali inapata kwa Chuki kuendelea kukosa matibabu
stahiki, zaidi ya kujenga hisia kwamba kuna watu wanafurahi Mwislamu akiteseka.
-
Usalama gani wa nchi hii mtoto huyu wa umri wa miaka 17, anahatarisha hata
afungwe pingu pamoja na kupooza kwake kutokana na risasi alizopigwa na
polisi wa Serikali!
-
Usalama gani wa Serikali hii anauhatarisha! Kwamba mtoto huyo wa miaka
17 kaoneka hatari sana anatengeneza pengine mabomu ya kuua au kupindua
serikali!
-
Hata kama ni jambazi lililoua, si anatibiwa kwanza akipona ndio umshitaki!
Hata kama mwisho wake itakuwa kuhukumiwa kunyongwa! Huu ndio utaratibu
duniani kote.
-
Tunaamini uhai na umauti upo katika milki ya Mwenyezi Mungu. Kila mtu ana
siku yake ya kuzaliwa na siku ya kufa. Lakini mwanadamu hubeba lawama anapokiuka
hulka na busara katika maamuzi na matendo yake.
-
Huyu mtoto kwanza kapigwa risasi ya kifuani (kwa kosa lipi?). Pili anakosa
matibabu yanayostahiki na kafungwa pingu. Tatu anakosa huduma na uangalizi
wa karibu katika hali yake hii ya kupooza mpaka anaota vidonda. Inachokikusudia
hasa Serikali kwa mtoto huyu nini? Mwenyezi Mungu akichukua roho yake,
kwanini Waislamu wasidhanie kwamba hilo ndilo mlilokuwa mkitaka litokee!
-
Katika suala la "Parole" Mheshimiwa Rais ametufariji kwamba yupo pale kwa
maslahi ya nchi hii. Na kwamba uadilifu na haki itazingatiwa bila kujali
dini ya mtu.Kwa moyo huo haya yanayomkuta mtoto Chuki hatudhani ni agizo
la Mhe. Rais Benjamin William Mkapa au hata kama anajua.Kama Mhe. Rais
Mkapa ameliona hili la "Parole" likamgusa hatuoni ni vipi, aagize askari
wamtie pingu mtoto aliyepooza akose kutibiwa; akose; huduma na kuota madonda
kwa kulalia mikojo na hata kupewa chakula iwe taabu!Yawezekana wapo watu
ndani ya Serikali ambao pengine kwa chuki zao wanayafurahia haya. Lakini
tunaamini pia kwamba wapo watu wanaiona hatari iliyopo mbele yetu! Mwenyezi
Mungu atunusuru. Na kwa kuhofia hilo na jukumu letu la kuinusuru nchi yetu
inabidi tuyaseme haya. Watu wasiangalie "furaha" ya nafsi zao kuona wenzao
wakiteseka wakatuangamiza sote.Yapo mambo mengi yanayoweza kuhatarisha
amani na usalama wa nchi, lakini hili linaloleta picha kwamba wapo watu
wanafurahi kuona Muislamu akiteseka ni la hatari zaidi.
-
Pingu hufungwa mtu na nguvu zake na anayeweza akaleta vurugu akatoroka.
Huyu mtoto mgonjwa, kapooza mwenyewe hajiwezi maskini kiasi anatoka vidonda
kwa kushindwa kujigeuza, kama si chuki na ukatili tu wa baadhi ya viongozi,
pingu anafungwa za nini! Na je inadhaniwa hili ndugu zake Waislamu hawalioni!
Na je inadhaniwa watalikubali tu na kutokujiuliza kwanini?!
-
Wakristo na Waislamu wanaishi kwa pamoja mitaani kwa udugu wakisaidiana
kwa furaha na shida. Wanasaidiana na kushirikiana kufukuza wezi na vibaka
ambao wamekuwa kero mitaani. Hawa tupo nao bega kwa bega tunakula nao magengeni
na kwa Mama Ntilie. Nao wanateswa na hali hii. Wana wasiwasi kesho hali
itakuwaje. Ndio maana tunashindwa kuelewa hao wanaohisi kunufaika kwa namna
yoyote na kuteswa kwa Chuki Abdallah wana agenda gani! Wapi wamekusudia
kuizamisha nchi hii.
-
Chuki Athumani (17) anateseka; yupo mikononi mwa Serikali toka Februari
13, 1998. Ndugu zake Waislamu na Watanzania wenzake wenye upendo, huruma
na uungwana ambao wangeweza kumsaidia kwa gharama yoyote na mahali popote
ndani na nje ya nchi wamezuiwa japo kumjulia hali.

|
YALIYOMO
TAHARIRI
Uvamizi wa Polisi Mwembe Chai:
Mwanafunzi aliyepigwa risasi apooza Muhimbili
Maoni yetu: Vipi watu wafurahie
mateso ya wengine?
Wanawake wakutana na kudai:
Gewe, Makamba wajiuzulu
Maelezo ya Mjumbe wa Kisarawe
katika mkutano wa kina mama
Waraka wa Baraza Kuu kwa Mh. Rais
BARUA ZA WASOMAJI
Mmiliki wa Biblia na mbinu za kuhubiri
MAONI YA WASHAIRI
MAKALA:
KAMATI YA KINA MAMA WA KIISLAMU
- TAARIFA YA MATUKIO JUU YA UNYANYASAJI WA POLISI DHIDI YA WANAWAME WA
KIISLAMU
MAKALA MAALUM
Waziri Dossa Azizi: Shujaa aliyesahaulika
- Na. Mohammed Said
Mdahalo juu ya kudhulumiwa Waislamu:
Tuache hisia na kejeli, tutoe hoja
TAMKO LA WANAWAKE WA KIISLAMU DHIDI
YA MAUAJI YA WAISLAMU MWEMBECHAI NA KUDHALILISHWA WANAWAKE WAISLAMU
MAHABUSU
Hali ilivyokuwa kwenye shule za Misheni
Makala: Baada ya miaka 34 Zanzibar
yakosa Majaji - na S. Mzee
Bakwata ithamini juhudi za wengine
Masheih Arusha wamuunga mkono
K.K.
Na Mwandishi Wetu Arusha
Makamba aliongezea
AN-NUUR 'Mashitaka'
MSAUD wafikisha suala la Chuki
AMNESTY
Wazee Handeni wakwamisha
mhadhara |