AN-NUUR
Na.153 Safar 1419, Juni 12-18, 1998
 
Home 

Links 

Islam Tanzania 

Matoleo ya nyuma 
 
 

Makamba aliongezea  AN-NUUR 'Mashitaka'

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mheshimiwa Yusuf Rajab Makamba ametoa nyongeza ya madai yake dhidi ya gazeti la AN-NUUR. Katika nyongeza hiyo Mhe. Mkuu wa Mkoa Bw. Makamba amedai kwamba kitendo cha kumuita "Al-Ustaadh Sheikh Makamba" ni kumkejeli na kumdhalilisha. 

Katika barua yake No. MD/P.10/8/47 ya Juni 6, 1998 kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari, Mheshimiwa Makamba amesema; "Nalalamika kwamba mwandishi wa makala ameniita Al-Ustaadh na Sheikh kwa dhamira ya kunikejeli au kunidhalilisha". 

Akaongeza kusema "mimi (yeye Mhe. Makamba) sina makamu ya kuitgwa Ustaadh au Sheikh; mimi ni muuamini wa dini ya Kiislamu na mwanafunzi", ilisema sehemu ya barua yake.Kwa ajili hiyo Mhe. Yusuf Rajab Makamba anamtaka Mhariri wa AN-NUUR athibitishe kuwa kwa kumuita Al-Ustaadh na Sheikh hakukusudia kumnyanyasa. 
 
 

Sheikh Mohammed Ummy afariki

Na Muhibu Said

MHADHIRI wa Jumuiya ya Wahubiri wa Kiislamu nchini (JUWAKITA), Sheikh Mohamed Athumani A. Ummy, amefariki dunia Jumamosi ya Mei 30, 1998, nyumbani kwa baba yake mdogo, Tandale Uzuri, jijini Dar es Salaam,baada ya kuugua muda mfupi. 

Kwa mujibu wa msemaji mkuu wa familia yake, marehemu kabla ya kifo chake alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya figo na kibofu mbapo aliwahi kulazwa katika Hospitali ya Serikali yaMwananyamala kwa zaidi ya siku kumi na moja bila mafanikio.Aidha kwa mujibu wa msemaji huyo, baadae marehemu alihamishiwa katika hospitali ya T.M.J.iliyopo Kikocheni ambako hadi anafariki ndiko alikokuwa akitibiwa.Marehemu Sheikh Mohamed Ummy atakumbukwa sana na ndugu, jamaa, marafiki, majirani, Waislamu na Wasiokuwa Waislamu hususan wakazi wa mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es Salaam na kwingineko kwa mchango wake mkubwa wa kupigania ili kuuhuisha Uislamu bila woga.

Marehemu Sheikh Mohamed Ummy ni miongoni mwa Waislamu waliounda Jumuiya ya kwanza za kuligania Uislamu ijulikanayo kwa kifupi kwa jina la "UWAMDI" mwanzoni mwa miaka ya 1980. Alianza rasmi harakati za kulingania Uislamu mnamo mwaka wa 1979 kwa kufanya mijadala ya Qur'ani Tukufu na tofauti zilizo baina ya Waislamu na Ahmadiyyah na madhehebu mengine ya Kikristo katika shuleya msingi ya Lumumba, Mnazi Mmoja na baadae Sokoni Kriakoo na mikoani alipoitwa kwenda kujibu hoja hizo.

Mwaka 1982 alianza kufanya mijadala ya ulinganishi wa vitabu vinne (Torati, Zaburi, Injili na Qur'ani Tukufu) katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Saaam na kufundisha elimu hiyo (ya Ulinganishi) katika shule ya Lumumba.

Katika kuimarisha kazi hiyo, mnamo mwaka wa 1983, marehemu alishirikiana sambamba na Waislamu wengine waliounda Umoja wa Wahubiri wa Kiislamu wa Mlingano wa Didini (UWAMDI), akiwemo Almarhuman Sheikh Muhdin, Sheikh Khalifa Khamisi Sheikh Sadiki Watuta na wengineo.Katika harakati hizo, mwaka 1984 waliungana na Wahadhiri wengine, akiwemo Al-m 

arhum Sheikh Ngariba Musa Fundi, ustaadhi Kawemba Mohamed, Sheikh Abubakar Mwilima na Sheikh Othmani Matata ili kuimarisha UWAMDI. 
 
 
 

Wazee Handeni wakwamisha mhadhara

Na Abu Said

WAZEE wa Kijiji cha Kwediboma katika Wilaya ya Handeni walikwamisha muhadhara ambao ulikuwa uendeshwe na ustaadh Hamim Ali Boza kuanzia tarehe 6 Juni mpaka tarehe 14 Juni. 

Kijiji hicho kilioko mwendo wa masaa manne na nusu kwa gari ya abiria, kutoka Handeni mjini, kilikuwa kiwe cha mwanzo kufaidika na kibali cha ruhusa cha mkuu wa Polisi wa Wilaya, chenye kumbukumbu No. HAN/A.25/Vol.V/247 cha tarehe 21 Mei. 

Tangu ujumbe ulipowasili saa tatu na nusu usiku wa tarehe 6, kulionekana ingia toka isiyo ya kawaida kwenye ofisi ya Katibu Tarafa wa Bakwata. Pirika hizo zilizowahusisha wazee na vijana hatimaye zilikoma baada ya sala ya Alasiri ya siku ya Jumapili.

Akitoa ufafanuzi wa kuzuilika kwa muhadhara huo, katibu wa Bakwata Bwana Juma Bakari, alisema yeye kama kiongozi wa Bakwata hakuwa na kikwazo chochote kwa jambo la kheri kama hilo na hasa kwa vile alikwishapata taarifa kabla.Hata hivyo, aliendelea kusema kuwa asingeweza kwenda kinyume na uamuzi wa wazee walioweka pingamizi, ambao ni wajumbe wa kamati ya msikiti,ujumbe wa muhadhara ulipofikia.

Ustaadh Hamim aliruhusiwa kutoa mawaidha mafupi ndaniya msikiti, katika mawaidha hayo aliishukuru nyumba ya wageni ya Bwana Zuberi kwa kutoruhusu matendo yoyote machafu kutendeka humo pia mkahawa mmoja ambao pia umezuia ulevi kunywewe humo. Pia aliwahimiza Waislamu kujenga shule na kituo cha afya.Sehemu nyingine ambazo zilikuwa zifaidike na mihadhara hiyo ni pamoja na Kilindi, Mgera na Kisangasa. 
 
 

MSAUD wafikisha suala la Chuki AMNESTY

Na Mwandishi Wetu
WANAFUNZI Waislamu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (MSAUD) wameiomba Taasisi za Kutetea Wafungwa (Amnesty International) kumsihi Mhe. Rais Benjamin William Mkapa kumhurumia mwanafunzi Chuki Athumani ambaye alipigwa risasi na Polisi Februari 13. 

Mwanafunzi huyo yupo hospitalini Muhimbili na anakosa matibabu kwa vile anahesabika kama mhalifu aliye mahabusu. 

Katika barua yao yenye kumb. Na. MSA/AM/005 wameeleza kwamba tayari walishamuandikia Mhe.Rais kuhusu suala hilo kwa hiyo sasa wanaomba `Amnesty International' iwasaidie juhudi hizo. 

Tayari zaidi ya robo tatu ya watu waliokuwa rumande wameshaachiwa na kufutiwa mashitaka.Kwa mara ya mwisho waliachiwa watu 68. Hiyo ilikuwa jana Alhamis, Juni 11, 1998. 
 

 
 

YALIYOMO

TAHARIRI  

Uvamizi wa Polisi Mwembe Chai:  Mwanafunzi aliyepigwa risasi apooza Muhimbili   

Maoni yetu: Vipi watu wafurahie mateso ya wengine?  

Wanawake wakutana na kudai:  Gewe, Makamba wajiuzulu    
  
Maelezo ya Mjumbe wa Kisarawe katika mkutano wa kina mama   

Waraka wa Baraza Kuu kwa Mh. Rais   

BARUA ZA WASOMAJI  

Mmiliki wa Biblia na mbinu za kuhubiri   

MAONI YA WASHAIRI  

MAKALA:   
KAMATI YA KINA MAMA WA KIISLAMU - TAARIFA YA MATUKIO JUU YA UNYANYASAJI WA POLISI DHIDI YA WANAWAME WA KIISLAMU   

MAKALA MAALUM   
Waziri Dossa Azizi: Shujaa aliyesahaulika - Na. Mohammed Said  

Mdahalo juu ya kudhulumiwa Waislamu: Tuache hisia na kejeli, tutoe hoja  

TAMKO LA WANAWAKE WA KIISLAMU DHIDI YA MAUAJI YA WAISLAMU MWEMBECHAI NA KUDHALILISHWA WANAWAKE WAISLAMU MAHABUSU   

Hali ilivyokuwa kwenye shule za Misheni   

Makala: Baada ya miaka 34 Zanzibar yakosa Majaji - na S. Mzee   

Bakwata ithamini juhudi za wengine  

Masheih Arusha wamuunga mkono K.K.   
Na Mwandishi Wetu Arusha  

Makamba aliongezea  AN-NUUR 'Mashitaka'  

MSAUD wafikisha suala la Chuki AMNESTY  
  
Wazee Handeni wakwamisha mhadhara 

 
 Maoni yoyote kuhusu ukarasa huu yapelekwe kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
An-nuur Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita