| Home
Links
Islam Tanzania
Matoleo ya nyuma
|
Tahariri
Sasa tutafika
Kumbe Rais anasikia
-
KWA kipindi kirefu umekuwepo mdahalo " wa viziwi" kati ya Waislamu na Serikali.
Waislamu wanatoa malalamiko na madai yao kwa serikali kwamba hawatendewi
haki, lakini serikali ama inakaa kimya au inaibuka na shutuma dhidi ya
Waislamu na kuepuka kabisa kusema lolote juu ya madai yao. Hata pale ambapo
serikali imelazimika kutoa ufafanuzi, basi ufafanuzi wenyewe umekuwa ama
kuwadhania Waislamu wajinga, wasioelewa kitu au wasioona na kufikiria yanayotokea
nchini hapa.Waislamu wameuliwa pale Mwembechai, wengine kujeruhiwa kwa
risasi na wanawake kudhalilishwa. Waislamu wadai iundwe Tume huru kuchunguza
kadhia hii; Mh. Ali Ameir anasema kwamba, "serikali haifanyi kazi kwa shinikizo".Kumbe
shinikizo kwa Waislamu tu? Lile la Paroko je? Lilikuwa agizo!Waislamu wanasema
kwa kusema Yesu si Mungu, hawatukani wala hawamkashifu mtu, kwani ndivyo
kitabu chao kinavyosema, serikali inasema "mnakashifu". Inawakamata Waislamu,
inawaweka ndani na kuwanyima dhamana. Inadai inawanyima dhamana kwa usalama
wao. Kwamba wamekashifu sana na watu huko nje wamekasirika, watawadhuru.Lakini
wenye dini yao wamejitokeza wamesema waziwazi kwamba Mkristo kusema Yesu
ni Mungu si kashfa na Muislamu kusema Yesu si Mungu si kashfa vilevile.Hilo
amelitamka mpaka Muadhama Kadinali Pengo. Tafsiri yake wanasema kwamba
kama serikali inataka kuwapiga risasi Waislamu, iwapige tu, kama inataka
kuwanyima dhamana iwanyime tu na kama inataka kuwanyima matibabu huko jela
wafe mmoja mmoja iwanyime tu. Lakini isiwasingizie Wakristo. Wao hawana
mashitaka dhidi ya Waislamu.Kasimama Mbunge, tena Mbunge mzito asiyehitaji
sifa wala umaarufu. Aliyoyafanya toka kupigania uhuru hadi leo yashatosha
kumpa huo umaarufu. Huyo ameishauri na kuitahadharisha serikali yake kwamba
kuna dhulma hapa. Watu wanasingiziwa kosa la kashfa, watu wamenyimwa dhamana,
watu wananyimwa matibabu, watu wanatishwa kwa sababu ya kusaidia shughuli
za taasisi halali.Hoja hazijibiwi. Anasimama Naibu Waziri anazungumza yake.
Waziri naye anaibuka na yake. Kana kwamba hawakuzielewa hoja na madai yaliyotolewa.
-
Mpaka leo wananchi hawaelewi kauli na msimamo wa serikali ni upi. Ni ule
wa Sigela Nswima, Waziri Ali Ameir au ule wa msemaji mkuu wa Baraza moja
mashuhuri nchini!Ndani ya mkanganyiko huo likaja hili la "Parole". Likaundwa
na kutangazwa katika sura ambayo inapeleka salamu kwa Waislamu "Mtakoma
tunafanya hivi mtafanya nini". Baraza Kuu likahoji, vyombo vingi vya habari
vikaona upogo na dosari ile na kuisemea mpaka kwenye tahariri zao. Kwamba
jamani hii sasa mmezidi!Mheshimiwa Ali Ameir kaibuka tena kuwajibu (anaowadhania
hawaoni wala hawaelewi) Waislamu, kwamba Baraza lile kuwa la Wakristo watupu
pamoja na Maakofu wao, sio geni. Wao serikali watu safi, hawaangalii dini!
Lakini kwa bahati njema kaja Rais, katuondolewa kukanganyikiwa. Kwanza
sasa tumejua msimamo wa serikali utaelezwa na nani. Na zaidi imetuonyesha
kwamba kilio cha Waislamu kinasikilizwa.Katika kauli yake Mh. Ameir alisema
"sisi " hatuangalii dini "sisi" ile ilimaanisha ama CCM au Serikali. Lakini
tunashukuru kwa kauli na hatua alizochukua Rais "sisi" ile sio ya serikali:
Labda sasa wakati Waislamu wanampongeza Mheshimiwa Rais Benjamin William
Mkapa, Bw. Ali Ameir atueleze "sisi" ile yeye na nani?Pamoja na kumpongeza
Mh. Rais, tungependa pia kuyataja magazeti ya Rai na Mtanzania
ambayo kwa misingi tu ya uzalendo wamesimama na kupinga dhulma ile
kwa kuizungumza kwa uzito wake katika tahariri zao.Kwa mwendo huu, tunaamini
kwamba tutafika. Kwamba kumbe Rais wa nchi anasikia kilio cha wananchi,
na barua anazisoma kama ile ya gazetini. Hii inatupa imani kwamba hata
zile za AN-NUUR ujumbe wake unafika kwa Mh. Rais. Lakini Mheshimiwa
Rais, Parole haina maana kama tunakuwa na wahalifu na wahalifu wakabaki
nje na wasio wahalifu wakabaki ndani. Hawa hawahitaji Parole.
-
Kuna watu wameua pale Mwembechai wapo nje wanakunywa bia zao. Sana sana
pengine waweza kutolewa Dar es Salaam wakapelekwa Moshi, Musoma au pengine
popote kufichwa. Wapo na wale waliompiga Chuki Athumani risasi na wakamkosesha
matibabu stahiki kwa kumfunga pingu. Wapo na wale waliowarusha wanawake
kichura wakiwa uchi.Anayehitaji Parole nani. Huyu muuaji au yule
aliyekoswakoswa na risasi akawekwa jela! anayehitaji Parole nani,
huyu muuaji au Chuki aliyepigwa risasi akipita njia! Anayehitaji Parole
nani, huyu muuaji au waliojeruhiwa kwa risasi na marungu na wakanyimwa
dhamana na dawa huko Segerea mpaka wengine wakafa! Parole haipo
hapa.Nani anayehitaji Parole ,aliyemuweka mtu ndani na kumnyima
dawa kwa vile kasaidia taasisi halali iliyosajiliwa na serikali au huyu
aliyemfunga mtu bila ya kosa!Anayehitaji Parole nani, huyu aliyewaweka
watu ndani akawanyima dhamana na matibabu kwa kusema kwao Yesu si Mungu
au huyu anayewekwa ndani kinyume cha Katiba na sheria.Ili Parole ifanye
kazi ni lazima kwanza mhalifu awepo. Pili ahukumiwe, afungwe. Na tatu ajirekebishe.
Huyu mhalifu anayeua atajirekebishaje wakati hafikishwi mahakamani. Aliyedhulumiwa
ajirekebishe awe nani? Ajirekebishe wakati toka mwanzo sio mhalifu! Zaidi
atajenga chuki na hasira dhidi ya wale waliomdhulumu.
-
Parole imevunjwa, lakini tuangalie wakati wa kuundwa kwake upya.
Kuna watu wa NGOs na Mabaraza ya Kidini hao hawasiti kusimama na kutoa
msimamo wa serikali, wakati wao si serikali. Hao hawawezi kuwa na sifa
za ujumbe wa Parole. Tunamshukuru Mh. Rais kwa hatua hii, lakini
Parole imekuja jana. Yapo yaliyotangulia.
Tusingependa tuyarejee malalamiko yote ya Waislamu wa nchi hii. Lakini
historia imerikodi kilio chao kupunjwa elimu.Waliopata bahati kusoma kazi
hawapati, wanaopata kazi, cheo hapati na anayepata cheo fitna humwandama.
Kosa lake aanze kuswali au avae kofia atajizolea kejeli za `siasa kali',
Mujahidina', n.k.Lakini yule anayetundika msalaba shingoni, picha au sanamu
ya Yesu ofisini na Biblia juu ya meza ya ofisi, huyu husifiwa. Kaokoka,
mtu wa Mungu!Haya ya kupakaziana ndiyo yaliyotuletea hili Parole lisilo
na mwelekeo. Ndio maana wengi walihoji, vipi Jumanne Mangara asifae?
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Uvamizi wa Polisi Mwembe Chai:
Mwanafunzi aliyepigwa risasi apooza Muhimbili
Maoni yetu: Vipi watu wafurahie
mateso ya wengine?
Wanawake wakutana na kudai:
Gewe, Makamba wajiuzulu
Maelezo ya Mjumbe wa Kisarawe
katika mkutano wa kina mama
Waraka wa Baraza Kuu kwa Mh. Rais
BARUA ZA WASOMAJI
Mmiliki wa Biblia na mbinu za kuhubiri
MAONI YA WASHAIRI
MAKALA:
KAMATI YA KINA MAMA WA KIISLAMU
- TAARIFA YA MATUKIO JUU YA UNYANYASAJI WA POLISI DHIDI YA WANAWAME WA
KIISLAMU
MAKALA MAALUM
Waziri Dossa Azizi: Shujaa aliyesahaulika
- Na. Mohammed Said
Mdahalo juu ya kudhulumiwa Waislamu:
Tuache hisia na kejeli, tutoe hoja
TAMKO LA WANAWAKE WA KIISLAMU DHIDI
YA MAUAJI YA WAISLAMU MWEMBECHAI NA KUDHALILISHWA WANAWAKE WAISLAMU
MAHABUSU
Hali ilivyokuwa kwenye shule za Misheni
Makala: Baada ya miaka 34 Zanzibar
yakosa Majaji - na S. Mzee
Bakwata ithamini juhudi za wengine
Masheih Arusha wamuunga mkono
K.K.
Na Mwandishi Wetu Arusha
Makamba aliongezea
AN-NUUR 'Mashitaka'
MSAUD wafikisha suala la Chuki
AMNESTY
Wazee Handeni wakwamisha
mhadhara |