|
Na. 065 Jumatano Septemba 13 - 19, 2000 |
|
|
|
|
|
CCM mtashinda vipi? Ndugu Mhariri KATIKA kipindi hiki cha kampeni vyama mbalimbali vya kisisaa vyenye usajili wa kudumu vinazunguka sehemu mbalimbali nchini kuomba ridhaa ya wananchi ili vichaguliwe kuongoza nchi. Hiki ni kipindi cha kuwashawishi wananchi. Ni kipindi cha kuwabembeleza wapiga kura. Ninalonishangaza ni kauli ya Makamu wa Rais, Dr. Omar Ally Juma iliyoripotiwa wiki iliyopita. Ilielezwa kuwa Makamu amewaambia wananchi katika mkutano wake wa hadhara kuwa hata wasipoichagua CCM itashinda tu! Sasa watashinda vipi bila kura zetu? Jeuri hii ya kuwakejeli wananchi katika kipindi hiki msingi wake nini? Je ni nani anayetaka kushuhudia sera ya jino kwa jini ambayo imeshatangazwa iwapo uchaguzi utavurugwa ikitekelezwa. Wananchi tungependa kuona vyombo husika vikikemea kauli hizi zinazoashiria nia ya kuvuruga uchaguzi. Joel Fungo,
Ndugu Mhariri NCHI hii inadaiwa kuwa na amani na utulivu ambao wanasiasa wanaapa kuulinda. Lipo jambo moja linalonishangaza huku mitaaani. Wananchi wanaishi kwa hofu. Watu wanalazimika kutundika bender na picha za mgombea ambaye hawamtaki ili tu waweze kuendelea kufanya biashara katika eneo fulani. Watu wanalazimika kuishi kwa unafiki ili wasibughudhiwe. Wanaotoa bughudha hizi kwa wale wasio na itikadi sawa nao hawaoni aibu kudai hadharani kuwa tuna amani na utulivu. Mimi napenda kutoa mwito kwa wananchi kuwa umefika wakati wa kujipatia uhuru. Itumie kura yako kuchagua chama kitakachosimamia haki sawa kwa wote. Kataeni kuishi kwa hofu katika nchi yenu. Alfonce Massawe,
Ndugu Mhariri GAZETI moja litolewalo kila siku kwa lugha ya Kiswahili Na. 00093 toleo la Jumanne ya Septemba 12, limemkariri Balozi Diria alidai kuwa CUF haitaki uchaguzi ufanyike Zanzibar. Diria ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar amedai kuwa CUF imekata tamaa baada ya kutolewa takwimu za waliojiandikisha kupiga kura na Tume ya Uchaguzi Zanzibar. Aliendelea kudai kuwa CUF wanaona watashindwa kwa vile Wapemba waliojiandikisha ni 150,000 tu wakati Waunguja ni watu 300,000. Mtazamo huu wa Diria ni wa hatari sana hasa kwa wadhifa alio nao katika CCM. Kwanza anaonesha kuwa kura zote za Unguja ni za CCM. Hii ni dhana potofu kwani inaligawa Taifa la Zanzibar. Ni kipimo gani anachotumia kujua kuwa Waunguja wote ni CCM? Lazima Tume ya Uchaguzi iwakemee watu hawa wanaotoa vigezo vya ushindi ambavyo vinapotosha. Ussi Makame,
Ndugu Mhariri KATIKA ziara yake hapa nchini hivi karibuni Rais Bill Clinton wa Marekani aliisifia Tanzania kuwa ni nchi yenye kuongoza kwa amani na utulivu barani Afrika. Nikikubaliana na Rais huyo wa Marekani, napenda kuhoji je vipi aje na mbwa wake na wainuse gari ya Rais wetu Mkapa, kama maneno yake siyo ya kejeli kwa Watanzania. Clinton anajua wazi kuwa kwa umaskini unaoikabili nchi hii ni rahisi kwa hata Rais wetu au wapambe wake kama si raia wake kufanya ugaidi ili wapate malipo ya fedha au mengineyo. Kwa ajili hiyo ndiyo maana hakumwamini hata Rais wetu na watu wa usalama wakaamua kuipekua gari ya Rais wetu kwa kuinusisha mbwa. Kweli umaskini ni balaa ni hasa inapokuwa umaskini wa kujitakia kama wa nchi hii, na kwamba kwenye umasikini hapana amani isipokuwa uoga tu. Peter Maganga,
Ndugu Mhariri CHONDE! Chonde! Ndugu zangu Wazanzibari jinsi hali inavyoelekea ipo dalili za kufuta katika uso wa dunia Taifa la kisiwa maarufu duniani cha Zanzibar. Inavyoelekea hali hiyo ya kutisha na kuhuzunisha mno! Itatokana na nyinyi wenyewe kwa kuwaendekeza na kuwaunga mkono hawa viongozi wenu wa sasa ambao wanapata maelekezo yao toka Bara. Leo tumefikishwa mahali Rais wenu lazima akapatikane toka Dodoma kwa ridhaa ya Watanganyika! Viongozi wenu hao wa CCM wanafumbwa macho eti kwa vile tu maslahi yao yanalindwa. Wako tayari kushuhudia taifa linadhalilishwa na watu wenye mpango wa kufanya Zanzibar mkoa sawa na mikoa mingine ya Tanzania Bara. Nawaomba ndugu zangu wa Zanzibar okoeni taifa lenu na mlipe hadhi kamili inayostahili kama taifa ili muweze kunufaika. Iwapo mtashindwa kutekeleza wajibu wenu Oktoba 29, muelewe wazi kwamba, taifa la Zanzibar na umaarufu wake wote litaangamia. R.A. Lukwele,
Ndugu Mhariri TUMESIKIA au hata kuona toka Madiwani wa CCM mpaka wabunge wao rushwa ikitolewa na kupokelewa. Je, kiapo chao CCM kimekwenda wapi? Au kile kiapo kilikuwa enzi za TANU tu? Wakati wa pilika pilika za udiwani, mkubwa mmoja wa CCM katika kujiosha aliwahi kusema kwamba vurugu za rushwa ilisababishwa na Chama cha upinzani na alikitaja ni CUF. Sasa namuuliza Mheshimiwa, je, na hizo vurugu za wabunge Tanzania nzima mchawi nani? Udiwani ulidai CUF wametowa milioni nani (8), Mheshimiwa, je, na ubunge milioni ngapi za CUF iligawa kwa waheshimiwa hao Tanzania nzima? Uongo una mwisho. Mwaka 2000 ni ukombozi tu. Mohamed Mlawa,
|
YALIYOMO
TAHARIRI
Wazanzibar
wawaambia Dk. Omar na Karume:
CCM ni nguruwe aliyenona - Mtopea Kabobe asisitiza uchaguzi huru Mkapa aomba kura kwa hoja ya uzawa Vifaa vya uchaguzi vimeanza kusambazwa Mizengwe yatupwa,wagombea upinzani wapeta USHAURI NASAHA
MAKALA
Kampeni za uchaguzi Zanzibar zimetosha kumvua chui ngozi ya mwana kondoo MPASHO NASAHA
MAKALA
KALAMU YA MWANDISHI
MAKALA
MAKALA
CUF Tanga wamsihi Mufti wa BAKWATA aachane na siasa Kodi ya Maendeleo haitaondolewa -Mkapa |
|
|
|
|