NASAHA
Na. 065 Jumatano Septemba 13 - 19, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
HABARI 
Kabobe asisitiza uchaguzi huru
  • Aonya kutokea vurugu 
Na Mwandishi wetu 

MKUU wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Askofu Mkuu Zakaria Kakobe, ameendelea kuitaka serikali kuhakikisha uchaguzi mkuu wa mwaka huu unakuwa huru na haki ili kuepusha vurugu. 

Kwa mujibu wa gazeti moja la kila siku, Askofu Kakobe ametahadharisha kuwa endapo haki haitotendeka, wananchi hawatokubali kudhulumiwa na hivyo wanaweza kudai haki yao kwa nguvu, jambo linaloweza kupelekea kuvunjika kwa amani nchini. 

Ameikumbusha serikali na vyombo vyake kutoa haki sawa kwa vyama vyote , kwani alisema kiongozi huyo wa dini, amani ya kweli haipatikani paliposhamiri dhuluma. 

Askofu Kakobe mara kadhaa amekuwa akiikosoa CCM na serikali yake hadharani, jambo ambalo liliwahi kupelekea kutupiana maneno kati yake na viongozi hao wa chama tawala. Mathalani,aliwahi kuwataka wananchi kuihoji CCM kile ilichowafanyia kwa kipindi cha miaka 40 iliyopita kabla ya kuipa tena ridhaa ya kuongoza kipindi kingine cha miaka mitano. 


Mkapa aomba kura kwa hoja ya uzawa

Na Mwandishi Wetu 

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ndie rais anaemaliza muda wake Oktoba, Mhe.Benjamin Mkapa amewataka wananchi wa Mtwara wamchague kwa sababu amezaliwa mkoa huo. 

Akinukuliwa na gazeti moja la Jumapili iliyopia (Na. 018729)Rais Mkapa aliwataka wananchi hao wampigie kura kwa wingi kwa sababu amezaliwa katika mkoa wa Mtwara. Mhe. Mkapa ni mzaliwa waMasasi mkoani humo. 

Hata hivyo, gazeti hilo limemripoti Rais Mkapa katika ziara yake ya kampeni mkoani Mtwara akiwataka wananchi wasivichague vyama vya upinzani kwa sababu sera zao ni za ubaguzi wa kikabila,jino kwa jino,udini na jinsia. 


Vifaa vya uchaguzi vimeanza kusambazwa 

Na Mwandishi Wetu 

VIFAA kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu vimeanza kusambazwa sehemu mbali mbali nchini, imefahamika. 

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini jana, vifaa hivyo vimeanza kusambazwa jana kwa lengo la kuepuka matatizo yaliyojitokeza katika uchaguzi wa 1995. 

Aidha Tume hiyo ya uchaguzi imesema haina nguvu ya kisheria kuwadhibiti wanasiasa wanaofanya vurugu na kutumia udini katika kampeni. 

Mwanzoni mwa wiki hii, imeripotiwa kuwa baadhi ya wagombea ubunge waliripotiwa kupigiwa debe makanisani huko mkoani Kilimanjaro. 


Mizengwe yatupwa,wagombea upinzani wapeta 

Na Mwandishi Wetu 

MIZENGWE iliyodaiwa kuwekwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Liwale dhidi ya wagombea udiwani wa upinzani, hatimaye imetupwa na tume ya taifa ya uchaguzi na wagombea hao kuruhusiwa kuendelea na kampeni. 

Mizengwe hiyo iliyodumu kwa takriban siku 20 imekwisha kufuatia juhudi kubwa zilizofanywa na Katibu wa CUF wilaya ya Liwale Bw. Ahmed Mmou na Tume ya Uchaguzi ya Taifa ya chama hicho. 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Bw. Mmou alisema kuwa pamoja na kuchelewa kwa makusudi kwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo kutoa fomu kwa ajili ya madiwani, alitangaza kubadilika kwa picha kutoka zile za rangi na kuwa za kawaida (Blackand White) Aogist 14. 

Wagombea wa upinzani waliwasiliana na mpiga picha ambaye alipiga picha na kwenda kusafisha picha hizo Nachingwea akiahidi kurudisha picha hizo Agosti 17, lakini mpaka Agost 18 siku ya mwisho ambayo maelezo na picha za wagombea zilitakiwa kubandikwa kwenye ubao wa matangazo, mpiga picha huyo alikuwa hajarejea. 

Bw. Mmou alidai kuwa walimsihi msimamizi huyo kuwa aruhusu kubandikwa kwa picha za rangi ambazo zilikuwa zimeshaambatanishwa na maelezo mpaka zitakapoletwa picha nyeusi kutoka Nachingwea .Msimamizi huyo alikataa katakata, huku akiwatuhumu kuwa ni wazembe. 

Ilipofika saa 11.30 jioni ya siku hiyo baadaya kwisha muda, mpiga picha huyo alirejea jambo ambalo alidai Bw. Mmou liliwajengea dhana kuwa kuna mchezo umefanyika wa kuwahujumu. 

Baada ya hapo ulianza msururu wa mawasiliano ya barua kati ya viongozi wa upinzani jimboni humo na msimamizi huyo,lakini haikusaidia. Ndipo Bw. Mmou alipoamua kuja moja kwa moja hapa jijini kuwasiliana na tume ya Taifa ya uchaguzi ambayo, baada ya kukaa kikao chake maalum kwa ajili hiyo, wagombea hao waliruhusiwa kuendelea na kampeni zao. 

Mratibu wa uchaguzi wa Kanda ya Kusini alitarajiwa kuondoka jana kwenda Liwale kupelekea barua kwa wagombea hao na kwa msimamizi wa uchaguzi jimboni humo. 

Majina yawagombea udiwani haowa upinzani navyama vyao ni kama ifuatavyo:- 

Hassan Mkupeta,Saidi Abdallah (NCCR-Mageuzi) naJaphet AliKumbinga (CHADEMA). 

Kutoka CUF wapo Ahmad Nakwenda, AliLigai, Abdallah Ngatomela na Hemed Rashid. 

Wengine ni Abdallah Ngalemba, Kasim Kikowela, Ahmed A. Mmou na Abdallah Makere. 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Tume, kauli ipi sawa? 

CCM maji shingoni 

Wazanzibar wawaambia Dk. Omar na Karume:
Kura tutawanyima, mtang’oka 

CCM ni nguruwe aliyenona - Mtopea 

Kabobe asisitiza uchaguzi huru 

Mkapa aomba kura kwa hoja ya uzawa 

Vifaa vya uchaguzi vimeanza kusambazwa 

Mizengwe yatupwa,wagombea upinzani wapeta 

HABARI ZA KIMATAIFA

USHAURI NASAHA
Haya ndiyo mambo ya wanawake - 2 

MAKALA
Kura ni silaha 

Kampeni za uchaguzi Zanzibar zimetosha kumvua chui ngozi ya mwana kondoo 

MPASHO NASAHA
BEN NA BULLY 

MAKALA
Wimbo wa Umoja na Amani wa CCM  ni ghilba za kisiasa 

KALAMU YA MWANDISHI
Hojini Ubalozi wa Vatican kwanza 

MAKALA
CCM kushinda uchaguzi bila kupigiwa kura? 

MAKALA
Mwenye macho haambiwi tazama - 4 

CUF Tanga wamsihi Mufti wa BAKWATA aachane na siasa 

Kodi ya Maendeleo haitaondolewa -Mkapa 

Wazee waijibu CCM 

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Yanga watakiona - Kajumulo
  • Simba yajaribu kombe la FAT
  • Tarimba akataa ubabe
  • Jeshi laongeza timu Ligi Kuu

  •  

       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita