NASAHA
Na. 065 Jumatano Septemba 13 - 19, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
HABARI ZA MATAIFA

Upinzani washinda Mauritius 

KUFUATIA ushindi wa muungano wa upinzani nchini Mauritius, Waziri Mkuu Rom Gullam wa nchi hiyo ameahidi kujiuzulu baadaye wiki hii. 

Ushindi huo wa robo tatu ya viti vyote katika bunge umeifanya upinzani kupata viti 50 kati ya 70. 

Waziri Mkuu wa nchi hiyo inayotamba barani Afrika kwa kiwango chake cha kukua kwa uchumi kwa mwaka na mfano wa kuigwa kwa demokrasia, ameahidi kujiuzulu pamoja na kuwa ameweza kutetea kiti chake bungeni. 

Asilimia kuwa ya wakazi wa kisiwa hicho cha Mauritius ni wa asili ya asia. 


Burundi yaituhumu Tanzania kusaidia waasi

SERIKALI ya Burundi imetuhumu Tanzania kwa kuruhusu ardhi yake kutumiwa na waasi wa nchi hiyo ambayo imedai huingia nchini huo kufanya mashambulizi na kurejea Tanzania. 

Taarifa zilizotolewa kwa waandishi wa habari na Afisa wa jeshi la Burundi mjini Bujumbura. 

Katika hatua hiyo, majeshi ya Burundi, alisema afisa huyo majeshi yamesogezwa kwenye eneo la kusini mashariki ya mpaka wa nchi hiyo ambayo yanapakana na mkoa wa Kigoma. 

Aidha, nchi hiyo imeitaka Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuhakikisha nchi hizo haziruhusu ardhi zao kutumika na waasi hao ili kusaidia kuwepo kwa amani katika nchi hiyo ndogo ya Afrika ya kati iliyoathiriwa vibaya na vita ya kikabila. 

Nchi hiyo imependekeza kuwa Tanzania na DRC zishirikishwe kikamilifu katika utafutaji wa amani nchini humo ili kuweza kuwadhibiti waasi. 

Mara kwa mara serikali ya Burundi imekuwa ikiituhumu nchi jirani ya Tanzania kwa kuhifadhi waasi na kuwaruhusu kuishambulia nchi hiyo. Lakini serikali ya Tanzania mara zote imekuwa ikikanusha. 


Wapinzani wapata mafanikio DRC

WAPINZANI wa chama cha MLC kinachoendesha mapigano dhidi ya serikai ya Rais Laurent Kabila wa DRC kimetangaza kupata mafanikio baada ya kuuteka mji wa Dongo. 

Chama hicho chenye kuongozwa na Bw. Jean Pierre Bemba hivi karibuni kilitangaza kuanza kwa mapambano makali ya kuikomboa miji yote iliyotekwa na majeshi ya serikali. 

Katika mapigano hayo ya siku tatu ya kuuteka mji wa Dongo, Chama hicho kimedai kuwakamata mateka askari 43 wa serikali na kuwakamata wengine 100. Aidha kimedai kuwa wapiganaji wake wanne wameuawa. 

Mpaka sasas hakuna duru zozote huru zilizokanusha au kuthibitisha taarifa hizo zilizotolewa na katibu mkuu wa MLC. 

Vyombo vya habari vya serikali vimelaumu kuvunjwa kwa mkataba wa amani wa Lusaka kunakofanywa na MLC ambacho kimepania kumwondoa madarakani kwa njia ya mtutu Rais Laurent Kabila. 

DRC imekuwa katika kipindi kirefu cha vita vya ndani tangu kuangushwa kwa utawala wa Rais wa zamani wa nchi hiyo Mobutu Seseseko. 


Wapiganaji Kashmir wapambana na India 

WAPIGANAJI wa Kiislamu katika jimbo linalopigania uhuru wa kujiamulia mambo yake kutoka India wamewaua askari wanne wa jeshi la India katika shambulizi la kushutukiza la kujitoa muhanga. 

Shambulio hilo ambalo lilipelekea mapigano ya masaa sita, liliisha kwa India kushambulia kwa mizinga na maroketi jengo moja ambalo wapiganaji wawili wa Kashmir waliuawa. 

Katika tukio jingine mwanamke mmoja aliuawa baada ya kutokea mapigano katika eneo la Kashmir linaloshikiliwa kwa pamoja na India na Pakistan ambapo makombora yalitumika. 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Tume, kauli ipi sawa? 

CCM maji shingoni 

Wazanzibar wawaambia Dk. Omar na Karume:
Kura tutawanyima, mtang’oka 

CCM ni nguruwe aliyenona - Mtopea 

Kabobe asisitiza uchaguzi huru 

Mkapa aomba kura kwa hoja ya uzawa 

Vifaa vya uchaguzi vimeanza kusambazwa 

Mizengwe yatupwa,wagombea upinzani wapeta 

HABARI ZA KIMATAIFA

USHAURI NASAHA
Haya ndiyo mambo ya wanawake - 2 

MAKALA
Kura ni silaha 

Kampeni za uchaguzi Zanzibar zimetosha kumvua chui ngozi ya mwana kondoo 

MPASHO NASAHA
BEN NA BULLY 

MAKALA
Wimbo wa Umoja na Amani wa CCM  ni ghilba za kisiasa 

KALAMU YA MWANDISHI
Hojini Ubalozi wa Vatican kwanza 

MAKALA
CCM kushinda uchaguzi bila kupigiwa kura? 

MAKALA
Mwenye macho haambiwi tazama - 4 

CUF Tanga wamsihi Mufti wa BAKWATA aachane na siasa 

Kodi ya Maendeleo haitaondolewa -Mkapa 

Wazee waijibu CCM 

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Yanga watakiona - Kajumulo
  • Simba yajaribu kombe la FAT
  • Tarimba akataa ubabe
  • Jeshi laongeza timu Ligi Kuu

  •  

       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita