NASAHA
Na. 065 Jumatano Septemba 13 - 19, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
TAHARIRI 
S.L.P. 72045, Dar es Salaam

Tume, kauli ipi sawa? 

Hivi karibuni imeripotiwa katika vyombo vya habari, kauli za baadhi ya viongozi wa juu wa Chama Tawala ambazo tunadhani zinadhalilisha katiba ya nchi na demokrasia. 

Kauli za kwamba, wakishinda hatuwachii. Kauli kwamba, magari ya kivita yameandaliwa kupambana na wapizani. Au kauli za majigambo kwamba wananchi wapige kura wasipige kura chama tawala kitashinda. 

Nchi yetu ni huru. Haiko chini ya utawala wa Kikoloni wala wa kijeshi ni nchi inayoongozwa na katiba; katiba inayoashiria kuwepo kwa serikali iliyoingia madarakani kwa ridhaa ya wananchi. 

Ni kwa mujibu wa katiba hiyo, leo tuna vyama vingi, vyama ambavyo ni vya wananchi na vyote vina haki na hadhi sawa mbele ya katiba. Hivi sasa tupo kwenye kampeni za uchaguzi mkuu utakaofanyika mwisho wa mwezi ujao kwa mujibu wa katiba ya nchi. Uchaguzi mkuu ni fursa ya wananchi kuchagua viongozi wa chama kitakachounda serikali waitakayo. Serikali gani itakayochaguliwa ni siri ya wananchi itakayojulikana baada ya Oktoba 29 mwaka huu. Na ili hilo litimie hapana budi katiba ya nchi iheshimiwe, na sheria zilizounda tume ya uchaguzi, na zile zinazosimamia taratibu za uchaguzi pia ziheshimiwe. 

Wenye wajibu wa kuhakikisha yote hayo ni tume ya uchaguzi. Hivyo Tume ya Uchaguzi ina wajibu wa kuweka mazingira muafaka ambayo yatahakikisha kuwepo kwa haki na uhuru kwa mwananchi kujiandaa hivi sasa na kupiga kura tarehe 29 Oktoba pasipo vitisho, hadaa,kejeli au kebehi. 

Hivyo tunaposikia kauli kama hizo zilizotolewa na viongozi wa chama tawala siku kadhaa zilizopita, na tume kukaa kimya hatuna budi kujiuliza kama ambavyo wananchi wengi wamekuwa wakijiuliza, je, kauli hizo ni sahihi? 

Kauli za kwamba wakishinda hatuwaachii, haziendi kinyume na katiba? Na zile za kuwatangazia wananchi vitisho vya magari ya jeshi vinakubalika? Au zile za kuwaambia wananchi "watake wasitake, mpige kura msipige tutashinda", zinaashiria nini? 

Hivyo ni tegemeo letu kwamba tume haitoendelea kuzinyamazia kauli hizo maana itakuwa ni sawa na kuwaachia wananchi wachukue hatua zifaazo. 

Hatuamini kwamba hiyo ndiyo nia ya tume. Bado tuna imani na matarajio mema kwa Tume kutimiza wajibu wake. 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
Tume, kauli ipi sawa? 

CCM maji shingoni 

Wazanzibar wawaambia Dk. Omar na Karume:
Kura tutawanyima, mtang’oka 

CCM ni nguruwe aliyenona - Mtopea 

Kabobe asisitiza uchaguzi huru 

Mkapa aomba kura kwa hoja ya uzawa 

Vifaa vya uchaguzi vimeanza kusambazwa 

Mizengwe yatupwa,wagombea upinzani wapeta 

HABARI ZA KIMATAIFA

USHAURI NASAHA
Haya ndiyo mambo ya wanawake - 2 

MAKALA
Kura ni silaha 

Kampeni za uchaguzi Zanzibar zimetosha kumvua chui ngozi ya mwana kondoo 

MPASHO NASAHA
BEN NA BULLY 

MAKALA
Wimbo wa Umoja na Amani wa CCM  ni ghilba za kisiasa 

KALAMU YA MWANDISHI
Hojini Ubalozi wa Vatican kwanza 

MAKALA
CCM kushinda uchaguzi bila kupigiwa kura? 

MAKALA
Mwenye macho haambiwi tazama - 4 

CUF Tanga wamsihi Mufti wa BAKWATA aachane na siasa 

Kodi ya Maendeleo haitaondolewa -Mkapa 

Wazee waijibu CCM 

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Yanga watakiona - Kajumulo
  • Simba yajaribu kombe la FAT
  • Tarimba akataa ubabe
  • Jeshi laongeza timu Ligi Kuu

  •    Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita