|
|
| Mlo
wa Daku
Na Mujahid Mwinyimvua KATIKA makala ya chakula na lishe ya wiki iliyopita tulitoa somo maalum (futari ya tende) kwa ajili ya wasomaji wetu Waislamu wanaotarajia kuanza funga ya mwezi wa Ramadhani siku chache zijazo. Kwa muhtasari tulisema kwamba Waislamu na wanadamu wote kwa ujumla wanahimizwa na Qur’an kufanya uchaguzi wa vyakula wanavyokula (tazama Qur’an 2:168, 2:178, 5:88). Sababu ya uchaguzi huo ni kwamba Mwenyezi Mungu katika kuumba kwake vyakula vingine anavifanya bora kwa kula (ladha, virutubisho n.k.) kuliko vingine (tazama Qur’an 13:4). Vile vile tulisema kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.) amewahimiza sana Waislamu kufuturu kwa tende. Pamoja na vitu vingine, tende ina sukari (glucose) ambayo inaweza kuyeyuka kwa haraka tumboni na hivyo kuweza kutumika na mwili kwa muda mfupi na hivyo kuweza kuupa mwili nguvu (nishati). Jambo hili ni muhimu sana kwa mtu aliyefunga. Pia tulisema kwamba, kwa kuzingatia virutubisho vinavyopatikana katika tende, futari yoyote ile lazima itengenezwe kwa kutumia vyakula vyenye sukari na pia vyakula futari hivyo visiwe na mafuta mengi. Makala yetu ya wiki hii mwendelezo wa kusudio la makala ya wiki iliyopita. Somo tuliloliwakilisha wiki hii ni mlo wa daku. Katika makala hii neno daku ni chakula kinacholiwa usiku wa manane kwa ajili ya kujiandaa kufunga siku inayofuata. Kula daku ni sunnah aliyoikokoteza sana Mtume (s.a.w.) kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo: "Anas (r.a.) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Kula daku kabla ya alfajiri kwa sababu katika daku kuna baraka". (Abu Daud). Mlo wa daku unaweza kuwa mlo wowote ule hata kama maji ya kunywa kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo: Amesema Abu Said Khudri (r.a.) kwamba: "Daku ni baraka kwa hiyo msiliache japokuwa kwa tunda la maji. Maana Mwenyezi Mungu na Malaika wake huwarehemu wanaokula daku". (Ahmad) Hata hivyo, ni vyema ikakumbukwa kwamba kusudio kubwa la daku ni kumpa nguvu mfungaji na ndiyo maana Mtume (s.a.w.) alihimiza watu kula daku karibu na alfajiri. Mtu asidhani kuwa kula daku mapema kuwa ndiyo ucha Mungu. Ibada ya funga (na nyinginezo) haikukusudiwa kuwatesa wafungaji. Mlo wa daku lazima uwe mlo kamili (balanced diet) hasa kama mtu hakupata mlo mwingine baada ya kufuturu. Kitendo cha kuchelewesha mlo wa daku na kuwahi kufuturu (mambo ambayo yanasisitizwa na Uislamu) maana yake ni kuwa muda wa mwili kukosa chakula unapungua. Hivyo basi afya ya mfungaji haiathiriki. Mtume (s.a.w.) kama alivyosisitiza kufuturu kwa tende pia amehimiza daku ya tende. Haya tunayapata katika Hadith ifuatayo: Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Ni uzuri ulioje kwa muumini kula daku ya tende kabla ya alfajiri". (Abu Daud) Katika toleo lililopita katika mfululizo huu, kimakosa tulichapisha kuwa futari iwe na mafuta mengi, lakini usahihi ni kwamba futari isiwe na mafuta mengi. Tunawaomba radhi mwandishi na wasomaji wetu. - Mhariri |
YALIYOMO
Tahariri Umaskini unachafua mazingira! Mauaji ya Mwembechai: Spika wa Bunge aombwa atoe gharama za kuunda Tume UN yaidhinisha udhalimu wa Marekani Qur’an yachomwa moto Shinyanga Marekani yadhihirisha Ubeberu wake MARADHI
YA KISAIKOLOJIA: SEXUAL SADISM
Kitengo cha Zaka chazinduliwa Dar Tume ya Jiji kubomoa Msikiti wa vipofu Akheri ya
zamani
UWAWARU yaleta nusura Ikwiriri Tamko la Masjid NNUUR juu ya kuanzishwa kwa UWAWARU Wasomi
Waislamu wawajibike
Madrasa Akhlaqil Islamiya yapiga hatua MADRASATUL
Husseiniyi Shadhily
Changieni vyombo vya mihadhara - Sheikh Said Misikiti yakosa maji ya kutawadhia Bakwata Tanga haifuati katiba yake Sheikh Mbukuzi ataka Waislamu watafute radhi za Allah Je,
hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 3
Njia
ya uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 3
Sheikh Omar Bashir afikishwa mahakamani Mufti pekee kuidhinisha watu kufunga Nguruwe wanaofugwa maeneo wanayoishi watu kusababisha magonjwa ya kuambikiza Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|