|
|
| Kitengo
cha Zaka chazinduliwa Dar
KITENGO cha Zakat na Sadaqa kinachojulikana kama The Dar es Salaam Yemen Community for Charity & Culture (D.Y.C.C.C) Jumapili ya Desemba 13, mwaka huu kilizinduliwa rasmi katika ukumbi wa Starlight Jijini. Katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa mfuko huo wa Zakat na Sadaqa Sheikh Saidi A. Abri alitoa taarifa fupi kuhusiana na kitengo chake na kusema tatizo kubwa linaloikabika jumuiya yake ni uchache wa watoaji wa zakati na sadaqa wakati ambapo wanaohitaji kupewa ni wengi. Amewahimiza Waislamu kulipa suala hili uzito unaostahiki kwani ni miongoni mwa nguzo za Uislamu na imepewa msisitizo mkubwa katika Qur’an. Naye mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Mhe. Iddi Simba Waziri wa Viwanda na Biashara katika nasaha zake kwa Waislamu waliohudhuria uzinduzi huo akiwataka Waislamu kutekeleza nguzo ya Zakat ili kuweza kusaidia katika mambo mbalimbali. Zawadi mbalimbali zilitolewa katika uzinduzi huo ambazo zilikabidhiwa kwa baadhi ya wahitaji. Akitoa nasaha zake Mbunge wa Dodoma Mjini Mhe. Hashim Saggaf katika
nasaha zake aliwataka wale wote waliopewa zawadi kuzitumia vizuri na kuwataka
wale wenye uwezo wajijengee utamaduni wa kutoa misaada kwa ndugu zao wasiokuwa
na uwezo.
Tume ya Jiji kubomoa Msikiti wa vipofu
Kwa mujibu wa barua iliyoandikiwa Bakwata kuiomba iingilie kati suala hili; kabla ya kuingia kwa Tume ya Jiji watoto hao wasioona walipewa jengo moja walitumie kama Msikiti. Jengo hilo lilitumika hadi kufikia Mh. Keenja kuwa Bwana Mkubwa wa Jiji, imesema sehemu ya barua hiyo. Ambapo barua hiyo inadai kwamba yeye Mh. Keenja ameona hakuna umuhimu wowote jengo hilo kutumiwa na watoto hao vipofu kumuabudia Mola wao na hivyo yako mbioni kuligeuza litumike kwa shughuli nyingine. Barua hiyo No. TABMO/RE/66 ya Desemba 13 iliyosainiwa na Katibu Mkuu wake Bw. Amiri A.S. Andanenga imemuomba Katibu Mtendaji wa Bakwata afanye hima kuwaokolea wanafunzi Waislamu wasioona sehemu yao muhimu kwa ibada kabla hawajaangukiwa na nyundo ya Tume ya Jiji. Juhudi za kumpata Bw. Keenja ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Jiji kuzungumzia suala hili hadi tunakwenda mitamboni hazikuweza kufanikiwa. Waislamu wasioona nchini wameunda umoja wao ambao hujulikana kwa jina la "Tanzania Blind Muslims Organisation" (TABMO) na moja ya shughuli zao ni kuwasaidia watoto wasioona walio mashuleni katika jumla ya kuwarahisishia kujua Uislamu wao na kuwajengea mazingira ya kuutekeleza. Makao Makuu ya Chama hicho yapo Dar es Salaam yakitumia anuwani P.O. Box 90228. Kwa sasa Katibu Mkuu wake ni Mzee Amiri A.S. Andanenga. |
YALIYOMO
Tahariri Umaskini unachafua mazingira! Mauaji ya Mwembechai: Spika wa Bunge aombwa atoe gharama za kuunda Tume UN yaidhinisha udhalimu wa Marekani Qur’an yachomwa moto Shinyanga Marekani yadhihirisha Ubeberu wake MARADHI
YA KISAIKOLOJIA: SEXUAL SADISM
Kitengo cha Zaka chazinduliwa Dar Tume ya Jiji kubomoa Msikiti wa vipofu Akheri ya
zamani
UWAWARU yaleta nusura Ikwiriri Tamko la Masjid NNUUR juu ya kuanzishwa kwa UWAWARU Wasomi
Waislamu wawajibike
Madrasa Akhlaqil Islamiya yapiga hatua MADRASATUL
Husseiniyi Shadhily
Changieni vyombo vya mihadhara - Sheikh Said Misikiti yakosa maji ya kutawadhia Bakwata Tanga haifuati katiba yake Sheikh Mbukuzi ataka Waislamu watafute radhi za Allah Je,
hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 3
Njia
ya uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 3
Sheikh Omar Bashir afikishwa mahakamani Mufti pekee kuidhinisha watu kufunga Nguruwe wanaofugwa maeneo wanayoishi watu kusababisha magonjwa ya kuambikiza Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|