AN-NUUR 
Na.180 Shaaban 28 - Ramadhan 1419, Desemba 18 - 24, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Albucasis 936 - 1013 (CE)
 

ABDUL Qasim Al Zahrawi (Albucasis) alikuwa bila shaka yeyote ni Daktari mwenye taaluma kubwa ya (surgery) upasuaji wakati wa zama za kati yaani ‘medieval period’. Yeye ameweza kugundua aina mbalimbali ya tiba na njia za upasuaji na teknolojia ya kutengeneza na kubuni vyombo vya upasuaji (surgical instruments) ambavyo vinakisiwa kutimia mia mbili hivi. 

Alikamilisha Encyclopaedia ya matibabu na upasuaji ambayo hadi leo imetia fora isiyo kifani katika historia ya fani ya ya surgery na kuweza kutambulikana kama ‘The Father of modern surgery’ yaani baba wa fani ya upasuaji wa kisasa. 

Elimu yake hiyo aliipata katika mji wa Qurtuba, ambao ulikuwa ni mji mkuu wa Ukhalifa wa Kiislamu wa Spain na kujiendeleza katika Chuo cha Utabibu kilichokuwepo katika Falme ya Kiislamu iliyopo Baghdad, mji mkuu wa Iraq. Aliwahi kupata wadhifa wa Daktari wa Mfalme Al Hakam II wa Spain. 

Katika uhai wake mji wa Qurtuba ulikuwa ni maarufu sana kwa upokeaji Rufaa za upasuaji kutoka Ulaya na Asia. Katika kitabu cha ‘History of Arab Medicine’ kilichoandikwa na Dk. Campbell alitaja ‘Al Zahrawi’s principles of medical services surpassed those of Galen in the European medical curriculum’ yaani misingi ya sayansi ya utatibu Al Zahrawi yamevuka kikubwa sana mitaala ya fani hiyo ya Galen katika utabibu wa Ulaya. 

Encyclopaedia inayosifika zaidi ni ile ya Juzuu thelathini inayoitwa Al- Tasrif Li man ajaz an-il-talif ‘yaani kitabu kinachomwezesha asieweza kusoma vitabu vikubwa kuelewa taaluma’ ambayo imefafanua elimu ya upasuaji, zana za upasuaji na michoro ya kueleza namna ya upasuaji wa maumbile ya ndani ya mwili "Anatomy". 

Taaluma hii ya Udaktari ilizama zaidi katika fani za matibabu ya macho, masikio, koo, uzazi, utoaji wa mawe katika kibofu cha mkojo na upasuaji katika sehemu za mifupa na viungo. Yeye alikuwa ni wa mwanzo kutumia nyuzi za hariri katika ushonaji unaoutumika baada ya upasuaji. Katika fani ya utabibu wa meno "Dentistry" alianzisha uwekaji meno bandia na kusahihisha fizi zilizokaa upande. Vitabu vyake vimetafsiriwa katika lugha za Latin, Kiingereza, Kifaransa na Kihibrania. Mmoja kati ya Daktari mashuhuri wa Kifaransa aitwaye Guy de Chaulic (1300 - 1368) alinakili: ufundishaji wa Al Zahrawi katika kitabu chake cha upasuaji. Hapa vilifatia vitabu vingi ambavyo vilichapishwa Venice (1541) Basel (1541) na Oxford (1778) ambavyo vimenakili na kufafanua mafundisho ya Al Zahrawi. Mafundisho haya yamedumu hadi katika karne hii na kutoa ufafanuzi unaondeleza taaluma hii ya surgery. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri
Umaskini unachafua mazingira!

Mauaji ya Mwembechai: Spika wa Bunge aombwa atoe gharama za kuunda Tume

UWAWARU yafa Rufiji

UN yaidhinisha udhalimu wa Marekani

Qur’an yachomwa moto Shinyanga

Marekani yadhihirisha Ubeberu wake

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: SEXUAL SADISM
Na. Abu Halima Sachangwa

Kitengo cha Zaka chazinduliwa Dar

Tume ya Jiji kubomoa Msikiti wa vipofu

Akheri ya zamani
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC. USA

UWAWARU yaleta nusura Ikwiriri

Tamko la Masjid NNUUR juu ya kuanzishwa kwa UWAWARU

Kuanzishwa kwa UWAWARU

Wasomi Waislamu wawajibike
Na Mwandishi Wetu

Albucasis  936 - 1013 (CE)

Ijue Uhuru madrasa - Morogoro

Madrasa Akhlaqil Islamiya yapiga hatua

MADRASATUL Husseiniyi Shadhily
Na Jamillah Nassoro
 
Hatimaye kesi ya kushambulia kituo nayo yafutwa

Changieni vyombo vya mihadhara - Sheikh Said

Misikiti yakosa maji ya kutawadhia

Bakwata Tanga haifuati katiba yake

Sheikh Mbukuzi ataka Waislamu watafute radhi za Allah

Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 3
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache - 3
Na Yasin Valerian Massawe

Sheikh Omar Bashir afikishwa mahakamani

Mufti pekee kuidhinisha watu kufunga

Nguruwe wanaofugwa maeneo wanayoishi watu kusababisha magonjwa ya kuambikiza

200 wamesilimu

Sayansi na Teknolojia 
[Kuiweka Modem kwenye Kompyuta] 
 
Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Mlo wa Daku] 
 
Tangazo 
New Book: The untold story of the Muslim struggle against British Colonialism in Tanganyika. 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita