NASAHA
Na. 082 Jumatano Januari 10 - 16, 2001
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
MASHAIRI

Kijijini

Kijijini nakupenda, kunamahindi nandizi,
Kunayo mengi matunda, kunde, dengu na mbaazi,
Kuna mtamu mlenda, namkumbuka Shangazi,
 Mwenzenu ninakupneda, sana kijijini kwetu.

Jamani babu nabibi, kijijini wamepozi,
Jamani kuku wa bibi, na wale wa babu mbuzi,
Nataka kwenda kwa bibi, kula mihogo na ndizi,
 Mwenzunu na kukumbuka, sana kijijini kwetu.

Ifikapo asubuhi, JOGO la babau huwika,
Watu shambani huwahi,ili jembe kulishika,
Ndege nao hufurahi, mitini hufurahika,
Mwenzunu na kukumbuka, sana kijijini kwetu.

Amewaumba billahi, wazuri waloumbika,
Na angani hufurahi, wavutia kwa hakika,
Na Maji nayo Wallahi, TUNGINI yazizimika,
 Mwenzetu nakukumbuika, sana kijijini kwetu.

Almasi H. Shemdoe, “
Tunda la Matumaini”, 
Dar es Salaam, Tanzania.


Tabia za Watanga

Leo nachukua Tanga, kama fumbo jamiini,
Kuwaeleza Watanga, TABIA zao nchinini,
Tanga watu wa kuringa, hasa kwa kujua dini,
 Ukitaka uishi nao, jifunye wewe mjinga.

Tanga bwana kwa mamwinyi, karahaatake nani,
Tanga si kwa bwana Mwinyi, kwangu mwana wa HASANI,
Tanga utaminywa minyi, kwa fani ya ugangani,
 Ukitaka ishinao, jifanyewewe mjinga.

Watanga kwa majivuni, hakuna tena nchini,
Hjawachelewi kulani, wakipewa mtihani,
Tanga watu wa kulani, harakati ziko chini,
 Ukitaka ishinao, jifanye wewe mjinga.

Tanga kuzuli lakini! Kunapendeza machoni,
Hasa kwetu milimani,kule Lushoto nyumbani,
Tanga mjini jamani, KISIMA cha Qur-ani,
 Ukitaka ishi Tanga, jifanye wewe mjinga.

Tanga jama amekeni, wa Tanga badilikeni,
Ngangari wote kueni, ndivyo apenda manani,
Watanga moto washeni, umwinyisasa acheni,
 Ukitaka ishi Tanga,jifanye wewe mjinga.

Sita beti nimwishoni, Tanga kwenu ni fumboni,
Ngangari wapojueni, KILIMILE muoneni,
Wakali wa kila fani, Tanga hawakosekani,
 Ukitaka ishi Tanga, jiganye wewe mjinga.

Almasi H. Shemdoe, 
“Tunda la Matumaini”,
 Dar es Saaam.



Bandari Salama

Dar es Salaam yaleo, ndiyo Bandari Salama,
Myaka mingi hadi leo, mji wenye usalama,
Mji wa maendeleo, mji wa walikwa nyama,
 Karibuni ni walimwengu, mwone Bandari Salama.

Bandari ya raha leo, jiji maarufu sana,
Bandari yenye vileo, makabila chungu sana,
Taifani tegemeo, viwanda vimejazana,
 Karibuni walimwengu, mwone Bandari Salama.

Jiji lawatu kibao, hilo Bandari Salama,
Jamani urithi wao, toka tangu nyingi za miaka
Kutoka kwa Babu zao, akawapa Mola mwema,
 Karibuni walimwengu, mwone Bandari Salama.

Bora mawasiliano, Bandari Salama leo,
Bandari ya mapatano, kwa nchi yetu ya leo,
Taifani ni mfano, kwa yetu maendeleo,
 Karibuni walimwengu, mwone Bandari Salama.

Baba Bandari Salama,sasa ni Dar es Salaama,
Chetu kivutio chema, Badari ya watu wema,
Wapl.e wasio vuma, wakazi Dar es Salama,
 Karibuni walimwengu, mwone Bandari Salama.

Beti sita kaditama, karibu Dar es Salama,
Njoo Bandari Salama, Pwani upate simama,
Upepo Mwanana mwema, ufukwelini unavuma,
 Karibuni Walimwengu, mwone Bandari Salama.

Almasi H. Shemdoe
, “Tunda la Matumaini”,
Dar es Salaam, Tanzania.
 

Juu
 

YALIYOMO
 

MAONI YETU
Mapinduzi Zanzibar yameleta kilichokusudiwa?

Wananchi wamwambia Mkapa:
Mbumbumbu wa demokrasia waliomo katika chama tawala ni hatari zaidi

Waislamu watakiwa kuwa watekelezaji wa maamuzi

‘Hajj Trust’ yaongeza huduma kwa mahujaji

DONDOO MUHIMU

MAKALA
Jamii ijihadhari viongozi wasaliti

MAKALA
Msimamo wa Pengo haushangazi

KALAMU YA MWANDISHI
Kitendawili cha millenia: Urais bila dola

MAKALA
Dhana ya kumwabudu Mungu anayeafiki udhalimu lazima tuikatae

MAKALA
Mapinduzi Zanzibar: Dhuluma bado ipo

MAKALA
CCM haiwezi kuondosha umasikini Tanzania

MAKALA
Tirivyogo la sekta ya elimu

Mwenye Macho……
Demokrasia haiwezi kujengwa kwa kuvunja katiba

HABARI ZA KIMATAIFA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Baadaya Mkapa kushindwa kusaidia: Prof. Lipumba aombwa kuiombea Tanzania FIFA
  • Mtwa aanza kulala mapema
  • Salvatory aitwa Mtibwa

  •    Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita