NASAHA
Na. 035 Jumatano Februari 16 - 22, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
HABARI ZA KIMATAIFA



Matokeo kutoathiri sera ya mashamba

HARARE, Zimbabwe. 

Kura ya maoni iliyopigwa wiki iliyopita nchini Zimbabwe licha ya kutoa ushindi mkubwa kwa walio dhidi ya serikali ya chama cha ZANU-PF kinachoongozwa na Rais Mugabe bado matokeo hayo hayatoathiri sera ya Serikali ya kuchukua mashamba kutoka kwa Wazungu na kuwagawia Wazalendo wa nchi hiyo ambao wengi wao ni Waafrika weusi. Kura ya maoni iliitishwa ili kutoa maoni juu ya muswada wa kumuongezea madaraka Rais. 

Katika matokeo ya kura hiyo robo tatu asilimia wameupinga muswada huo. Zimbabwe inatarajia kufanya uchaguzi mkuu wa Bunge mwezi Aprili mwaka huu. 

Muswada huo uliokwama uliokuwa na lengo kumuongezea Rais madaraka umetafsiriwa na walio dhidi ya chama cha ZANU-PF kuwa ni agenda ya Rais Mugabe kumbakiza madarakani kwa muda zaidi. 

Rais Mugabe amekuwa Rais wa nchi hiyo kwa muda wa miaka ishirini hadi hivi sasa. Pamoja na matokeo hayo, msimamo wa serikali bado ni ule ule wa kuwagawia mashamba walio maskini kutoka kwa matajiri. Kwa muda mrefu hivi sasa Zimbabwe imekuwa katika mgogoro wa lipi lifanyike katika kuwapatia mashamba wasiokuwa nayo, walio wengi, kutoka kwa wamiliki wachache. 


Afrika yasifiwa kutoa mazao bora

BANKOOK, Thialand. 

Ripoti ya Umoja wa Matiafa imeisifu Afrika kuwa ni Bara linaloendelea kuongoza kwa ubora wa mazao yake. Katika mkutano wa mawaziri, ripoti hiyo ya UNCTAD imesema kuwa Afrika inaonesha kuwa ni maskani njema katika kutia rasilimali baadaye mwaka huu. Mazao yanayozalishwa katika bara la Afrika ni pamba ambayo huzalishwa kwa wingi huko Sudan na baadhi ya sehemu za Tanzania na zao la buni ambalo hulimwa kwa wingi maeneo ya milima na ukanda baridi wa bara hili. Mazao mengine ni mkonge, korosho na mengi ni ya mazao ya kilimo. Katika mkutano huo nchi zinazoendelea zimezitolea mwito nchi tajiri kurekebisha mifumo ya kibiashara ambayo haileti nafuu kwa nchi maskini. Vile vile nchi hizo zimezitaka nchi tajiri kuzifutia madeni nchi changa. Mwaka jana mataifa saba tajiri duniani yaliahidi kuzifutiamadeni nchi zinazodaiwa kwa masharti kuwa madeni hayo yatumike katika huduma za jamii. 


UNITA waendeleza mapigano

WINDHOEK, Namibia.

Waiganaji wa UNITA wamendeleza wimbi la mapigano katika harakati za kudai haki ya kupewa fursa sawa ya utawala nchini Angola dhidi ya Serikali iliyopo madarakani. Wapiganaji hao waliwaua wananchi kadhaa wiki hii katika mji wa Antagrara.

Rais Sam Nujoma wa Namibia ameahidi kushirikiana na serikali iliyopo madarakani katika kupambana na UNITA. 

Hata hivyo pamoja na kuwa Rais Nujoma ameahidi kufanya hivyo kwa upande wa mpaka wa Namibia, Umoja wa Makanisa ya Kikatoliki nchini humo yameilaumu Serikali ya Rais Nujoma kwa kuona kuwa vita ndio njia pekee ya kuleta suluhisho la amani katika eneo hilo. Makanisa hayo licha yakuikemea serikali hiyo yametaka njia ya mazungumzo itumike ili kuleta suluhisho la amani. 

Angola imekuwa katika vita na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa miongo kadhaa hali ambayo imegharimu maisha ya Waafrika wa nchi hiyo kwa kiasi kikubwa. 

Imeelzwa kuwa chanzo kikuu cha mgogoro huo ni kutokana na tofauti za kiitikadi kati ya itikadi ya kijamaa ya chama tawala cha MPLA na ile ya kibepari ya UNITA huku kila upande ukitetea itikadi ya wazo mpachiko na kuacha mfumo maridhawa wa Kiafrika. 


Rais wa Ujeramani ziarani mashariki ya kati 

JERUSALEM

Rais wa Ujerumani Bwana Yohannes Rao ameanza ziara ya siku kumi na moja, ziara ambayo itamchukua katika nchi mbili pamoja na Israel.

Nchi atakazozitembelea Rais huyo katika ziara hiyo iliyoanza jana ni Palestina na Misri. 

Akiwa huko Israel anatarajiwa kulihutubia Bunge la nchi hiyo pamoja kuhamasisha kuongeza ukaribu wa urafiki kati ya Wajerumani na Wayahudi. 

Wajerumani na Wayahudi wamekuwa katika uadui kutokana maangamizo makubwa ya Wayahudi yaliyofanywa na Wajerumani kipindi cha utawala wa Adolf Hitler, hali ambayo kizazi kilichopo kinajitahidi kuihusisha kwa kufanya ushirikiano wa aina mbalimbali. 

Rais Rao akiwa nchini Palestina anatarajiwa kugusia suala la amani ya Mashariki ya Kati pamoja na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Ziara hiyo itamalizikia Misri kwa kukutana na Rais Hosni Mubaraka. Rais Hosni Mubaraka anatarajiwa kuzungumzia pamoja na mambo mengine kuhusu kukatishwa ziara iliyokuwa ifanyike nhini mwake mwaka jana na Waziri wa Ujerumani Bwana Yoska Fisher. 

Juu
 

YALIYOMO
 

Tahariri:
Serikali itoe hatma ya mauaji ya Mwembechai 

Wanafunzi wa Kiislamu shule za sekondari za serikali Dar wanyanyaswa 

Kanisa liliishinikiza serikali-Waislamu

Sakata ya mabadiliko ya Katiba Zanzibar 

Kukiri kosa na kuomba radhi ndio kipimo cha utu 

HABARI ZA KIMATAIFA 

Ushauri Nasaha  
Kuongoza tabia za watoto 

MAKALA 
Uhuru wa pili na ukombozi wa mwananchi 

MAKALA 
Umuhimu wa uchumi katika Uislam 

Kalamu ya Mwandishi 
Kwa nini kadhia ya Mwembe Chai isifanyiwe uchunguzi? 

Makala 
UPINZANI  OCTOBA 2000 - 3 

MAKALA
MAREKEBISHO YA 13 YA KATIBA YA  JAMHURI YA MUUNGANO: Wananchi Tanzania amkeni 

Riwaya 
Ndoto ya mafanikio 

LISHE 
Vyakula vitupatiavyo mafuta 

Barua/Maoni

MASHAIRI

MICHEZO

  • Tauzany afurahia ligi ya makundi 
  • Kibadeni hakutokomea na fedha za usajili- Milambo 
  • FAT yamuangukia Gama

  •  

     


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com


    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita