AN-NUUR
Na.165 Jamadul Awwal 1419, Septembe 4 - 10, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Aliyeandika Yesu si Mungu bado akabiliwa na kesi 

- Adaiwa kujeruhi imani ya wengine 
- Ahoji waliojeruhiwa wako wapi? 
- Ustaadh Uliza arejeshwa rumande 

Na Mwandishi Wetu 

KIJANA Latifu Ismail Khan ambaye alikamatwa kwa kuandika baiskeli yake "Yesu si Mungu" bado anakabiliwa na kesi ya jinai kwa kile kilichodaiwa kwamba ni kuhatarisha amani. 

Kesi hiyo ambayo ipo katika mahakama ya Mwanzo mjini Korogwe imepangwa kuzungumzwa tena Septemba 22, 1998. 

Kwa mara ya kwanza kijana huyo alikamatwa Machi 28, mwaka huu na kupelekwa mahakamani Aprili 1, ambapo Mwendesha Mashitaka (polisi) Bw. Emanuel Kalenga alidai kwamba mtuhumiwa alihatarisha amani kwa kuandika kwenye baiskeli yake kwamba "Yesu si Mungu". 

Mtuhumiwa alikanusha na kwa vile upande wa mashitaka ulidai kwamba upelelezi umekamilika, mahakama ilipanga kesi ianze kusikilizwa. 

Katika kesi hii inayoshitaki ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mashahidi wake ni polisi wawili ambao kijana Latifu amewataja kwamba ni Bw. Stamili na Robert. Akiongea na mwandishi wa habari hizi mjini Korogwe Agosti 31, Latifu amedai kwamba kesi hiyo imeshazungumzwa mara moja tu, kwani mashahidi wamekuwa hawaji mahakamani. 

Kwa mara ya kwanza amesema ilizungumzwa Mei 24, ambapo shahidi wa kwanza Bw. Stamili alishuhudia kuona baiskeli kuandikwa "Yesu si Mungu" na akadai kwamba kwa kufanya hivyo mtuhumiwa alijeruhi imani ya watu wengine na hivyo kuhatarisha amani. 

Katika utetezi wake Bw. Latifu alitaka kujua kutoka kwa shahidi endapo kutangaza imani tofauti na watu wengine iwe kwa maneno au kwa maandishi kunahatarisha amani. Kwa maelezo ya Latifu, polisi Stamili (shahidi) alijibu kwamba kuna watu wanalalamika, ambapo alitakiwa na mshitakiwa awalete mahakamani hao wanaolalamika. Mpaka kesi ilipoahirishwa kwa mara ya mwisho Agosti, 28, bado Bw. Stamili alikuwa hajawaleta walalamikaji hao. 

Pamoja na hayo Bw. Latifu alitaka kujua kwa shahidi kwamba ni imani ipi inayokubalika mbele ya sheria za Tanzania; Yesu ni Mungu au Yesu si Mungu, ambapo alijibu kwamba zote zinakubalika. 

Shahidi wa pili Bw. Robert alikuwa atoe ushahidi wake Agosti 28, lakini hakutokea mahakamani. Kwa mujibu wa maelezo ya Bw. Latifu kesi imepangwa kusikilizwa tena Septemba 22, 1998. 

Akiongea na mwandishi wa habari hizi nyumbani kwao mjini Korogwe, Bw. Latifu Ismail Khan ametoa wito na kuwakumbusha Waislamu wote kwamba wamche Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha na kuhakikisha kwamba hawafi ila wamekuwa Waislamu kamili. 

Wakati huo huo, mshiriki maarufu wa mihadhara ya kidini Jijini Dar es Salaam, Ustaadh Uliza Rashid amerejeshwa rumande baada ya dhamana yake kufutwa kwa madai ya kutohudhuria mahakamani mara kadhaa wakati wa kesi yake ikitajwa. 

Ustaadh Uliza ameshitakiwa kwa tuhuma ya kuhusika na vurugu zilizotokea mwaka jana (1997) katika mhadhara uliofanyika katika maeneo ya Mwananyamala jirani na kituo cha polisi cha Msisiri. 

Mapema mwaka huu wakati akizungumza na viongozi wa dini katika ukumbi wa Karimjee, Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Ali Ameir aliagiza kufutwa kesi zote zinazohusiana na mihadhara ya kidini iliyofanyika kabla ya kikao hicho na aliahidi kwamba serikali ilikuwa ikifungua ukurasa mpya wa mawasiliano na dini zote. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 
 
TAHARIRI 
HAKI YA KUABUDU MASHULENI: Hoja ya uwingi isizuie haki ya wachache 

Aliyeandika Yesu si Mungu bado akabiliwa na kesi 
Na Mwandishi Wetu 

Wazazi walia na Mkuu wa shule Mkwawa 
Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Serikali iache kudhulumu  Waislamu - Bakwata  
Na Mwandishi Wetu

KESI YA MIRATHI: Hukumu ya Jaji Agostino yatupwa 
Na Mwandishi Wetu 

Sumaye sasa atoa ‘waadhi’ Msikitini 
Na Mwandishi Wetu, Arusha 

Sekondari ya Kiislamu Sumbawanga, mtihani kwenu – Sheikh Akilimali 
Na Harun Rashid, Sumbawanga 

37 wasilimu  Mwanza 
Na Mwandishi Wetu, Mwanza 

Akamatwa kwa kusoma gazeti la ANNUUR ! 

MGOGORO WA CHWAKA NA MARUMBI: Serikali ya Dk. Salmin itafute ufumbuzi 
Na Mwandishi Wetu, Pemba 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 4 

Kwa nini walengwa wa mabomu wawe ni Marekani? 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Profesa amekosea kusema kwamba... 
Na A.M. Hamza 

Ugaidi ni ugaidi, hata wa Marekani ni ugaidi 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Dhana ya Udugu wa kiislamu 

UGAIDI: Chanzo si magaidi, ni dhuluma ya Marekani 
Na HASSAN KIMANGALE 

Jengeni familia bora 
Na Abuu Said, Iringa 

Tuwasaidie Waislamu kielimu na kiuchumi - Bi Zuhura 
Na SAID RAMADHANI KISSIMBA 

Tumieni uhuru wenu vyema 
Na Abuu Zaina, Iringa 

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 4  
Na Muhibu Said 

Mihadhara ya Wakristo yatawala Handeni 
Na Mwandishi Wetu, Handeni 

Ziara ya Kadinali Pengo Moro  
Na Mussa Ally, Morogoro 

Aonyesha ujuzi wa kutengeneza Trekta 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu wasizifanye sharia za dini kuwa nzito – Sheikh Mzonge 
Na Ashraf  Yusuf, Moshi 

Sengerema waomba msaada 
Na Idd Katimba, Mwanza 
 
Mafundisho ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi: 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matunzo ya mtoto mwenye lishe duni 

Matangazo 
 
 

 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita