AN-NUUR
Na.165 Jamadul Awwal 1419, Septembe 4 - 10, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
S.L.P. 55105, SIMU 181365, DSM 

TAHARIRI 

HAKI YA KUABUDU MASHULENI: 
Hoja ya uwingi isizuie haki ya wachache 
  

ZIPO haki za msingi za binadamu ambazo hazina bei wala hazitegemei ridhaa ya mtu yeyote. Na haki si fadhila ambayo mtu aweza kupewa na kupokonywa wakakati wowote. 

Uhai na kuishi ni haki ya msingi ya binadamu yeyote na katiba za nchi zote duniani hata zile za kidikteta zimeitambua haki hii japo kwa maandishi tu. 

Linaloandamana na haki hii ni haki ya mtu kulindwa yeye na mali yake. Mantiki ya haki hii ni kuwa uhai, heshima na mali ya mtu ni vitu vitakatifu. Uhai ni amana anayopewa mtu na Mola wake na hayupo yeyote aliyeidhinishiwa kumpora uhai huo bila sheria. 

Ndio maana tutaendelea kuhoji, kulikuwa na sheria gani iliyoidhinisha kuuliwa kwa Waislamu pale Mwembechai. Swali hili haliwezi kupata jibu maridhawa bila ya suala hili kufikishwa mahakamani. 

Damu ya watu imemwagwa, ni haki yetu wafiwa kuelezwa ni sheria gani ya nchi iliyo halalisha kukiukwa ile haki ya msingi ya kuishi watu wale. 

Haki nyingine inayoambatana na haki hii ni haki ya imani. Kwamba kila mtu ana haki ya kuamini dini atakayo, kuabudu na kuitangaza dini hiyo. 

Haki hiyo nayo si ya mjadala, fadhila wala yenye kutegemea ridhaa ya mtu. Kuitukuza siku ya Sabato ni moja ya mambo ya msingi katika imani ya watu wengine na hivyo ni haki yao ya kikatiba kupumzika siku hiyo. 

Kwa mantiki hiyo, ni makosa na kukiuka katiba kwa mamlaka yoyote kuihujumu haki hiyo kwa visingizio vyovyote viwavyo. 

Mfano hawezi kutokea mkuu wa shule akapanga mtihani ufanyike siku ya Jumamosi kwa kisingizio kwamba Wasabato ni wachache. Au akawazuia wanafunzi Wakatoliki wa bweni kwenda Kanisani siku ya Jumapili kwa hoja kwamba wengine wakipewa ruhusa hiyo huishia kijijini kunywa ulanzi. Inachoweza kufanya shule ni kuweka utaratibu wa kuwapata na kuwaadhibu hao wanaohujumu fursa hiyo na sio kuwanyima wengine haki yao. 

Ni kwa msingi huo huo hatutarajii Mkuu yeyote wa shule au sehemu ya kazi awazuie mabinti wa Kiislamu kuvaa hijab kwa kisingizio cha uchache wao au kuvaa sare. Wala hatutarajii kusikia wanafunzi Waislamu wazuiwe kwenda kuswali Ijumaa kwa hoja eti ni wachache na wanafunzi wengi Waislamu hawaswali. 

Suala la imani na ibada si jambo la kupigiwa kura, kwamba wengi wape. Ni haki ya msingi ya kikatiba hata akiwa mtu mmoja ni lazima haki yake hiyo iheshimiwe. 

Na tunadhani ni muhimu Masheikh wetu na Jumuiya za Kiislamu wachukue fursa hii kuwaelimisha waumini hasa hasa sehemu za kazi, mashuleni na vyuoni, juu ya haki zao hizi za msingi. 

Lakini ni muhimu vile vile serikali yetu ikawa makini juu ya masuala haya. Miongoni mwa mambo yanayochochea kuwepo mahusiano mabaya kati ya raia na serikali ni raia kuhisi wanaonewa, kupuuzwa na kudhulumiwa haki zao. 

Na ili kuzuia hali hiyo isitokee ni vyema yanapoibuka malalamiko yatizamwe kwa uadilifu na kama kweli wapo viongozi wanaokiuka katiba na maadili ya nchi wachukuliwe hatua za kisheria. 

Juu 
 

YALIYOMO
 
 
TAHARIRI 
HAKI YA KUABUDU MASHULENI: Hoja ya uwingi isizuie haki ya wachache 

Aliyeandika Yesu si Mungu bado akabiliwa na kesi 
Na Mwandishi Wetu 

Wazazi walia na Mkuu wa shule Mkwawa 
Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Serikali iache kudhulumu  Waislamu - Bakwata  
Na Mwandishi Wetu

KESI YA MIRATHI: Hukumu ya Jaji Agostino yatupwa 
Na Mwandishi Wetu 

Sumaye sasa atoa ‘waadhi’ Msikitini 
Na Mwandishi Wetu, Arusha 

Sekondari ya Kiislamu Sumbawanga, mtihani kwenu – Sheikh Akilimali 
Na Harun Rashid, Sumbawanga 

37 wasilimu  Mwanza 
Na Mwandishi Wetu, Mwanza 

Akamatwa kwa kusoma gazeti la ANNUUR ! 

MGOGORO WA CHWAKA NA MARUMBI: Serikali ya Dk. Salmin itafute ufumbuzi 
Na Mwandishi Wetu, Pemba 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 4 

Kwa nini walengwa wa mabomu wawe ni Marekani? 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Profesa amekosea kusema kwamba... 
Na A.M. Hamza 

Ugaidi ni ugaidi, hata wa Marekani ni ugaidi 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Dhana ya Udugu wa kiislamu 

UGAIDI: Chanzo si magaidi, ni dhuluma ya Marekani 
Na HASSAN KIMANGALE 

Jengeni familia bora 
Na Abuu Said, Iringa 

Tuwasaidie Waislamu kielimu na kiuchumi - Bi Zuhura 
Na SAID RAMADHANI KISSIMBA 

Tumieni uhuru wenu vyema 
Na Abuu Zaina, Iringa 

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 4  
Na Muhibu Said 

Mihadhara ya Wakristo yatawala Handeni 
Na Mwandishi Wetu, Handeni 

Ziara ya Kadinali Pengo Moro  
Na Mussa Ally, Morogoro 

Aonyesha ujuzi wa kutengeneza Trekta 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu wasizifanye sharia za dini kuwa nzito – Sheikh Mzonge 
Na Ashraf  Yusuf, Moshi 

Sengerema waomba msaada 
Na Idd Katimba, Mwanza 
 
Mafundisho ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi: 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matunzo ya mtoto mwenye lishe duni 

Matangazo 
 
 

 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita