AN-NUUR
Na.165 Jamadul Awwal 1419, Septembe 4 - 10, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Mihadhara ya Wakristo yatawala Handeni 
 
  • Wawateka mabinti wa Kiislamu 
  • Wanaharakati walilia tawi la Al-Malid 
Na Mwandishi Wetu, Handeni 

UTAFITI uliofanywa na vijana wanaharakati wa Kiislamu wilayani Handeni umegundua kuwa zaidi ya asilimia 95 ya wananchi wa Handeni ni Waislamu na zaidi ya asilimia 98 ya mihadhara iliyofanyika na inayoendelea kufanyika ndani ya wilaya ya Handeni ni ya Wakristo tu. 

Sababu hasa zinazosababisha Uislamu kuzorota na kushindwa kufanya mihadhara ya dini yao ni kukosekana kwa chombo madhubuti cha kutetea Uislamu na kuanzisha mihadhara ya kuwazindua Waislamu na wasio Waislamu kurudi kwenye Uislamu. 

Uchunguzi umeonyesha kuwa mfumko wa mihadhara ya Wakristo toka awali ilikuwa ikifanyika kwa wingi na kwakuwakebehi Waislamu kwa kusema kuwa mtu yeyote wa Handeni asiye Mkristo hasa asiye mlokole hataingia peponi, vile vile mihadhara ya Wakristo imekuwa ikiwadanganya watu wa Handeni kuwa Yesu ni Mfalme wa Handeni na Yesu ni Mungu. 

Halikadhalika, mabinti wa Kiislamu hudanganywa na hatimaye kufanya ufuska na kuozwa ndoa za haramu kwa vijana wa dini nyingine. Huu ni mpango wao maalum watu hao wa Handeni kuhakikisha kuwa wanafanya kila hila ili kufanya ufuska na mabinti wa Kiislamu mwisho wanawaoa kabisa kiharamu. 

Baada ya hapo huwapa mafunzo ya dini zao na kuwatumia katika mihadhara yao ili kuwapotosha mabinti wengine wa Kiislamu. 

Takwimu ndogo tuliyoifanya inaonyesha kuwa zaidi ya mabinti tisa wa Kiislamu wilayani hapa tayari wamepotoshwa na kuingia katika dini hiyo na wengine wanaosoma, kundi hilo linawanyemelea kwa kuwadanganya kuwa watawaoa na kuwajengea nyumba ili waingie kwenye mtego. Huu ni msiba mzito ndugu Waislamu popote mlipo duniani. 

Jambo jingine la kusikitisha ni kuona kuwa baadhi ya Masheikh wilayani Handeni hushiriki katika harakati za kuzuia mawaidha na mihadhara ya Kiislamu kwa mfano Ijumaa moja baadhi ya vijana wa kundi la Tabligh wa mjini Chanika walizuiliwa kutofanya kazi ya kutoa mawaidha baada ya sala ya Ijumaa. Imamu wa Msikiti huo wa Kijiji cha Kwenjugo alizuia ujumbe huo wa Mwenyezi Mungu bila ya sababu yoyote ile ya msingi, alieleza kwa uchungu Ustadh Yasini ambaye alikuwa ni miongoni mwa vijana waliokwenda huko. 

Kutokana na kero hizo zote, baadhi ya wanaharakati wilayani Handeni wamegundua kuwa ili kuondokana na kero hizo pamoja na kero nyingine, Waislamu ni muhimu sana kuanzisha tawi la Al-Malid ambalo litahakikisha kuwa linashirikiana kikamilifu na vyombo vyote vya Kiislamu vyenye msimamo pamoja na Waislamu katika kuamsha na kuutangaza Uislamu kwa njia za mihadhara. 

Ustadh Fikirini Salimu akizungumza na vijana wenzake mara kwa mara nje ya Msikiti wa wilaya huwaambia kuwa ili haki na nusra ya Waislamu iweze kupatikana kwa kasi Handeni upo umuhimu wa kuwasiliana na uongozi wa Al-Malid Taifa ili kufanya mihadhara ya mara kwa mara kwa kuanzia Handeni Mjini hadi vijijini. 

"Tusipofanya harakati hizi dada zetu watazidi kuziniwa na Makanisa yatazidi kushamiri Handeni. Majuzi baada ya mawaidha ya Sheikh Hamim Boza wilayani Handeni yamesababisha makundi ya mikutano ya Wakristo kufanyika kwa kasi wilayani Handeni kwa mbwembwe na kebehi kwa Waislamu. 

"Kwa hiyo sisi vijana wa Kiislamu pamoja na baadhi ya wazee wenye msimamo tunaomba kuwa popote walipo viongozi wa Al-Malid Taifa yaani Sheikh H. Boza, Riko, Mwaipopo, Mazinge, Hussein E. Feruzi, Kipozeo, Magezi n.k. msikie kilio chetu sisi Waislamu wa Handeni ili mje mapema kushirikiana nasi kuunusuru Uislamu wilayani Handeni" alimalizia Ustadh Fikiri. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 
 
TAHARIRI 
HAKI YA KUABUDU MASHULENI: Hoja ya uwingi isizuie haki ya wachache 

Aliyeandika Yesu si Mungu bado akabiliwa na kesi 
Na Mwandishi Wetu 

Wazazi walia na Mkuu wa shule Mkwawa 
Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Serikali iache kudhulumu  Waislamu - Bakwata  
Na Mwandishi Wetu

KESI YA MIRATHI: Hukumu ya Jaji Agostino yatupwa 
Na Mwandishi Wetu 

Sumaye sasa atoa ‘waadhi’ Msikitini 
Na Mwandishi Wetu, Arusha 

Sekondari ya Kiislamu Sumbawanga, mtihani kwenu – Sheikh Akilimali 
Na Harun Rashid, Sumbawanga 

37 wasilimu  Mwanza 
Na Mwandishi Wetu, Mwanza 

Akamatwa kwa kusoma gazeti la ANNUUR ! 

MGOGORO WA CHWAKA NA MARUMBI: Serikali ya Dk. Salmin itafute ufumbuzi 
Na Mwandishi Wetu, Pemba 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 4 

Kwa nini walengwa wa mabomu wawe ni Marekani? 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Profesa amekosea kusema kwamba... 
Na A.M. Hamza 

Ugaidi ni ugaidi, hata wa Marekani ni ugaidi 
Na Maalim Ali Bassaleh 

Dhana ya Udugu wa kiislamu 

UGAIDI: Chanzo si magaidi, ni dhuluma ya Marekani 
Na HASSAN KIMANGALE 

Jengeni familia bora 
Na Abuu Said, Iringa 

Tuwasaidie Waislamu kielimu na kiuchumi - Bi Zuhura 
Na SAID RAMADHANI KISSIMBA 

Tumieni uhuru wenu vyema 
Na Abuu Zaina, Iringa 

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 4  
Na Muhibu Said 

Mihadhara ya Wakristo yatawala Handeni 
Na Mwandishi Wetu, Handeni 

Ziara ya Kadinali Pengo Moro  
Na Mussa Ally, Morogoro 

Aonyesha ujuzi wa kutengeneza Trekta 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu wasizifanye sharia za dini kuwa nzito – Sheikh Mzonge 
Na Ashraf  Yusuf, Moshi 

Sengerema waomba msaada 
Na Idd Katimba, Mwanza 
 
Mafundisho ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi: 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Matunzo ya mtoto mwenye lishe duni 

Matangazo 
 
 

 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita