AN-NUUR 
Na.176 Shaaban  1419, Novemba 20 - 26, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Serikali yatakiwa iwachukulie hatua wauaji
 
  • Lindi, Newala, Mtwara wasisitiza msimamo wa Waislamu
  • Walaumu mikoa ya kusini kutelekezwa
Na Mwandishi Wetu

Wanawake wa Kiislamu mikoa ya kusini wameungana na wenzao wa sehemu mbali mbali nchini katika matamko ya kuitaka Serikali iwachukulie hatua waliohusika na mauaji Mwembechai. 

Wanawake hao wa miji ya Lindi, Newala, Mtwara, Nachingwea na Masasi, walitoa matamko hayo katika makongamano tofauti yaliyofanyika katika miji hiyo wiki iliyopita. 

Aidha waliazimia kuwa na mshikamano miongoni mwao na kuunda jumuiya itakayosimamia shughuli mbali mbali za kijamii kanda hiyo. 

Wakizungumza katika makongamano hayo, wahadhiri mbali mbali waliilaumu Serikali kwa kushindwa kuunda tume ambayo wamesema ingechunguza tukio zima la Mwembechai na kutoa taarifa ya kina kama ilivyokwisha wahi kufanywa katika matukio mengine yanayofanana na hili. Walihoji ni kwa vipi polisi wavamie msikiti, kupiga na kudhalilisha waumini ambako ni kinyume na katiba ya nchi, Serikali isione umuhimu wa kufuatilia suala hilo mbali ya kuwatuhumu waathirika na kuwasweka rumande miezi kadhaa kabla ya kuwafikisha mahakamani. 

Wakizungumzia kudumaa kwa mikoa ya kusini kimaendeleo, waliilamu Serikali kwa kuitelekeza mikoa hiyo tangu nchi ipate uhuru. 

Walitoa mfano wa ubovu wa barabara kuu ya Dar es Salaam hadi Liwale na kusema kwamba umechangia kwa kiasi kikubwa kuiweka nyuma mikoa hiyo. 

Walionyesha wasi wasi kwamba huenda kutelekezwa kwa mikoa ya kusini kunatokana na idadi kubwa ya wakazi wa kanda hiyo kuwa Waislamu. 

Makongamano hayo yaliazimia pamoja na mambo mengine kuandaa kongamano kubwa la kanda ya kusini mwakani 1999 kula kiapo cha kutokurudia makosa ya kuwaweka madarakani watu ambao hawako tayari kufanya uadilifu. 

Wakati huo huo, wanawake wa Kiislamu wilaya ya Newala wamechanga shilingi 20,000 kwa ajili ya marehemu Ustaadh Swaleh Isa na kijana Chuki Athumani aliyepooza baada ya kupigwa risasi na polisi Jijini Dar es Salaam. 

Marehemu Ustaadh Swaleh aliyepigwa risasi na kufa papo hapo katika maeneo ya Mwembechai Jijini alikuwa mzaliwa wa Lindi. 

Swaleh alipigwa risasi na polisi Februari 13, mwaka huu katika kile kilichodaiwa na viongozi kuwa ni jitihada za polisi "kujihami" dhidi ya mawe yaliyokuwa yakirushwa na waumini wa dini ya Kiislamu. 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
Maoni 
Kuwa na mawazo ya kufugwa tunajidharaulisha 

Sakata la mabucha  ya Nguruwe kuibuka upya 
Na Mwandishi Wetu  

Kondom sio kinga ya Ukimwi 

Bakwata yairushia polisi makombora Ngaramtoni 

MACHO YA SHUTUMA 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Serikali yatakiwa iwachukulie hatua wauaji 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya Msikiti wa Ngaramtoni 

Silaha yetu ni kura ya pamoja 
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC  U.S.A 

Anuani ya fikra 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Kuukaribisha mwezi mtukufu 

Tunahitaji "UN' ya Waislamu! 
Na Said  Rajab 

Kongamano la wanawake wa Kiislamu Newala lafana 

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 2 
Na Ustaadh Kupa Pazi Said 

Kesi mojawapo ya mihadhara yafutwa 

Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo 

Mahafali ya kidato cha nne Thaqafa: Wazazi wakumbushwa wajibu wao 

Wanafunzi Mwanza wadai haki za kuabudu mashuleni kwa usawa 
Na Iddi M. Katiba, Mwanza 

Saidianeni katika shida - Sheikh Abdallah 

Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja 

Someni  muiokoe jamii kimaadili 

Acheni Shirki 

Kesi nyingine ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa 
Na Muhibu Said 

Kusilimu kwa Wakristo kwaleta kero Mwanza 

Nzasa waomba msaada wa chakula, madawa 

Katibu wa Bakwata Moro ang'olewa Msikitini 

Masomo ya Dini ya Kiislamu  

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Umuhimu wa chakula katika shule za awali]  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita