|
|
Washitakiwa katika kesi hiyo walikuwa wakikabiliwa na tuhuma ya kutoa maneno yenye lengo la kukashifu Biblia Takatifu, Wakristo, Jeshi la Polisi na viongozi wakuu na kutishia usalama wa nchi. Watuhumiwa hao ni pamoja na Uliza Rashid (37), Swalehe Rashid (30), Ramadhani Mkwangu (30), Ally Majapa (42), Ally Athumani (40), Hamisi Swalehe (50) na Ramadhani Hamisi (30). Kufutwa kwa kesi hiyo kumezingatia ombi la Wakili wa washitakiwa, Bw. Twaha Taslima aliloliwasilisha mahakamani hapo hivi karibuni. Wakili Taslima aliiomba mahakama hiyo iwaondolee wateja wake shauri hilo kwa vile lilikuwa limekwishachukua zaidi ya mwaka mmoja mahakamani hapo bila kusikilizwa. Aidha, kutosikilizwa kwa kesi hiyo kwa muda wote kumetokana na mashahidi wa upande wa serikali waliotarajiwa kushindwa kufika mahakamani tangu upelelezi wa kesi hiyo ukamilike hapo Septemba 4, mwaka huu. Hata hivyo haikuelezwa ni kwa nini walishindwa kufika. Wakili Taslima aliiambia mahakama hiyo kuwa wateja wake wanayo haki ya kufutiwa kesi hiyo kulingana na kifungu cha 225 (5) cha sheria ya kanuni za mwenendo wa Jinai ya mwaka 1984 kinachoruhusu washitakiwa kufutiwa kesi husika iwapo itafikisha siku sitini (60) mahakamani bila kusikilizwa na pia mwendesha mashitaka wa serikali (PP) au mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa mkoa (RCO) kushindwa kutoa sababu za msingi za kuendelea kuwepo kwa kesi hiyo mahakamani bila kusikilizwa. Awali katika kesi hiyo, mwendesha mashitaka wa serikali, Inspekta msaidizi wa polisi, mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo, Bi. Cypriane William, alidai kuwa mnamo Septemba 23, mwaka jana (1997) huko Mwanyamala A, wilayani Kinondoni, Jijini Dar es Salaam, washitakiwa kupitia mhadhara wao walitoa maneno yenye lengo la kukashifu imani ya watu wengine. Wakati huo huo, kesi nyingine namba 1383/97 ya tuhuma ya kukishambulia
kituo kidogo cha polisi cha Msisiri, kilichopo maeneo ya Mwananyamala A,
Jijini inatazamiwa tena kuanza kusikilizwa hapo Novemba 24, mwaka huu,
katika mahakama ya Kisutu, Jijini Dar es Salaam.
Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo WAZAZI Waislamu wametakiwa kuwasadia na kuwaendeleza watoto wenye vipaji mbalimbali ili kuvikuza. Profesa Bukhet Kilonzo ametoa nasaha hizo hivi karibuni akiwa mgeni rasmi katika mahafali ya 15 ya shule ya sekondari ya Kiislamu ya Jabal Hira iliyoko mjini Morogoro. Profesa Kilonzo alisisitiza kwamba ni muhimu wazazi kuwa na mikakati madhubuti ya kuwalea na kuwapa elimu vijana wao kwani hilo ndilo jambo la muhimu zaidi katika Uislamu wao na maisha yao kwa ujumla. Profesa Bukhet Kilonzo ambaye ni mtaalam bingwa wa taaluma ya vijidudu vienezavyo maradhi kwa binadamu na wanyama (Sokoine University) ameuomba uongozi wa shule ya Jabal Hira kutoa motisha na kuwa na namna nzuri ya kukaa na waalimu ili kuepukana na tatizo la waalimu kuhama hama. Kwa upande wa wahitimu, Profesa Kilonzo aliwaasa wasitosheke na kiwango cha elimu walichokipata kwani hata yeye pamoja na uprofesa wake bado anatafuta elimu. Wengine waliokuwa wamehudhuria sherehe hizo ni Dk. Dihenga ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine na Imam wa Msikiti Mkuu wa Morogoro Sheikh Kairo.
Meneja wa shule ya sekondari ya Thaqafa ya mjini Mwanza Bw. Maruzuku Magongo alitoa ukumbusho huo wakati wa mahafali ya kidato cha nne shuleni hapo hivi karibuni mbele ya Bodi ya shule, wazazi na wanafunzi wenyewe kwenye ukumbi wa shule hiyo. Bw. Maruzuku aliyasema hayo mara baada ya mkuu wa shule hiyo Mwalimu Hamza Kayemba kumaliza hotuba yake iliyokuwa na malalamiko pamoja na masikitiko kwa mienendo mibaya inayoonyesha kushuka kwa maadili miongoni mwa jamii za sasa. Mwalimu Kayamba alisema kuwa Thaqafa sekondari Mwanza iliamua kufuata sheria za shule nchini na taratibu za malezi ya Kiislamu barabara na matokeo yake ni idadi kubwa ya wanafunzi kushindwa na kuamua kuacha shule, wengine kufukuzwa na baadhi yao kuhama, wazazi wengi hawako karibu na walimu ili kushirikiana kuwarudi watoto mara wafanyapo mambo ya hovyo. Alisema kuwa wanafunzi ambao walikuwa wanasheherekea kumaliza kidato cha nne mwaka huu shuleni hapo, walianza wakiwa 200 lakini watakaofanya mitihani ni 103 tu, waliobakia wote kwa sababu mbalimbali hawako shuleni Thaqafa. Alitoa ushauri kwa wazazi na walezi wa wanafunzi kwa ujumla kuwa karibu na uongozi wa shule na walimu kwa ujumla ili kushirikiana kuwarekebisha watoto ili wawe ni kizazi bora cha baadaye. "Kwa kuwa kidato cha nne si vyema siku kama hii kuita ni mafahali, kwani kazi iliyo mbele yao bado ni kubwa na inahitaji subira na nidhamu ya hali ya juu, miaka minne waliyokaa hapa Thaqafa Mwanza haitoshi kusheherekea ila iwape picha tu ya mwanzo mgumu wa vitivo vya elimu ya juu", Bw. Maruzuku alisema. Akikazia kampeni za sasa za taifa za uzinifu "salama" aliwashauri waachane kabisa na uasherati kwa ujumla wake. "Hakuna cha kondomu, maradhi ya zinaa mwisho wake ni kifo tu, lugha ya kuwa na mpenzi mmoja, tumia kondomu ni ya hatari mno, mtaangamia bure", alisema. Akimalizia hotuba yake, Bw. Maruzuku Magongo aliwaomba wazazi na walezi kwa pamoja kuwadhibiti watoto kutokuwa na muda mwingi wa kupoteza (free time) aliwashauri watoto kutopoteza muda kwenye magenge, kusoma magazeti ya kipuuzi na vichekesho ambavyo haviwasaidii chochote, vitabu vya matusi, vipindi vya upuuzi vya TV na video, pia waache kulala na uvivu ni vitu vya kupigwa vita sana. Katika hafla hiyo mzee Hezron Ndonho kwa niaba ya wazai alitoa shukrani za pekee kwa mkuu wa kitengo cha dini ya Kiislamu shuleni hapo kwa nasaha zake bora kabisa. Alisema kuwa anaamini kabisa kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.) hakusema maneno hayo ila aliambiwa na Allah (s.w.) kuwa sema, yaani atwambie sisi. Mkuu huyo wa kitengo cha dini (Mudir) Ustadh Mussa Juma Kondo katika nasaha zake aliwafafanulia Hadith ya Mtume isemayo: "Fanya mambo matato, kabla ya kufikwa na matano mengine". Aliyataja mambo haya kuwa ni: Utumie ujana wako katika mambo ya kheri kabla ya uzee, utumie afya yako katika mambo ya kheri kabla ya kifo, utumie wasaa wako (nafasi) kabla ya shughuli nyingi, itumie mali yako (utajiri) kabla ya umasikini, utumie uhai wako (maisha) kabla ya kifo. |
YALIYOMO
Maoni Kuwa na mawazo ya kufugwa tunajidharaulisha Sakata la
mabucha ya Nguruwe kuibuka upya
Bakwata yairushia polisi makombora Ngaramtoni MACHO YA
SHUTUMA
Serikali
yatakiwa iwachukulie hatua wauaji
Historia ya Msikiti wa Ngaramtoni Silaha yetu
ni kura ya pamoja
Anuani
ya fikra
Tunahitaji
"UN' ya Waislamu!
Kongamano la wanawake wa Kiislamu Newala lafana Umuhimu
wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 2
Kesi mojawapo ya mihadhara yafutwa Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo Mahafali ya kidato cha nne Thaqafa: Wazazi wakumbushwa wajibu wao Wanafunzi
Mwanza wadai haki za kuabudu mashuleni kwa usawa
Saidianeni katika shida - Sheikh Abdallah Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja Someni muiokoe jamii kimaadili Kesi
nyingine ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa
Kusilimu kwa Wakristo kwaleta kero Mwanza Nzasa waomba msaada wa chakula, madawa Katibu wa Bakwata Moro ang'olewa Msikitini Chakula
na lishe
|