AN-NUUR 
Na.176 Shaaban  1419, Novemba 20 - 26, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
MACHO YA SHUTUMA
Na Abu Halima Sa Changwa
 
 

Kaka yangu na rafiki zake, wiki mbili zilizopita, walikuwa wakija nyumbani na nyuso za furaha, wakiwa wanaelezana kwamba mambo ni mazuri mwaka huu, kwani kila mtihani walioupata ulikuwa ndio wenyewe. 

Niliifahamu mipango yao yote. Kaka yangu alipewa hela za kununulia mitihani hiyo na mjomba. Rafiki zake walipewa na wazazi au ndugu zao. 

Mjomba alipoambiwa kwamba mitihani aliyoitolea fedha ilikuwa ndiyo yenyewe, alifurahi mno. Nilibahatika kuwaona pia baadhi ya ndugu na wazazi wa wale rafiki zake kaka. Wote hao walikuwa wakifurahi na kushukuru Mungu kuwa fedha zao hazikupotea bure, na wakawa na matumaini kwamba watoto wao wangefaulu kwa maksi za juu, na pengine kupelekwa kwenye shule za "watoto wenye akili nyingi." 

Lakini mara bomu likalipuka. Mitihani ikafutwa. Kaka yangu, rafiki zake, mjomba wangu, pamoja na wazazi na ndugu wa rafiki zake kaka wakawa wameudhika kupindukia. Fedha zao zimepotea, kurudishiwa haiwezekani. Waliokula wamekula na walioliwa wameliwa. Ni ule ule usemi usemao: wajinga ndio waliwao! 

Cha kushangaza ni kwamba, wale waliokuwa na furaha walipopata mitihani, na wale waliotoa fedha, eti sasa hivi ndio wamegeuka kuwa WAZALENDO wa kumshutumu Waziri wa Elimu kuwa ndiye anayewajibika. Midomo yao iko wazi kwa kelele: "Ajiuzulu! Ajiuzulu!" Kha! 

Sasa mimi nauliza: Hivi huyu Juma Kapuya anaambiwa ajiuzulu kwa sababu kawaumbua vibaka au? Mimi nadhani, wale ambao hawakubahatika kupata mitihani, ilibidi wamshangilie sana bwana.... Ah! samahani....Profesa Juma, kwa vile amewaumbua vibaka hawa. Ama wale ambao wameliwa hela zao, au walibahatika tu kupata mitihani ile, wapige tu kelele kwa vile wameumbuka! 

Kama mimi na akili yangu ya kitoto, ambayo bado haijaathirika na umri, ningepewa nafasi ya kutoa ushauri, ningewaambia wahusika kwamba, vibaka ni wale watendaji, na sio Juma. Watendaji ni tangu wanaotunga mitihani, wanaochapa, wanaoiweka kwenye mabahasha, wanaoisafirisha kuitawanya mikoani, na vile vile wanaoipokea huko ikifika. Katika hatua zote hizo nilizozitaja, Juma yuko katika section gani? Labda na yeye alikuwa akiipachika mitihani hiyo kwenye mabahasha!!! Akili ya kitoto kama yangu hailikubali hili. 

Sasa kama mambo ndio hivi, yaani likipatikana kosa la kiutendaji tu basi waziri anajiuzulu, nadhani wa kwanza kujiuzulu angekuwa ni yule wa Wizara ya Mambo ya Ndani, maana watu wa nchi hii hawaishi kwa raha kwa jinsi vibaka na majambazi wanavyowasumbua na kuwaua. Vile vile, kila Wizara ina uozo wake kiutendaji, mbona mawaziri wake hawatajwi? Au kwa vile huyu Juma amenasibishwa na "waswahili" wenzake ndio maana imekuwa nongwa? Mnataka refa ambaye angeacha mcheze rafu zenu tu bila ya kupiga filimbi? He! 

Watu wazima mtaacha lini chuki, husuda, uzandiki, udini na unafiki? 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
Maoni 
Kuwa na mawazo ya kufugwa tunajidharaulisha 

Sakata la mabucha  ya Nguruwe kuibuka upya 
Na Mwandishi Wetu  

Kondom sio kinga ya Ukimwi 

Bakwata yairushia polisi makombora Ngaramtoni 

MACHO YA SHUTUMA 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Serikali yatakiwa iwachukulie hatua wauaji 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya Msikiti wa Ngaramtoni 

Silaha yetu ni kura ya pamoja 
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC  U.S.A 

Anuani ya fikra 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Kuukaribisha mwezi mtukufu 

Tunahitaji "UN' ya Waislamu! 
Na Said  Rajab 

Kongamano la wanawake wa Kiislamu Newala lafana 

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 2 
Na Ustaadh Kupa Pazi Said 

Kesi mojawapo ya mihadhara yafutwa 

Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo 

Mahafali ya kidato cha nne Thaqafa: Wazazi wakumbushwa wajibu wao 

Wanafunzi Mwanza wadai haki za kuabudu mashuleni kwa usawa 
Na Iddi M. Katiba, Mwanza 

Saidianeni katika shida - Sheikh Abdallah 

Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja 

Someni  muiokoe jamii kimaadili 

Acheni Shirki 

Kesi nyingine ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa 
Na Muhibu Said 

Kusilimu kwa Wakristo kwaleta kero Mwanza 

Nzasa waomba msaada wa chakula, madawa 

Katibu wa Bakwata Moro ang'olewa Msikitini 

Masomo ya Dini ya Kiislamu  

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Umuhimu wa chakula katika shule za awali]  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita