|
|
Aidha, uongozi huo wa Bakwata umetaka Mkuu wa Kituo cha Polisi Ngaramtoni Juu aache kuingilia masuala ya Waislamu kwani Waislamu wenyewe wana taratibu zao za kuendesha mambo yao. Katika barua yake ya Novemba 3, kwa mkuu huyo wa kituo, Katibu wa Bakwata mkoani Arusha, Alhaj Major Mohammed S. Mollel amedai kwamba Bakwata ina habari kwamba waumini wa Ngaramtoni wamekuwa wakiwekwa ndani bila ya dhamana kwa shinikizo la mkuu huyo wa kituo. Barua hiyo Na. BKT/AR/ARM/98/66 ambayo imenakiliwa kwa OCD Arusha na Usalama wa Taifa Arumeru, imeeleza kwamba kwa shinikizo la Wasomali na Waarabu wanaodai Msikiti ni mali yao amewafungulia mashitaka baadhi ya Waislamu kwa "kosa la kubughudhi waumini Msikitini". Aidha, barua hiyo imedai kwamba hao wanaomshinikiza kamanda huyo wa polisi ndio wachochezi wakubwa. Hivyo ikamtaka afanye kazi zake kwa uadilifu na kufanya uchunguzi kabla ya kukurupukia mambo vinginevyo hao wanaomshinikiza watamuacha pabaya. Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba Sheikh Shaaban Juma aliwekwa ndani kwa muda wa siku tatu kwa tuhuma kwamba anawabughudhi waumini. Hata hivyo uchunguzi zaidi umeonyesha kwamba Sheikh huyo amekuwa akichukiwa na baadhi ya watu ambao hawataki taarifa ya mapato na matumizi ya Msikiti yawasilishwe kwa waumini. Aidha, imeelezwa kwamba Sheikh Shaaban Juma amekuwa mstari wa mbele kuwaelimisha Waislamu juu ya shirki ya sihiri. Imedaiwa kwamba wanaozuia waumini wasijue mapato ya Msikiti wao pamoja na wasiopendezwa na makemeo ya Qur’an dhidi ya sihiri ndio wanaomtilia fitna Sheikh Shaaban. Juhudi za gazeti hilo kuwasiliana na uongozi wa polisi mkoani Arusha
dhidi ya tuhuma hizi hazikuweza kufanikiwa.
|
YALIYOMO
Maoni Kuwa na mawazo ya kufugwa tunajidharaulisha Sakata la
mabucha ya Nguruwe kuibuka upya
Bakwata yairushia polisi makombora Ngaramtoni MACHO YA
SHUTUMA
Serikali
yatakiwa iwachukulie hatua wauaji
Historia ya Msikiti wa Ngaramtoni Silaha yetu
ni kura ya pamoja
Anuani
ya fikra
Tunahitaji
"UN' ya Waislamu!
Kongamano la wanawake wa Kiislamu Newala lafana Umuhimu
wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 2
Kesi mojawapo ya mihadhara yafutwa Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo Mahafali ya kidato cha nne Thaqafa: Wazazi wakumbushwa wajibu wao Wanafunzi
Mwanza wadai haki za kuabudu mashuleni kwa usawa
Saidianeni katika shida - Sheikh Abdallah Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja Someni muiokoe jamii kimaadili Kesi
nyingine ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa
Kusilimu kwa Wakristo kwaleta kero Mwanza Nzasa waomba msaada wa chakula, madawa Katibu wa Bakwata Moro ang'olewa Msikitini Chakula
na lishe
|