|
Na.175 Rajab 1419, Novemba 13 - 19, 1998 |
|
Na Mujahid Mwinyimvua TANGU wiki kadhaa zilizopita, makala zetu za chakula na lishe zinazungumzia ugonjwa wa kansa na namna ya kuukabili kwa silaha ya chakula. Katika kuendeleza kusudio hilo, makala hii inatoa ujumbe juu ya lishe na kansa ya tumbo. Kansa ya tumbo ni tatizo linalotishia maisha ya watu kama zilivyo aina nyingine za kansa. Wataalamu wanasema kwamba katika nchi ambayo vyakula vya kila siku vya watu ni vile vilivyohifadhiwa kwa madawa (preservatives), vyenye chumvi (nyingi) na vilivyosindikwa (Pickled foods), idadi ya watu wenye ugongwa wa kansa (salatani) ya tumbo huwa ni kubwa. Ukweli wa jambo hilo uko wazi zaidi katika nchi ya Japan, ambayo wananchi wake wanatumia zaidi vyakula vya aina niliyoitaja hapo juu. Kwa mujibu wa taarifa za mwaka 1984, kansa ya tumbo ndiyo iliyokuwa inaongoza kwa kuua watu wengi zaidi ikilinganishwa na aina nyingine za kansa. Hata hivyo, wataalamu hao wanasema kuwa, katika miaka 25 iliyopita, ugonjwa wa kansa ya tumbo duniani umepungua kwa asilimia sitini (60%). Hii ni kwa sababu ya teknolojia ya kuhifadhi vyakula kwenye majokofu (refrigeration). Vyakula vikihifadhiwa kwenye majokofu (ubaridi) huweza kukaa siku nyingi bila ya kuharibika. Kwa hiyo, mahitaji ya kuhifadhi vyakula kwa kutumia njia zenye kusababisha kansa (kama njia ya kuweka madawa, chumvi, moshi, n.k.) yanapungua. Ili kupunguza uwezekano wa kupata kansa ya tumbo hasa inayosababishwa na vyakula tunavyokula, watu lazima wazingatie ushauri wa lishe ufuatao: Kwanza, watu waache kula vyakula vilivyohifadhiwa kwa kutumia madawa hasa ‘nitrites’ na ‘nitrates’. Katika utumbo wa mwanaadamu, madawa hayo yanapambana na vitu vingine vijulikanavyo kama ‘aminesi’. Kutokana na mapambano hayo vitu vyenye kusababisha kansa hutokea. Vitu hivyo vinaitwa ‘nitrosamines’. Siku hizi ni jambo jepesi kununua vyakula visivyokuwa na ‘nitrites’, ‘nitrates’ na madawa mengine ya hatari. Jambo la kufanya ni kusoma ‘lebo’ kabla ya kununua chakula chochote kilichotengenezwa (kiwandani). Pili, epuka vyakula vyote vilivyohidhiwa kwa kutumia chumvi na kukaushwa kwa moshi. Vile vile epuka kula mara kwa mara aina ya vyakula vijulikanavyo kama ‘pickled foods’. Tatu, watu waepuke kula kila siku vyakula vilivyokaangwa kwa mafuta au vile vilivyookwa kwa kutumia oven (grilled foods). Hii ni kwa sababu njia hizo za kutayarisha vyakula zinasababisha nyama na samaki kutoa vitu vinavyosababisha kansa ya tumbo. Hivyo basi, ni vema watu wakapendelea vyakula vya asili na vile vilivyopikwa au kuokwa kwa njia ambazo si za hatari. Nne, watu wajitahidi kula vyakula vyenye vitamini A, B na C na pia vyenye
madini ya ‘selenium’. Kwa ushahidi wa utafiti, vitu hivyo (vitamini na
madini) vinasaidia kuzuia kutokea kwa kansa.
|
YALIYOMO
Maoni Kuvuja kwa mitihani: Tuweni wakweli kwa nchi yetu Katibu
wa Baraza Kuu azikwa Dar
Ubabe
wa madhalimu kuzimwa:
MACHO
YA SHUTUMA
Wazo
mpachiko (Programmed mind)
Ta'azia: Abbas Shaaban Kilima 1938-1998 Mdahalo
kati ya Waislamu na Wakristo- 4
Siri
ya Miujiza
Umuhimu
wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo
Ifahamu
Madrasat Ghazal Muslim - Moro
Pamoja
na sala, tusimamishe zakah
Aina
za maudhi yaliyoharamishwa juu ya Muislamu
Israi
na Miiraji ni miujiza
Pamoja
na ahadi ya Serikali kuzifuta: kesi za mihadhara zaendelea mahakamani
Waislamu Uluguruni Moro wazama kwenye matambiko Imarisheni
miradi ya elimu - Prof. Mikidadi
Teknologia:
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (5)
Mafunzo
ya Qur'an
Chakula
na lishe
|