|
Na.175 Rajab 1419, Novemba 13 - 19, 1998 |
|
Na Mwandishi Wetu IMAMU na Khatib wa Msikiti wa Ma’mur Sheikh Talib amesema kwamba ucha Mungu na kumtegemea Mwenyezi Mungu ni silaha na kinga kubwa kwa muumini. Akifafanua nukta hii, Sheikh Talib alitoa mfano wa tukio la Mtume (s.a.w.) kutoka salama akielekea Madina wakati nyumba yake ilikuwa imezungukwa na wauaji. Alisema Mtume (s.a.w.) alisoma Surat Yaasin huku akiwatupia mchanga wauaji hao na wakalala usingizi huku Mtume (s.a.w.) akiwapita hawana habari. Sheikh Talib akihutubia siku ya Ijumaa iliyopita alisema kwamba tukio kama hilo limejirudia katika miaka ya hivi karibuni ambapo ndege za Wamarekani zilipongana wenyewe kwa wenyewe zikiwa angani zilipokuwa zinajaribu kuivamia Iran ili kuwaokoa Wamarekani waliokuwa wanashikiliwa mateka. Kama alivyofanya Mtume (s.a.w.) Sheikh Talib alisema kwamba Wairan walisoma Surat Yaasin na nguvu za Wamerakani zikayeyuka angani. Kwa mifano hiyo Sheikh Talib alisisitiza kwamba mafanikio na ulinzi kwa waumini unatoka kwa Mwenyezi Mungu na kuwaonya wale wanaokimbilia kwenye mizimu. Hata hivyo, Sheikh Talib aliwakumbusha waumini kwamba wasitarajie kupata mafanikio pekee katika mambo yao halikadhalika kupata ushindi tu kila wakati. Alisema kwamba ni katika utaratibu wa Mwenyezi Mungu kuwajaribu waumini ili wapate kujulikana wale waumini wa kweli na wale waongo. Katika kujaribiwa huko Sheikh Talib alisema kwamba matatizo mbalimbali yatawakuta waumini na watakaofuzu na kufanikiwa ni wale watakao subiri na kumtegemea Mwenyezi Mungu. Awali katika khutba yake Sheikh Talib alieleza falsafa ya miraj na Israh ambayo ni katika matukio muhimu katika historia ya Uislamu. Miraj ni safari ya Mtume (s.a.w.) kutoka Makka hadi Baitil Muqadas wakati Israh ni safari ya Mtume (s.a.w.) kutoka Baitil Muqadas hadi wingu wa saba na kurejea. |
YALIYOMO
Maoni
Katibu
wa Baraza Kuu azikwa Dar
Ubabe
wa madhalimu kuzimwa:
MACHO
YA SHUTUMA
Wazo
mpachiko (Programmed mind)
Ta'azia: Abbas Shaaban Kilima 1938-1998 Mdahalo
kati ya Waislamu na Wakristo- 4
Siri
ya Miujiza
Umuhimu
wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo
Ifahamu
Madrasat Ghazal Muslim - Moro
Pamoja
na sala, tusimamishe zakah
Aina
za maudhi yaliyoharamishwa juu ya Muislamu
Israi
na Miiraji ni miujiza
Pamoja
na ahadi ya Serikali kuzifuta: kesi za mihadhara zaendelea mahakamani
Waislamu Uluguruni Moro wazama kwenye matambiko Imarisheni
miradi ya elimu - Prof. Mikidadi
Teknologia:
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (5)
Mafunzo
ya Qur'an
Chakula
na lishe
|