|
|
|
UONGOZI wa shule ya sekondari ya Mazengo umetoa uwanja kwa vijana (wanafunzi) wa Kiislamu kujenga Msikiti katika eneo la shule. Akithibitisha taarifa hii, mwalimu mlezi wa vijana wa Kiislamu Bw. Lwamo alisema ni muda mrefu sana tangu uongozi kuwapatia uwanja huu kilichokwamisha ni uwezo mdogo na ubadilishaji wa uongozi kila mwaka. Hata hivyo akasema kwamba kwa sasa ramani ya jengo la Msikiti inachorwa. Katibu wa Vijana wa Kiislamu tawi la Mazengo, Ustaadh Kamana alisema amepatikana mfadhili wa kuchora ramani hiyo na wakati huu umewekwa utaratibu wa kupata fedha kwa kuchangishana. Awali shule ya Mazengo ilitoa jengo moja lililopo kando ya uwanja wa mpira ambalo ni jukwaa la michezo chini ya jengo hilo vipo vyumba viwili, hivyo uongozi ulitoa chumba kimoja iwe sehemu ya kusalia, chumba hicho kinaweza kusaliwa na watu wasiozidi arobaini. Ustaadh Kamana amewaomba wazazi, walezi na Waislamu kwa ujumla waelekeze sadaka zao katika ujenzi wa Msikiti huo. MWANAFUNZI mmoja wa Chuo cha Afya Bweni ameamua kabisa kutojiunga katika chuo cha Afya kwa madai ya kwamba hawezi kabisa kutembea kichwa wazi bila ya kuvaa hijabu wakati anapokuwa masomoni. Mwanafunzi huyo (jina linahifadhiwa) alichukua hatua hiyo baada ya kutolewa tangazo rasmi na uongozi wa chuo hicho cha Afya Bweni. "Hii ni sheria ya Chuo, na vile vile ni alama ya kuwatambua madaktari kwa hivyo hairuhusiwi kwa mwanafunzi yoyote kuvaa hijaabu wakati akiwepo chuoni na hususani akiwemo darasani; isipokuwa kuvaa kijialama kidogo kwenye kichwa ambacho kitakuwa ni kama utambulisho kwa wanafunzi wanaosomea udaktari na sio kuvaa hijabu kichwa kizima, sheria hiyo ipo zamani chuoni na sio kwamba imeanza leo au jana". Mwandishi wa habari hizi alipojaribu kuzungumza na mwanamke huyo alimwambia
ya kwamba Hijabu ni miongoni mwa sheria muhimu katika dini ya Kiislamu
na ni vazi ambalo humpatia heshima kubwa mwanamke wakati anapovaa.
|
YALIYOMO
Wanawake Dodoma wataka mtoto aliyepigwa risasi akatibiwe nje Kesi za Mwembechai zaanza kusikilizwa Dondoo za saikolojia: Tuonavyo mambo Waraka wa Baraza Kuu kuhusu Parole Inawezekana kufanyika mdahalo kati
ya Waislamu na wasio Waislamu?
Teknologia
Serikali ihamie Dodoma kwanza !
Mahafali ya AMSIR Iringa
Bihawana Sekondari wafungua Ijumaa Vijana Shinyanga watakiwa
kuwa mfano mwema
Vyeo visiwasahaulishe majukumu
yenu- Sheikh Abri
Jiandaeni na kifo – Sheikh
Abdallah
Semina zawazindua wanawake
Bukoba
Waislamu wanaomaliza Kidato
cha Nne Tanga waaswa
Ndugu Kamuhabwa ndiye mwenye
chuki na AN-NUUR
'Ukombozi wa mwanamke si kugeuzwa
biashara huria'
Polisi walinda amani katika
muhadhara wa Wakristo
Mazengo wapewa uwanja wa
kujenga Msikiti
'Ajiengua Chuoni Z'bar kwa
kutoruhusiwa kuvaa hijab'
Shairi
|