AN-NUUR 
Na.172 Rajab 1419, Oktoba 23 - 29, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Bihawana Sekondari wafungua Ijumaa

JUMUIYA ya Wanafunzi, Waalimu na Wafanyakazi wa shule ya Sekondari Bihawana wameanza kuswali Ijumaa shuleni hapo Oktoba 16, mwaka huu. 

Akiongea na mwandishi wa habari hizi, Mwalimu Mlezi wa Wanafunzi Waislamu Mwalimu Mwinjuma alisema kwamba kufunguliwa kwa Ijumaa hiyo kutawapunguzia wanafunzi safari ndefu kufuata Msikiti wa Ijumaa. 

Aidha, kutawaokoa kutokana na kupoteza vipindi zaidi ya vitatu kila wiki. 

Akisoma Khutba katika Ijumaa hiyo ya kwanza, Ustaadh Ramadhani ambaye ni mwanafunzi wa shule hiyo amewausia wanafunzi washikamane na tabia njema kama zinavyofafanuliwa na Uislamu. 

Aidha. aliwataka wasome kwa bidii ili waweze kutekeleza vyema wajibu wao wa Ukhalifa. 

Wakati huo huo, wanafujzi wa Bihawana wamehimizwa kushikamana na mafunzo ya Qur’an na Sunnah kwani ndio njia pekee ya kufaulu hapa duniani na akhera. 

Aidha, amewahimiza wanafunzi kufanya juhudi katika elimu kwani ndio amri ya kwanza na njia pekee ya kujipatia maendeleo. 

Akitoa nasaha zake katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha nne, Sheikh Abdallah aliwatahadharisha vijana kutokana na tabia za Kimagharibi zinazokwenda kinyume na Uislamu. Aidha aliwaonya wasiige tabia za kihuni kama vile kuvaa hereni, mikufu kwa wanamume, mambo ambayo yamelaaniwa katika Uislamu. 

Naye Sheikh Abdallah Ali wa Masjid Quba ameahidi kutuma wanafunzi wake kuendesha ibada hiyo. Pamoja ahadi hiyo, Sheikh Abdallah ameahidi kutoa vitabu vya dini pamoja na miswala kwa ajili ya msikiti huo. 


Vijana Shinyanga watakiwa kuwa mfano mwema
Na Jihad R. Saballa, Shinyanga

VIJANA wametakiwa kuwa mfano mwema kimaadili, kujielimisha zaidi, kujitolea mhanga kupigania dini yao na kuishi Kiislamu. 

Ujumbe huo ulitolewa hivi karibuni na Amiri Mkuu wa Bodi ya maendeleo ya Waislamu Shinyanga, Ustaadh Mohammed Issa katika hafla ya kuwaaga vijana Waislamu wa shule ya sekondari Uhuru iliyofanyika shuleni hapo. 

Katika ujumbe wake huo, Ustaadh Mohammed aliwakumbusha vijana hao kuwa wao ni wawakilishi wa vijana wenzao ambao hawakubahatika kupata elimu waliyoipata wao hivyo wana deni kubwa la kuonyesha shukrani zao kwa Allah (sw) kwa kutumia vyema elimu waliyoipata kwa ajili ya manufaa ya wenzao na kwa dini yao kwa ujumla. 

Vijana hao walikumbushwa pia kuwa mwisho wa jambo moja ndiyo mwanzo wa jingine, hivyo katu wasiridhike na kiwango cha elimu walichopata bali wajiendeleze zaidi katika viwango vya juu ili waweze kunufaika wao na kuunufaisha Uislamu kwa ujumla. 

Kuhusu suala la uvaaji Hijaab, Ustaadh Mohammed aliwasisitiza mabinti wa Kiislamu kuvaa vazi hilo, kulipenda na kujifakharisha nalo. Alisema ni aibu na jambo la kushangaza sana kuona hadi leo hii bado mabinti wa Kiislamu hawataki kutekeleza amri hiyo ya Mola wao aliyewaumba pamoja na kuondolewa khofu kwa wizara husika kuruhusu uvaaji vazi hilo. 

Kilichosisimua zaidi katika suala la hijaab ni pale aliposimama Mwalimu Masanja kutoa nasaha zake kwa vijana hao. 

Mwalimu Masanja ni mwalimu wa shule hiyo na katika nasaha zake hizo Mwalimu aliwasisitiza wanafunzi wake kuvaa vazi hilo kwa kuliita la heshima, linapendeza, na ngao ya mambo maovu. 

"Qur’an yenu na Hadith za Mtume (s.a.w) vinawaamrisha hivyo, Wizara ya Elimu ilisharuhusu vazi hili, sasa basi kwa nini hamtaki kuvaa ? Mna tatizo gani ?", aliuliza Mwalimu huyo na ambaye si Muislamu kwa mshangao na masikitiko makubwa. 

Kwa kauli hiyo ya Mwalimu Masanja walisikika baadhi ya wageni waalikwa wakisema, ikiwa hata wasio Waislamu wamechukua dhamana ya kutufikishia ujumbe wa kutekeleza dini yetu basi hatutokuwa tena na udhuru wowote mbele ya Allah (sw). 

Hadi sasa ni mabinti wanne tu shuleni hapo ambao wamekuwa wakivaa hijaab na watatu kati yao wanatarajia kumaliza shule mwaka huu. 

Umetolewa wito kumpa moyo na kumwombea dua binti pekee anayebakia akivaa hijaab shuleni hapo ili asikate tamaa kwa kuona kabaki yeye peke yake avaaye vazi hilo, na hasa ukizingatia mazingira yetu yalivyo sasa hivi. 

Vijana wa Kiislamu wanaotarajia kumaliza masomo yao mwaka huu shuleni hapo ni kumi na wawili (12) kati ya jumla ya wanafunzi themanini na wanne (84). 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Kuangukia makaa hakuna nafuu kwa aliye kikaangoni 

Wanawake Dodoma wataka mtoto aliyepigwa risasi akatibiwe nje 

Kesi za Mwembechai zaanza kusikilizwa 

Fitna ya Bakwata 

Dondoo za saikolojia: Tuonavyo mambo 

Waraka wa Baraza Kuu kuhusu Parole 

Inawezekana kufanyika mdahalo kati ya Waislamu na wasio Waislamu? 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Teknologia 
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (2) 
Na Hassan Omar 

Serikali ihamie Dodoma kwanza ! 
Na. Said Rajab 

Mahafali ya AMSIR Iringa 
Na Mwandishi Wetu 

Madrasatul Nnajjary Islamiya 

Ijue Madrasatul Riyaadh 

Bihawana Sekondari wafungua Ijumaa 

Vijana Shinyanga watakiwa kuwa mfano mwema 
Na Jihad R. Saballa, Shinyanga 

Vyeo visiwasahaulishe majukumu yenu- Sheikh Abri 
Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Jiandaeni na kifo – Sheikh Abdallah 
Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

Semina zawazindua wanawake Bukoba 
Na Nadhiru Ishengoma 

Waislamu wanaomaliza Kidato cha Nne Tanga waaswa 
Na Ibn Mohamed 

Ndugu Kamuhabwa ndiye mwenye chuki na AN-NUUR 
Mwandishi: Maalim Bassalah 

'Ukombozi wa mwanamke si kugeuzwa biashara huria' 
Na Japhary Lemah, Arusha 

Polisi walinda amani katika muhadhara wa Wakristo 
Na Badru Kimwaga 

Mazengo wapewa uwanja wa kujenga Msikiti 
Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

'Ajiengua Chuoni Z'bar kwa kutoruhusiwa kuvaa hijab' 
Na Seif Hamad Suleiman, Zanzibar 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Shairi 
Simlazimishe Yesu ukombozi wa ulimwengu (jibu) 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita